Polisi apigwa kitu kizito na kupoteza fahamu katika mapambano na wachimbaji wadogo

nyampanaga

JF-Expert Member
Nov 16, 2012
1,104
559
Wakuu wa Fikra,

Jana majira ya jioni kulitokea mapigano makali kwenye mgodi wa Almas wa Mwadui, Shinyanga kati ya Polisi na wachimbaji haramu maarufu kwa jina la WABESHI ambao walivamia eneo la mgodi huo nakuanza kuchimba mchanga wa madini kwa nguvu.

Katika kadhia hiyo askari polisi mmoja alipigwa na kitu kizito kilichorushwa na Wabeshi kwa kutumia Kombeo na kuzimia na amelazwa katika hospitali ya mgodi huo.Polisi walilazimika kuongeza nguvu kutoka mkoani, na wilayani Kishapu.

Mapambano yaliendelea mpaka saa 6 usiku na kupelekea wabeshi wapatao 10 kutiwa nguvuni na mmoja kati yao amelazwa katika hospitali ya mgodi huo baada ya Polisi nao kumpiga kwa vitu vizito mara walipomtia nguvuni.

Source: Kaka yangu ambaye ni Mwalimu pale Mwadui A Primary School
 
Hope hakikuwa chenye incha kali au kizito sana watapona,hivi huko mwadui wachimbaji wadogo hawajatengewa eneo lao la kuchimba au wanalo tamaa tu ndo inawatesa!
 
Hope hakikuwa chenye incha kali au kizito sana watapona,hivi huko mwadui wachimbaji wadogo hawajatengewa eneo lao la kuchimba au wanalo tamaa tu ndo inawatesa!

wewe wakikutoa kwenye bonde la rufiji na kukupeleka dodoma ukalime mpunga utakubali?
 
Nahisi JF tumewapendelea sana Polis kwa sasa napendekeza heading ziwapendelee zaidi raia kwenye machafuko kama haya
 
mchanga wa block B,namba 8 sio mchezo.

Jamaa wanaijua sana almasi,heshima kwa wabesh wote popote walipo ndani ya mwadui,maganzo na kolandoto pia ndani ya kishapu.
 
wewe wakikutoa kwenye bonde la rufiji na kukupeleka dodoma ukalime mpunga utakubali?

Perfect answer Mkuu.. Na ndio tatizo kubwa la viongozi bogus wa bongo.. Yaani eneo lenye madini wanatoa kwa wawekezaji uchwara halafu sehem ndogo ambayo wanajua haina madini ndo wanawapatia wachimbaji wadogo..
 
Back
Top Bottom