Polisi kushiriki ualifu

Daudi Mchambuzi

JF-Expert Member
Nov 25, 2010
62,204
128,020
Hili ni moja kati ya matukio 1000 yanayofanywa na askari wa jeshi la polisi.
Iko hivi, kuna jamaa nilipata kusoma naye kitambo na sasa ni polisi kitengo cha FFU.
Juzi polisi huyu kaniambia kuwa, huwa anakodisha silaha yake kwa majambazi wakati wa lindo usiku (hasa akipangwa bank) na asubuhi hurejeshewa silaha yake na kitita cha laki mbili mpaka tatu kutoka kwa majambazi hayo.
Hakuishia hapo, polisi huyo alizidi kunidokeza kuwa wanapoishiwa na pesa za matumizi huwa wanachukua silaha wakati wa lindo mida ya jioni na kuvaa makoti makubwa kama raia na kuvamia maduka makubwa ya biashara za jumla wakati wa kufunga na kutishia kwa silaha hizo za jamuhuri na kupora fedha kutoka ktk duka husika.

MY TAKE:
Polisi wetu wakiwa huko mafunzoni hufundishwa utii wa uwoga na wanapewa treatment mbaya sana kiasi cha kuwafanya kuwa na roho mbaya na ya kikatili badala ya kuwa waaminifu na watii wa sheria.
Mafunzo ya ukatili wanayofundishwa askari wetu yanawafanya walinzi hawa wa usalama wa raia na mali zao kukengeuka na kuwa majambazi kwa kujaribu kujikwamua kwenye umaskini kwa kutumia ukatili uleule waliofunzwa huko CCP.
Swala la mafunzo ya askari na malipo yao litazamwe upya.
Askari anayelipwa laki mbili unusu kwa kazi ya kulinda bank yenye billions of money lazima awe mwizi.
Kwa kifupi polisi ndo wezi hapa tanzania.
 
Hili ni moja kati ya matukio 1000 yanayofanywa na askari wa jeshi la polisi.
Iko hivi, kuna jamaa nilipata kusoma naye kitambo na sasa ni polisi kitengo cha FFU.
Juzi polisi huyu kaniambia kuwa, huwa anakodisha silaha yake kwa majambazi wakati wa lindo usiku (hasa akipangwa bank) na asubuhi hurejeshewa silaha yake na kitita cha laki mbili mpaka tatu kutoka kwa majambazi hayo.
Hakuishia hapo, polisi huyo alizidi kunidokeza kuwa wanapoishiwa na pesa za matumizi huwa wanachukua silaha wakati wa lindo mida ya jioni na kuvaa makoti makubwa kama raia na kuvamia maduka makubwa ya biashara za jumla wakati wa kufunga na kutishia kwa silaha hizo za jamuhuri na kupora fedha kutoka ktk duka husika.

MY TAKE:
Polisi wetu wakiwa huko mafunzoni hufundishwa utii wa uwoga na wanapewa treatment mbaya sana kiasi cha kuwafanya kuwa na roho mbaya na ya kikatili badala ya kuwa waaminifu na watii wa sheria.
Mafunzo ya ukatili wanayofundishwa askari wetu yanawafanya walinzi hawa wa usalama wa raia na mali zao kukengeuka na kuwa majambazi kwa kujaribu kujikwamua kwenye umaskini kwa kutumia ukatili uleule waliofunzwa huko CCP.
Swala la mafunzo ya askari na malipo yao litazamwe upya.
Askari anayelipwa laki mbili unusu kwa kazi ya kulinda bank yenye billions of money lazima awe mwizi.
Kwa kifupi polisi ndo wezi hapa tanzania.

naunga mkono mkuu. me pia kuna jamaa yangu mmoja nilisoma naye a level tabora kwa bahati mbaya akafukuzwa kwa uvutaji wa sigara na bangi. baada ya hapo alijiunga na jeshi la polisi,nikiwa chuo dar nilikutana naye akiwa cid wa kwenye ma tzr. duuuh,huyu jamaa ni soo kwani story alizonipigia ni hatari sana. wanaua raia na kuwanyang'anya pesa kisha wanasema ni jambazi,wanakodisha silaha ile mbaya,wanasindikiza mizigo ya wizi kwa kutumia defenders zao,wanakamata madawa ya kulevya then wanayauza tena kwa wauzaji wengine,wanawajua vizuri sana majambazi na wauza madawa na ndio washirika wao wakubwa! askari wa bongo ni kama askari wa kwenye movie za kihindi miaka ile,mchana askari lakini usiku jambazi.
 
naunga mkono mkuu. me pia kuna jamaa yangu mmoja nilisoma naye a level tabora kwa bahati mbaya akafukuzwa kwa uvutaji wa sigara na bangi. baada ya hapo alijiunga na jeshi la polisi,nikiwa chuo dar nilikutana naye akiwa cid wa kwenye ma tzr. duuuh,huyu jamaa ni soo kwani story alizonipigia ni hatari sana. wanaua raia na kuwanyang'anya pesa kisha wanasema ni jambazi,wanakodisha silaha ile mbaya,wanasindikiza mizigo ya wizi kwa kutumia defenders zao,wanakamata madawa ya kulevya then wanayauza tena kwa wauzaji wengine,wanawajua vizuri sana majambazi na wauza madawa na ndio washirika wao wakubwa! askari wa bongo ni kama askari wa kwenye movie za kihindi miaka ile,mchana askari lakini usiku jambazi.

Haya yote ni kwa sababu ya serikali ya jk legelege.

Lawama yote ni yao yote!
Watatumaliza hawa majambazi police.
 
Nakubaliana na wewe kabisa, mi nimeshashuhudia matukio matatu ya wizi wa magari na kwa asilimia kubwa polisi ndio wanahusika na wizi huo moja kwa moja.
 
ni kweli mkuu kakaangu siku moja usiku alivamiwa na majambazi wakampora vitu kadhaa vya thaman. Akaripoti polisi lakini kila akipojaribu kufatilia upelelezi polis walimjibu bado.siku ya tatu ndipo askari mmoja bila aibu akamwambi atoe posho vitu vinaweza kupatikana.ikabidi atoe lakini huku akiwa amekata tamaa cha kushangaza asubui wakampigia sim na kumwambia aje atambue vitu vyake kufika pale akakuta ndo vilevile japo vingine walikua wameshaanza kuviuza lakini mwizi hakumuona hata mmoja. Na inasamekana wezi wote polis wanawafaham awe mdokoz mwizi au jambazi kwa hiyo wizi ukifanyika wenyewe hawahangaiki ni kunyosha kwenye kundi ambalo watahis limehusika au wanawapigia sim .kweli tz ni zaidi ya ujuavyo
 
Back
Top Bottom