Je, wajua Sudan Mtu mweusi huitwa 'Mtumwa'?

Analogia Malenga

JF-Expert Member
Feb 24, 2012
5,010
9,875
Japo dunia inapinga ubaguzi wa rangi kwa nguvu zote, Sudan moja kati ya nchi zilizoko Afrika imeonekana kuwa ubaguzi ni kitu cha kawaida.

Nchini humo katika hali ya kuutukuza ubaguzi, mtu mweusi huwa wanamuita mtumwa. Pia nafasi nyingi za kisiasa zinakaliwa na waarabu na wanubi ambao ni weupe huku watu weusi wakifanya kazi za kawaida.

Nchini humo hata ndoa kati ya mtu mweusi na mweupe huonekana kama kitu kibaya kiasi cha mtu kukutana na upinzani mkubwa kutoka kwa jamii.

Ubaguzi wa rangi nchini Sudan umekuwa kama jadi ya taifa hilo tangu walipopata uhuru wao.

=

Maoni kutoka Sudan - ambako watu weusi huitwa watumwa​

27 Julai 2020
Reem Khougli and Issam Abdulraheem

Reem Khougli na Issam Abdulraheem walikabiliwa na matusi kwa kuoana

Katika msururu wa taarifa zetu kutoka kwa waandishi wa habari wa Afrika ,Zeinab Mohammed Salih anaelezea juu ya unyanyasaji wa kutisha wa ubaguzi wa rangi dhidi ya watu weusi nchini Sudan.

Onyo: Taarifa hii ina maneno makali

Maandamano ya kupinga ubaguzi wa rangi yalienea pande zote za dunia kufuatia kifo cha Mmarekani mweusi George Floyd ambaye aliuliwa wakati polisi aliposhindilia goti kwenye shingo lake nchini Marekani, lakini Sudan inaonekana kuwa iko katika dunia tofauti juu ya suala la ubaguzi wa watu weusi.

Kulikua na kampeni kuhusu hashtag #BlackLivesMatter. Badala yake Wasudani wengi wanaotumia mitandao ya kijamii walimshambulia mchezaji soka maarufu mweusi , Issam Abdulraheem, na mwarabu mweupe ambaye ni msanii wa masuala ya vipodozi , Reem Khougli, baada ya kuoana.

"Kusema ukweli we msichana hii ni haramu ... malkia anaolewa na mtumwa ," mwanaume mmoja aliandika kwenye ukurasa wake wa Facebook baada ya kuona picha ya wawili hao.

Facebook mubashara kutoka fungate
Kulikuwa na makumi ya ujumbe- ambao sio wa kushangaza katika nchi ambapo Wasudani wengi ambao hujitazama kama Waarabu, kuliko walivyo Waafrika, mara kwa mara hutumia nene'utumwa'', na maneno mengine yasiyo ya dharau, kuwaelezea watu weusi.

Sudan imekuwa ni nchi inayotawaliwa na watu wenye ngozi nyeupe, wasomi wa kiarabu, ,huku Waafrika weusi wanaoishi katika maeneo ya kusini na magharibi wakiendelea kukabiliwa na ubaguzi na kuachwa nyuma kimaendeleo,

Ni jambo la kawaida kwa magazeti nchini humo kuchapisha maneno ya ubaguzi kuwahusu watu weusi likiwemo neno "mtumwa".

Engraving depicting Abyssinian slaves being taken from the Sudan across the desert to the Red Sea to be taken to Jeddah

Sudan lilikua ni eneo kuu la biashara ya utumwa katika karne ya 19

Wiki chache zilizopita, mwandishi wa taarifa za maoni katika gazeti Al-Intibah linalomuunga amkono rais wa zamani wa Sudan Omar-al-Bashir - ,ambaye hakubaliani na suala la mwanamke kucheza soka, alimuelezea kocha wa kike wa timu ya soka ya Gunners, ambaye anatambulika sana kwa kuifunza timu ya wasichana ya Gunners kama mtumwa.

Na karibu kila chombo cha habari huwaelezea wahalifu wadogo wadogo katika mji mkuu , Khartoum, kama "negros" kwasababu wanawaona kama ni watu maskini na wala si watu wa jamii ya Waarabu.

Wakati nilipomuuliza Abdulraheem kuhusu kile anachoweza kusema juu ya unyanyasaji na ubaguzi aliofanyiwa yeye na mke wake, alisema : Sikuweza kutuma picha zaidi kwenye kurasa za mitandao yangu ya kijamii kwa kuogopa kupokea matusi zaidi."

Badala yake Abdulraheem mwenye umri wa miaka 29- na mke wake mwenye umri wa miaka 24 walifanya Facebook mubashara wakati wa fungate yao, wakisema kuwa wanapendana na ubaguzi hauna maana kwao.

Sura chache za watu weusi​

Katika tukio la hivi karibuni, mkuu wa kikundi cha haki za wanawake kinachoitwa , No To Women Oppression, alitoa maoni yake kwenye picha inayoonesha kijana mmoja mweusi akiwa na mke wake mzungu kutoka Ulaya kwa kusema kuwa mwanamke yule, katika kumchagua mume wake, huenda alikua anaangalia kiumbe ambacho kinakosekana katika mabadiliko kati ya binadamu na nyani.

