Polisi mwanamke ajipiga risasi nne Arusha

Polisi mwanamke ajipiga risasi nne Arusha

geprony

Member
Joined
Mar 17, 2009
Posts
23
Reaction score
1
Hello all

Natumaini kwa namna mmoja ama nyingine umesikia kilichotokea huko Arusha hivi karibuni, kama bado basi habari ni kwamba polisi mmoja wa kike amejipiga risasi kisa kakoromewa na maofisa wa usalama wa taifa baada ya kukosea kuongoza msafara wa mweshimiwa Rais.

Swali ninalojiuliza ni hili, hivi hawa vijana wa usalama wa taifa wana haki gani ya kumfokea na kumtishia askari mwenzao sababu tu kakosea kitu kidogo, pili je hawa usalama wa taifa wanafanya kazi ki-professional au ndio mjomba mjomba na kutumia mabavu na je mweshimiwa rais au usalama wa taifa wenyewe wame toa tamko lolote au angalau kufutilia kujua ukweli wa kashfa hii.

Mimi binafsi ningependa usalama wa taifa wafuatilie hili na pili kama ni kweli hiyo ndiyo sababu ya huyo askari kujiua basi waombe msamahani na askari huska wachukuliwe hatua za kisheria.
 
mimi nipo arusha na niko karibu sana na baadhi ya hao polisi,jana jion nilikua polisi central sijasikia hizo habari.labda tuambie ni kituo kipi cha polisi mkuu.
 
Hapo kwenye risasi nne ndo sijaelewa hivi inawezekana m2 ukajitwanga risasi nne ???
au alijimiminia kwenye mguu hizo risasi maana kama nikuanzia kwenye tumbo kuja juu akiweza sana kuzifyatua hazizidi mbili..
maana dah! nne?:roll:
 
Mtoa habari, habari hii ndiyo naisikia kwa mara ya kwanza na sijui rais alikuwepo lini Arusha na msafara uliongozwa vibaya wapi? Tafadhali hebu tupe habari kamili ili tuweze kuchangia. Au umetunga hii habari au umeoanisha na habari iliyotokea Musuma 1-2 years ago?
 
Geprony hoja ulioitoa imeeleweka ila mwishoni sikuelewi. Inakuwaje hao hao unaowatuhumu ndio tena wachunguze jambo hilo? Nashani ungesema an independent body ilichunguze. Kesi ya nyani mpelekee ngedere --wapi na wapi...
 
Mh Arusha? huyu jamaa kachanganya na ile ya kule kwa kina mura
 
Huyu mtoa habari huenda anachanganya madawa...labda ni ile ya kule tarime ya mwaka jana, kwa Arusha hatujasikia lolote hata tetesi pia hazipo mtaani ngoja tuendelee kumsikiliza....:coffee:
 
Fanya utafiti kabla ya kutoa taarifa maana ukisikiliza watu wasio na habari za uhakika na wewe ukachukulia ni habari hapo sio,source ni wapi ?
 
Mkuu umetumia muda we tu kusoma uongo kweli!!!!!Tafuta ustaarabu ukafanye kazi ya uafisa uhusiano TANESCO manake unafaa
 
Umepotosha uma kwa kukurupuka Nimekusamehe bure!
 
Napenda umakini wenu wa kuangalia tarehe ya tukio. Lakini ndugu yetu hapo juu alichokitoa kidogo naona hakijakaa sawa. RISASI NNE kwa mtu kujipiga labda atatumia mitambo James Bond au Rambo, maelezo kuwa alijipiga mwenyewe kweli akilini yanaingia.
 
Swala la usalama ktk msafara wa Rais siyo kitu cha kufanyia mchezo wala mzaha na mtu yeyote aliyekabidhiwa jukumu la kutekeleza.

Neno kukosea kwa bahati mbaya ni kitu ambacho hakitakiwi kuwepo na tafsiri yake ni uzembe kwa sababu askari kabla ya kwenda kuongoza msafara wanapewa maelekezo juu ya nini cha kufanya
 
Hapo kwenye risasi nne ndo sijaelewa hivi inawezekana m2 ukajitwanga risasi nne ???
au alijimiminia kwenye mguu hizo risasi maana kama nikuanzia kwenye tumbo kuja juu akiweza sana kuzifyatua hazizidi mbili..
maana dah! nne?:roll:
Anapiga ile kitu tunaita rapid!!!!
 
hivi hizi thread za mwaka 2011 zianaibukaje kwenye new post?
Na bado watu wanacoment vitu invalid? au ni mwendelezo wa hiyo hadithi/story

Mhariri
Paw
 
Back
Top Bottom