Watanzania tulio wengi hatulipendi kabisa jeshi la polisi kwa kuwa ni jeshi la wenye pesa,linatumika sana kunyanyasa maskini na kuwalinda matajiri,mtu asiye na hatia anakamatwa na kubambikiwa kesi nzito,na kwa sababu ya umaskini wake anafungwa miaka mingi sana jela,sisi maskini ni wahanga wa jeshi hili,ndo maana hakuna mtu anayeumia roho kusikia polisi kajiua,wanatamani wajiue polisi wote ili watu wapumzike na kadhia ya jeshi hili,sheria ya kijinga na inayotumika na taifa la wajinga eti "uzembe na uzururaji"ndo wanaitumia sana police kunyanyasa maskini,mtu anakudai badala aende mahakamani eti anakushtaki police,kwa kuwa police ndo wavunja sheria wanakuweka ndani bila kukufikisha mahakamani hadi utoe kitu kidogo,na kama huna wanakubambikiza kesi nzito,Tanzania haiwezi kuendelea hadi mwisho wa dunia kama ccm itaendelea kutawala,Biblia inasema HAKI HUINUA TAIFA,je hapa kwetu kuna haki? kuna laana ya dhuluma na uonevu wa hali ya juu,ipo siku MUNGU ATAFUTA MACHOZI YETU.