Kufuatia malalamiko ya watu juu ya ujumbe huo, Ihsan Fagiri alitangaza kujiuzulu, lakini No To Women Oppression kikakataa kukubali kujiuzulu kwake, likisema kuwa hakua na maana hiyo aliyoiandika.

A Sudanese protester holds up a sign reading in Arabic our martyrs are not dead, they are alive with the revolutionaries along with the English slogans #BLUEforSUDAN and #BLACKLIVESMATTER, as demonstrators mark the first anniversary of a raid on an anti-government sit-in and some demonstrate in support of US protesters over the death of George Floyd, in the Riyadh district in the east of the capital Khartoum on June 3, 2020

Kumekuwa na maandamano madogo ya kupinga ubaguzi wa rangi nchini Sudan
Ubaguzi wa rangi ni kitu cha jadi nchini Sudan, kihistoria na tangu uhuru wa taifa hilo , ambapo vyeo vya juu zaidi vya kazi vimekua vikijazwa na watu kutoka kaskazini - ambao ni wa jamii za Waarabu na Wanubi.

Takriban maafisa wote wa ngazi ya juu katika jeshi wanatoka katika jamii hizi, jambo linalowaruhusu kutumia ushawishi wao kumiliki sekta ya biashara.

Leo kama ikiingia katika idara yoyote ya serikali au benki mjini Khartoum , ni nadra kumuona mtu mweusi akifanya kazi muhimu.
Hakuna takwimu za kuaminika juu ya idadi ya watu kulingana na jamii zao, ukiachana na utajiri wao, lakini kikundi cha waasi wanaopigania haki za watu weusi cha Darfur kinakadiria kuwa 60% ya wakazi wa Khartoum ni weusi.

Wafanyabiashara wa utumwa 'walitukuzwa'
Ubaguzi wa rangi una mizizi yake tangu kuasisiwa kwa mji wa Khartoum mwaka 1821 kama soko la watumwa.
Kufikia nusu karne, karibu theluthi mbili ya watu waliokuwa katika mji huo walikua watumwa.

Sudan ilikuwa ni mojawapo ya maeneo ya Afrika ya kupata watumwa, huku watumwa waliosafirishwa kutoka kusini hadi kaskazini, na Misri , Mashariki ya kati na maeneo ya Mediterranean wakichukuliwa kutoka Sudan.

Al-Zubair Pasha Rahma alikua mfanyabiashara maarufu wa watumwa


Bado wafanyabiashara ya utumwa wanatukuzwa-mtaa katikati mwa mji mkuu umepewa jina la al-Zubair Pasha Rahma, ambaye jhimaya yake ya biashara ilipanuka hadi katika maeneo ya ile inayoitwa Jamuhuri ya Afrika ya katikwa sasa na Chad.

Wanahistoria wanasema aliwakamata zaidi watumwa wanawake kutoka maeneo ya Sudan ambayo kwa sasa yanafahamaika kama Blue Nile na milima ya Nuba Mountains, pamoja na Sudan Kusini na kutoka katika jimbo la Oromia nchini Ethiopia. Alikua anafahamaika kwa jeshi lake la watumwa, ambalo liliwajumuisha watumwa waliotekwa kutoka Sudan Kusini.

Mtaa mwingine umepewa jina la Osman Digna - mfanyabiashara wa watumwa na kamanda wa kijeshi, ambaye biashara yake wakati huo iliyonoga wakati huo ilivunjwa na kisheria utumwa.

Biashara hiyo ilizuiwa rasmi mnamo mwaka 1924, lakini uamuzi wa kuizuwia ulikabiliwa na upinzani mkali kutoka zaidi kwa Waarabu na viongozi wa Kiislamu, miongoni mwao wakiwa ni Abdelrahman al-Mahdi na Ali al-Mirghani, ambao wengi wanamini walikua na watumwa wanawafanyia kazi katika ardhi yao iliyokuwa kando ya mto Nile.

Waliuandikia utawala wa kikoloni wakiutaka wasizuwie utumwa, lakini ombi lao lilipuuzwa.

Wanaume hao wawili, pamoja na vyama vyao vya kisiasa - Unionist na Umma - waliendelea kuwa na ushawishi mkubwa baada ya uhuru wakiingiza fikra za ubora wa Waarabu katika taifa jipya kwa kutoa karibu ajira zote kwa Waarabu na kushindwa kuendeleza maeneo yanayokaliwa na watu weusi.

Mjukuu wa Mahdi, Sadiq al-Mahdi,alihudumu kama waziri mkuu kuanzia mwaka 1966 hadi 1967 na tena kuanzia mwaka 1986 hadi 1989, wakati mtoto wake Mirghani, Ahmed, alipokua rais katika serikali ya Muungano iliyoundwa na wanaume hao wawili.

