Polisi akipokea rushwa live

Polisi akipokea rushwa live

jamaa fala kweli, tutaandikiwa 30K mpaka tukome
Hahaha hahaha
Kwani cha ajabu ni nini. Sisi tushazoea kutoa 10 kila siku. Maana hakuna wa kuwakemea. Nani yuko tayari kwenda kuacha gari polisi hadi ukalipe hiyo 30, au kwenda mahakamani kama umekataa kosa? Maana traffic police akishang'amua kua umekiuka sheria ya usalama yeye ndo mwisho. Hakuna haja ya kugombana nao. Msimbazi halali yao.
Bora tusio na magari
 
Dah dogo huyo hata wino wa Pale CCP haujakauka kwenye faili ameshaanza pokea Rushwa!Kweli Rushwa kupambana nayo inahitaji uzalendo!Lakini sishangai Mtoa rushwa kabla hajalalamika Aliona nafuu badala ya kulipa 30,000 akapata na risiti halali ya EFD
 
Inasikitisha sana...

Ila kama huna kosa kwa nini utoe pesa...
Ukiona unatoa pesa basi ujue unamatatizo...



cc: mahondaw
 
hivi hii video ina madhara gani kwa wote wawili..mtoaji na mpokeaji?
 

Katika pita pita nimekutana na hii video ikimuonyesha askari Polisi kijana kabisa akipokea rushwa kutoka kwa dereva wa gari ndogo. Pamoja na hali ilivyosasa lakini mambo bado hayajabadilika. Namshauri Mh. Magu aondoe mifuko kwenye sare zao labda kidogo tutapunguza hili tatizo.

Mbongo kwa ubunifu wa uharibifu kashindikana,watawaelekeza wakaache kwa shoe shine au Wauza magazeti,watu wanaiibia kompyuta sembuse binadamu.
 
Inasikitisha sana...

Ila kama huna kosa kwa nini utoe pesa...
Ukiona unatoa pesa basi ujue unamatatizo...



cc: mahondaw
Hata kama huna kosa wakishang'amua kuwa umekosa, na ameshachukua leseni yako bora mmalizane. Mfano sheria ya zebra crossing, hakuna mahali inasema usimame na kuwasha double hazard hata kama hakuna mtu anayetaka kuvuka. Lakini wamesimamia hapo, na wanakusanya 10k kila siku. So lipi bora? Utoe 30k au 10k ulale mbele 🙂😛😵
 
Anaetoa na anaepokea wote wako na makosa. Yaani mtu anajisifia akitoa rushwa na kujirekodi juu!!!
 
Back
Top Bottom