Polisi Makete waua mteja wa benki

Polisi Makete waua mteja wa benki

Askari yupo lindoni bank anahusiana vipi na maswala ya uvaaji elementi hii inaonyesha ni jinsi ganijeshi la polisi wanavyojichukulia sheria mkononi Mwenyezi mungu peleka siku haraka 2015 tufanye maamuzi sahihi
 
Kwa wenye akili tambuzi, shida hapa sio polisi bali ni KIKWETE!!!!!!
 
mmmhhh...hii nchi inakoelekea tutakuja kupigana na kumwaga damu..halafu utashangaa hilo liuaji linahamishwa kituo...
mmhhh eeh MUNGU ibariki TZ
 
Juz jumamosi nlipita nmb njombe nkakuta watu wamesimama mtandao ulikuwa unasumbua,askari alikuwa anapita pita wazee flani wakaanza kusema hapa bora kuondoka huyu askari anaweza kumpiga mtu risasi.
Kwa ufup kuna haja ya askar polisi hasa hawa vijana kutoruhusiwa kutumia silaha za moto na badala yake watumie virungu na kwa vile mabenk ni sensitive areas awepo askari mmoja mkomavu ambaye ndo atapewa silaha kwa sababu za usalama wa benk.
 

.....“Kila mtu ana Haki ya kuishi, haki ya uhuru, na haki ya kulindwa nafsi yake”...

.....Roho ya binadamu usiifananishe na Mnyama...

..kodi zetu zina kazi nyingi za kufanya ikiwemo kumtengenezea mazingira mazuri ya kazi huyo mwalimu....
but not the bullet!!!


RIP MWALIMU
 
Hii ni barabara kuelekea Demokrasia, kweli na heshma juu ya haki za binadamu. Sote tutakufa, Mwl huyu amelazimishwa kutangulia mbele ya haki. Matukio km haya hayakubaliki, Serikali ikikaa kimya Mungu ataipiganania familia ya marehemu dhidi ya watu wenye mamlaka ya kuchukua hatua bali hawachukui. R.I,P

Watanzania tusibaki kulalamika tu bali TUCHUKUE HATUA.KWANZA TUTAKE MATAMKO KUTOKA TAHOSSA,CWT,TUCTA NA WADAU WA ELIMU NA HAKI ZA BINADAMU.KUPOTEA KIZEMBE KWA RASILIMALI MWALIMU NI UHUJUMU,HIVYO MOJA KWA MOJA JESHI LA POLISI LIMEJENGA UHASAMA NA KADA YA WALIMU.NA NINYI WALIMU WA NCHI HII UNDENI INDEPENDENT TEACHERS MOVEMENT[ITM] ILI MSIKIKE KWANI HAMTASIKIA MATAMKO YA HAYO MACWT AU LITAHOSSA MAANA MNAJUA MALENGO YAO NI NINI.NCHI HII ITAKOMBOLEWA AU KUDUMAZWA NA MWALIMU[SIKU ITAKAYOITISHWA MAANDAMANO YA MWALIMU NDIYO SIKU YA UKOMBOZI TANZANIA].ACHA KULALAMIKA MTANZANIA,CHUKUA HATUA.BINAFSI NIMECHOKA KUSIKIA MAUAJI YA RAIA KATIKA NCHI HII TUKUFU ILIYOPATA UHURU WA BENDERA PASIPO KUTUMIA MTUTU WA BUNDUKI,JE KWA NINI TUTAFUTE UHURU WA KWELI NA MAENDELEO YA KWELI KWA VITU VIZITO NA VYENYE NCHA KALI? Kwa mtu yeyote anaye fikiria kulinda amani kwa kuficha matukio mabaya katika zama hizi za globalisation ambapo TRANSPARANCE IPO JUU NI SAWA NA MTU ANAYEFICHA MARADHI AMBAPO KIFO.........TUSIKUBALI TENA KUPOTEZA MASHUHUDA WA KUSHEREHEKEA UHURU WA KWELI MWAKA 2015,HIVYO KILA MTANZANIA AWE MLINZI WA MWENZAKE MAANA POLISI YA LEO NI ADUI WA RAIA NA SI MLINZI WA RAIA TENA.ALAMSIKI!
 
Nafikiri wakazi wa mkoa wa Mbeya wanatakiwa kugomea maiti hiyo kuingia mkoani humo hadi kuwe na uwajibikaji ndani ya Polisi na Wizara ya Mambo ya Ndani. Na hatu wa Makete wanatakiwa kusimamia haki hadi kupatikane jibu la huu unyama. Sina chembe ya ukabila bali huu ni upuuzi mtu kuondoa uhai wa mtu kwa kosa la kijinga.
 
mwangosi ni wa mbeya, ulimboka mbeya, ticha naye kutoka mbeya polisi na wanyampala kulikoni????

Eti kura za Mbeya ndizo hutoa Mshindi wa kiti cha Rais ha TZ.WATAZALIWA AKINA CASTO 2,000,000 MBEYA.RIP TICHA.
 
Kama hiyo shule aliyokuwa anafundisha marehemu ni miongoni mwa zile zenye walimu wawili, ina maana atakuwa amebakia mwalimu mmoja, sasa sijui hiyo shule itakuwa na division zero ngapi mwakani!

Tume ya Pinda iorodheshe matukio ya walimu kuuawa na polisi kama moja ya sababu za kuporomoka kwa elimu nchini
 
siyo bangi mkuu chunguza vzur chanzo cha tatizo man coz hil tatizo linajirudidia hamna jipya askar wa kikwete wamechakachuliwa
Mimi nimeona bangi imekuwa ikivutwa mno na askari vijana na nenda kwenye vijiwe vya pool table karibu na kambi za polisi,ongea na vijana wa hapo.
Kama kuna jambo jingine ongeza katika mtitiriko huo
 
Askari yupo lindoni bank anahusiana vipi na maswala ya uvaaji elementi hii inaonyesha ni jinsi ganijeshi la polisi wanavyojichukulia sheria mkononi Mwenyezi mungu peleka siku haraka 2015 tufanye maamuzi sahihi

Mkuu askari ni mlinzi wa amani hivyo popote anapokuwa anaruhusiwa kuhakikisha amani inatawala bila kusababisha madhara kwa wananch,askari alipaswa kumwelekeza marehemu nini cha kufanya na si kumuua, kitendo kilchofanywa na askari huyu ni mwendelezo wa vitendo vinavyofanywa na polisi academia wale wa enzi za mkapa mpaka JK,
Ukiiangalia hii picha vizuri utagundua kuwa marehemu alipigwa risasi mgongoni akiwa amempa kisogo muuaji tofauti na maelezo ya kamanda kuwa alitaka kumgonga askari.
 
dah!!ama kweli tuendako ni hatali tupu!!huyo mwalimu alikuwa akibomoa ATM,hadi kupigwa risasi? jamani,ninashawishika kuamini kuwa huyo askari alikuwa kalewa pombe kali. RIP TEACHER
 
Back
Top Bottom