masopakyindi
Platinum Member
- Jul 5, 2011
- 17,882
- 13,172
Kati ya matamko yaliyonikera mimi binafsi, ni lile tamko la Ndg Polepole alipotoka ziarani huko Mbeya.
Vyombo vya habari vilimnukuu akisema viongozi ndani ya mkoa wa Mbeya wana ukabila.
Sijui nini kilimsukuma kusema hivyo maana tuliotoka mkoa huo tupo pamoja katika mambo mengi ya kijamii.
Hata mila na heshima za watu wa mkoa huu zinalingana.
Kitendo cha Prof Mark Mwandosya kumpongeza Mbunge wa Mbeya Mjini Ndg Mbilinyi , ni kitendo ambacho watu wenye mawazo kama ya Humphrey Polepole kitawakanusha na kuwatia soni.
Picha ya Nd Mbilinyi na Prof Mwandosya imeongea mengi.
Wanasaikolojia wameshaanza kuhisi kuwa tamko lile la Polepole ni kutokana na kushindwa katika kile alichokiendea Mbeya.