Polisi ang'olewa meno sita Shinyanga

Wasukuma mmenipa raha sana! Kama kuna chance ya kulifadhiri kindi la Wabeshi mm ntachangia ili mlijenge Taifa hili.

Subiri nitatuma namba sasa hivi ili tuanze Michango. Hata mimi inaniuma saaana.
 
Meno yatashonwa kwa opp,na atarudia hali yake.na zaidi ataongeza mazoezi ili siku nyingine anapoenda kutuliza vurugu awadunde kwa hasira mpaka awatoe kiny esi.bado hawajapata ushindi kwenye haki wanayoitafuta sana sana matatizo tu,maana wameishakamatwa.

Alikuwa mjanja kwa kumlenga ffu na kumtoa meno,ila kawa mjinga tena kwa kuruhusu wamkamate.kapoteza mchezo.

Siku nyingine awe anarenga vizuri.
 
Du, Mkuu MZIMU, kwa jinsi ulivyozitoa "Likes" hapa naona hii habari ya FFU kutolewa meno inakuua kwa raha! Sishangai, maana tumezoe FFU kutoa watu meno, leo hii nao limewakuta, tena meno sita kwa mpigo! Hiyo itakuwa ni matatu juu matatu chini. Naona alikuwa akicheka wakati anapiga watu. Sasa reception mdomoni hakuna tena.
 
Hii taarifa nimeipenda sana, ila huyu mrusha kombeo ningemjua ningempa mbinu ya ziada ili next time anaporusha apige na kung'oa meno yote angalau haya mapoliccm yatumie akili.
Kilichoniudhi ni kuwaona watu wenye ardhi yao wanaitwa wachimbaji haramu.
Mungu atalipa tu na meno yatazidi kuwatoka, na mengine huko Dodoma hakukaliki kabisaaa
Huyo jamaa anashabaha aisee. Angepatikana siku moja arushe ling'oe meno ya pinda ili nae aonje utamu wa kupigwa ila namuombea asipate ugonjwa wa tezi dume maana alivyotuudhi hatutampeleka nje kutibiwa kwasababu zote wamebeba watu wa escrow
 
mnaoshabiki polisi kuumizwa ni wajinga na pumbavu sana ingetokea jambazi kakuvamia usingepiga simu polisi? mbona k
ila siku mmepanga foleni vituoni mkihitaji msaada wao sometimes it better to think before you act in anything b'se at end it will be seen you are crazy.. .

pole sana askari ulikuwa unatekeleza wajibu wako wa kulinda usalama wa ndani ya nchi...




Kwa nilivyowaelewa wananchi Ni hasira za kuporwa Mali zao na kuonekana kuwa wao Ni wezi na mzungu ndio mmiliki halali mtu anachimba miaka mitano bure baada ya hapo anachimba mwaka mmoja na kutangaza kuuza kampuni kwa mtu mwingine halafu anakaa miaka mitano tena bila kulipa kodi, Nibora tuwaachie watanzania wazawa wachimbe najua asipolipa kodi atanipa tenda ya kumjengea nyumba,atafungua miradi mbalimbali na nitapataa kazi, halafu Ni mswahili mwenzangu lakini mzungu na fisadi pesa zao hazikai nchi hii
 
Mhhhh hiyo hatari,huyu Iddi Makame yaonekana Ni mpemba,huyo aliyerusha hiyo kombeo kazi anayo..
 
Kumetokea tukio la aina yake katika mgodi wa madini ya almasi wa Mwaduiuliopo katika wilaya ya Kishapu mkoani Shinyanga ambapo askari polisi wa kikosi cha kutuliza ghasia wa jeshi la polisi mkoa wa Shinyanga Pc Idd Makame(25) amejeruhiwa vibaya mdomoni kwa kung'olewa meno sita baada ya kupigwa jiwe kwa kutumia kombeo (kwa lugha ya kisukuma Nh'ago) na watu wanaodaiwa kuwa ni wachimbaji haramu wa madini katika mgodi wa Mwadui wakati akitimiza wajibu wake wa kuhakikisha usalama wa raia na mali zao.

Tukio hilo limetokea Novemba 21,2014saa mb ili na robo usiku katika eneo la Tanex katika mgodi huo wakati askari huyo akiwa na askari wenzake wakiongeza nguvu baada ya askari wa kampuni ya ulinzi ya Zenneth inayolinda mgodi wa Mwadui kushindwa kuwadhibiti wachimbaji wadogo wa madini maarufu "Wabeshi" waliotaka kuingia kwa nguvu mgodini wakiwa na silaha za jadi.

Mashuhuda wa tukio hilo wamesema kuwa kampuni ya ulinzi ya Zenneth Security Services Limited inayolinda mgodi huo ilipata taarifa kuwa kuna wachimbaji haramu maarufu kwa jina la Wabeshi walitaka kuvamia mgodi wakiwa na silaha za jadi ikiwemo mishale, mikuki, virungu, makombeo, mapanga.

na fimbo. Kufuatia hali hiyo askari hao wa Zenneth walifika eneo la tukio kuwadhibiti Wabeshi hao lakini ghafla walianza kushambuliwa kwa silaha za jadi yakiwemo marungu, mishale, mikuki na makombeo. Baada ya kuona wanazidiwa nguvu,askari wa Zenneth walilazimika kuomba msaada wa askari wa kikosi cha kutuliza ghasia (FFU) cha jeshi la polisi mkoa wa Shinyanga.

Baada ya askari wa FFU kufika eneo la tukio nao walianza kushambuliwa na Wabeshi hao ,ndipo PC Idd akapigwa jiwe mdomoni kwa kutumia kombeo na kung'oka meno sita mdomoni na kukimbizwa katika hospitali ya mkoa wa Shinyanga kwa ajili ya matibabu. Mkurugenzi wa kampuni ya ulinzi ya Zenneth Security Services Limited Elisha Ndulu amethibitisha uwepo wa tukio hilo.

Naye mganga mfawidhi wa hospitali ya mkoa wa Shinyanga Dkt Mfaume Salum amesema Pc Idd alipigwa na kitu chenye ubapa mdomoni na kusababisha meno sita kung'oka na anaendelea kupatiwa matibabu,hali yake inaendelea vizuri. Kamanda wa polisi mkoa wa Shinyanga Justus Kamugisha alikiri kutokea kwa tukio hilo na kuongeza kuwa tayari wanawashikilia watu wanne kwa mahojiano zaidi na wanaendelea kufanya uchunguzi.

Wapigwe tu hao Polisi bado kucha sasa wamfuate huko Hospitalini wakamng'oe kucha, mimi nikipata nafasi nitapiga mwizi wangu Chenge au Warema na kung'oa meno pamoja na kucha.

Hao Wabeshi wameshindwa nini kuuchoma huo Mgodi wa mabwana wa mafisadi? Siku nyingine wautie kibiriti huo mgodi
 
Why not Maganga, Ngosha? ... Utumwa wa akili tu ndo unawasumbua MAJIZI ya CCM.... Drilling and Blasting unafanywa na kuratibiwa na Caspin ya Rostam Aziz!!!! Grrrrr
Kumbuka, mgodi unaitwa William Diamond,
Sasa unategemea nini hapo
 
Back
Top Bottom