Pole Mtu Mweusi

Idd Ninga

JF-Expert Member
Nov 18, 2012
5,136
4,298
*POLE MTU MWEUSI.*

1) _pole watu weusi,kwa kuzidi kuonewa._
_Poleni watu weusi,kwa kuzidi baguliwa._
_Poleni watu weusi,kwa kuzidi kuuliwa._
*Poleni watu mweusi,ubaguzu wendelea.*

2)wala si bahati mbaya,mambo wanakusudia._
Hata hawaoni haya,hiyo ndo yao tabia.
Wala wihisi vibaya,moyo wanafurahia.
Poleni watu weusi,ubaguzi wendelea.

3) _poleni watu weusi,mwazidi nyanyapaliwa._
_Poleni watu weusi,risasi mwashambuliwa_
_Poleni watu weusi,machungu_ _mnajaziwa._
*Poleni watu weusi,ubaguzi wendelea.*

4)wala hijaanza sasa,ilianzia zamani.
Yote visa na mikasa,kwao inayothamani.
Wote ubaguzi hasa,kwani ni kwao nyumbani.
*Poleni watu weusi,ubaguzi wendelea.*

5) _polenu watu weusi,hayo si mlopangiwa._
_Poleni watu weusi,enyi mmebarikiwa.
Poleni watu weusi_,wao watalaaniwa.
*Polenu watu weusi,ubaguzi wendelea.*
_Shairi_= *POLE MTU MWEUSI.*
_Mtunzi_= *Idd Ninga wa Tengeru Arusha*
*+255624010160*
*iddyallyninga@gmail.com*
_Facebook page_= *Idd ninga na mashairi.*
 
  • Thanks
Reactions: Auz

Similar Discussions

Back
Top Bottom