naomba nisikubaliane na wewe mpendwa,
kama umeishapanda ndege na ikaleta sintofahamu huko juu utakuwa unajua maini ya mwanadamu huwa yanapata hali gani tumboni katika hali hiyo.
naamini kujua sijui nani yuko au kafika marekani sio ishu ya kuandikwa hapa kwa magreat thinkers, kama ingekuwa hivyo, server za JF zingeishajaa siku nyingi kwa mambo kama hayo. by the way, mtu kama miss judith anapoandika hapa unadhani mara zpote yuko dar? hii dunia iko kama kijiji sasa, watu wanaingia na kutoka mara nyingi na hatulazimiki kusema leo tuko nchi gani na lini tumerudi, ila hutokea case nyingine unakuta umeishasema uko wapi au uliondoka/ulirudi lini tz hasa kwenye PM.
tusihusudu sana marekani wapendwa, ni nchi ya kawaida tu na katika baadhi ya maeneo kuna nchi nyingi tu ziko mbele yake. na zehemu nyingine zimetofautiana sana unaweza kudhani umevuka mpaka na kuingia nchi nyingine. tuwe na ubinadamu, msukosuuko wa ndege sio wa kubeza aisee, nimewahi kukiona cha moto lisbon 2008 na sitasahau, kama ni sala tulisali zikaisha
pole eliya, Mungu anakupenda sana
jina lake libarikiwe!