Ni suala la kushangaza, kama si la kukera, mkuu wa Mkoa wa Dsm, Paul Makonda kushangiliwa na kubebwa juu kwa juu na POLISI!!
ANGEBEBWA NA WANA CCM hilo ni suala lingeeleweka na kuonekana kuwa chama kimeshinda.
Sasa Mtu wa Serikali, Mkuu wa Mkoa, akipongezwa na vyombo vya usalama, kwa ushindi wa CCM!
Nategemea hapa IGP, Kamanda Sirro atawachukulia hatua askari wake kwa kuingilia mambo ya siasa katika nchi ya demokrasia.
MIMI MWANA CCM, na sioni mantiki ya kuipongeza serikali badala ya kuipongeza CCM.
Bashiru Ally, Katibu Mkuu CCM, na hata Polepole, mko wapi kukemea uozo huu.
Waswahili husema ukimwendekeza sana mtoto, atachezea shilingi chooni.
Makonda anachezea Shilingi ya CCM chooni.View attachment 869509
Amani kulindwa...Hivi uchaguzi ungekwenda vizuri Na polisi wakalinda amani ipasavyo,mbunge wa upinzani akaibuka kidedea!!!Je,mkuu wa mkoa angeagiza sherehe ifanyike kushangilia amani kipindi cha uchaguzi?
Kinachosherehekewa ni amani kulindwa au ni ccm kushinda?????
Mkuu umeandikaPolisi tenda wema nenda zako. Hata ccm isipowashukuru Leo mbingu na nchi zinashuhudia kazi nzuri mnazowafanyia. Msivunjike moyo, maana wakati mwingine shukrani ya punda mateke lakini haiwezi kuwa mwisho wa kumtumia punda. Mnafanya kazi nzuri sana kwa kukibeba Chama chetu na Watanzania wanaona na Dunia nzima inaona. Haya maneno mengine ya kupindisha ukweli huku yakionesha dharau dhidi ya kazi yenu nzuri iliyopelekea mkapongezwa na Kada Mkuu wa Chama hicho Mkoa wa Dsm ni ya kupuuza tu. Hata aliyeyaongea anajua alikuwa hasemi ukweli, anajua anatania, lakini hawezi kusema hadharani anatania. Endeleeni kukibeba Chama maana hamna namna nyingine isipokuwa kutekeleza amri toka juu. Polepole si msemaji wa mwisho kwenye chama , wa mwisho yupo na mnamjua, na huyu mliyeaherehekea naye ni mtoto mkubwa wa huyo Bwana Mkubwa. Sasa Polepole ni nani hadi apingane na Prince Paul?