Komeo Lachuma
JF-Expert Member
- Oct 31, 2014
- 11,173
- 22,772
Kumezuka mtindo askari waliovaa mavazi kama ya FFU combat za kijani kukamata magari kwa visingizio mbalimbali.
Wengi pia hukamata waendesha boda boda na kuwakung'uta mifuko yaani kuwapiga mkwara watoe rushwa. Pichani askari wawili wa aina hiyo wakiwa wanazunguka zunguka kutafuta wateja maungio ya barabara inayotoka Karume na inayotoka Veta Chang'ombe.
Ukivuka tu reli kama umetoka ile barabara inayotoka Ilala, Karume ikapita Machinga Complex kukutana na Nyerere Road.
Ni mara nyingi hawa askari huwa wanapita wakiwa na silaha kutafuta tafuta watu wa kuwapiga mkwara na kupewa rushwa.
Tabia hii naomba niulize kwa mamlaka je hawa FFU pia hufanya kazi za traffic? Maana mara nyingi nimewakuta hata wakisimamisha magari na kukagua. Lakini cha kujiuliza hawana hata zile mashine za kutoa risiti wakilipwa pesa.
Je hawa wamehalalishwa kufanya haya wayafanyayo? Ni nani anapasea kukamata raia kwa makosa ya vyombo vya usafiri au madereva barabarani?
Wengi pia hukamata waendesha boda boda na kuwakung'uta mifuko yaani kuwapiga mkwara watoe rushwa. Pichani askari wawili wa aina hiyo wakiwa wanazunguka zunguka kutafuta wateja maungio ya barabara inayotoka Karume na inayotoka Veta Chang'ombe.
Ukivuka tu reli kama umetoka ile barabara inayotoka Ilala, Karume ikapita Machinga Complex kukutana na Nyerere Road.
Ni mara nyingi hawa askari huwa wanapita wakiwa na silaha kutafuta tafuta watu wa kuwapiga mkwara na kupewa rushwa.
Tabia hii naomba niulize kwa mamlaka je hawa FFU pia hufanya kazi za traffic? Maana mara nyingi nimewakuta hata wakisimamisha magari na kukagua. Lakini cha kujiuliza hawana hata zile mashine za kutoa risiti wakilipwa pesa.
Je hawa wamehalalishwa kufanya haya wayafanyayo? Ni nani anapasea kukamata raia kwa makosa ya vyombo vya usafiri au madereva barabarani?