Wasomi wawili wa Sudan, Sulimen Baldona Ushari Mahoumwalidai wazi kwamba waligundua ushahidi wa Waarabu wa makundi yaliyoko wanaowatumikisha watu weusi kutoka kusini kama watumwa. Walisema makundi haya yalipewa silaha na jeshi la Sadiq al-Mahdi - na walikua ndio mwanzo wa wanamgambo wa Janjaweed, ambao baadae walishutumiwa kwa kwa mauaji ya kimbari ya Darfur.

Sadiq al-Mahdi amekuwa kwenye siasa kwa zaidi ya miaka 50


Madai ya uvamizi wa watumwa yalikanushwa na serikali ya Ahmed Mirghani na Sadiq Mahdi, ambao waliendelea kuwa na ushawishi katika siasa za Sudan na wako karibu na serikali ya sasa, ambayo ilichukua mamlaka baada ya kumpindua madarakani Bwana Bashir mwaka 2019.

Uvamizi wa biashara ya karne ya 21​

Kujiona wao ndio wa maana zaidi kwa wengi miongoni mwa wasomi Waarabu, ndio sababu kuu ya baadhi ya mizozo mibaya zaidi iliyoikumba Sudan tangu ilipopata uhuru, huku watu weusi ama wanadai usawa au ardhi yao wenyewe.

Uvamizi wa watumwa kusini mwa nchi uliripotiwa sana kuwa uliendelea hadi mwishoni mwa vita vya wenyewe kwa wenyewe mwaka 2005, jambo lililosababisha watu weushi hasa Waafrika wa Sudan Kusini kujitenga na Sudan miaka mitano baadae.

Wanawake na watoto waliotekwa na makundi ya Waarabu kufanya kazi kwa ajili ya "bwana" bila malipo mara nyingi hawakuziona familia zao tena, ingawa mara kadhaa uhuru wao waliupata kupitia makundi ya msaada kama Christian Solidarity International.

Na tangu mzoizo wa Darfur ulipoanza mwanzoni mwa miaka ya 2000s, kundi la wanamgambo Waarabu wanaounga mkono serikali la Janjaweed limekua likiripotiwa mara kwa mara kwa kuvamia vijiji vya watu weusi, kuwauwa wanaume na kuwabaka wanawake.

Ni mchache yaliyobadilika huko mwaka jana, huku ripoti za ubakaji na uchomaji wa vijiji zikiendelea licha ya mazungumzo ya amani yaliyoandaliwa na serikali ya muungano, ambayo inaongoza kipindi cha mpito cha miaka mitatu.
Maasi mengi yamekuwa yakifanyika katika Darfur


Serikali ya mpito iliundwa na jeshi na makundi ya kiraia yaliyoongoza mapinduzi mwaka 2019, lakini haijawa wazi ikiwa kweli imejitolewa kushughulikia suala la mfumo wa ubaguzi wa rangi ndani ya taifa la Wasudan.

Chama cha Congress (SCP), ambacho ni mjumbe muhimu wa raia katika serikali, kinasema kwamba sheria zimekwisha pendekezwa za kutambua kauli za chuki kama uhalifu. Chini ya pendekezo la sheria hiyo, adhabu ya kutumia maneno ya ubaguzi wa rangi itakua ni kifungo cha gerezani cha miaka mitano, aliniambia msemaji wa chama cha SCP Mohamed Hassan Arabi.

Lakini weusi wengi hawafurahii nafasi ya jeshi katika serikali, ikizingatiwa kuwa lilikuwa ni sehemu ya utawala wa Bwana Bashir.

Mmoja wa mawaziri wachache weusi, Steven Amin Arno, alijiuzuru katika kipindi cha miezi miwili baada ya kuchukua mamlaka, akisema katika barua yake ya kujiuzulu ambayo ilionekana kwenye mitandao ya kijamii kwamba hakuna mtu aliyekua ana msikiliza.

Serikali haikutoa kauli yoyote kuhusu kujiuzulu kwake, jambo linalomaanisha kuwa alichokisema kilikua kweli.

"Kilichotokea kwangu kinaonesha kutengwa na taasisi ya ubaguzi wa rangi nchini ," aliniambia.
 
Hivi vi arabu vina husda sana. Hapa namkumbuka trump pamoja na matatizo yake ila ana vision ya kuona mbali sana

Na ndio maana trump alikua akianza kubagua alikua haachi kitu, haangalii huyu muarabu sijui ni mweupe hivyo asibaguliwe...no hilo hakujali

Halafu wao ndio wako kipaumbele sana kulialia pale wanapofanyiwa roho mbaya na wazungu
 
Nilikaa Sudan siku 8 tu.Sikuona haya mambo labda kwa kuwa nilikaa muda mfupi wa wiki moja tu. Kama ni kweli ni mbaya sana
Mkuu inategemea ulikuwa Sudan pande gani. Mpaka hili jambo limeripotiwa hi I na ushahidi wakumwaga jua hii hali imetawala huko.
 
Na wale tunaowaita mabeberu ni kina nani?

Kuitana majina, kupuuza imani na tamaduni za wengine, kujiona bora kuliko jamii zingine n.k hilo lipo ktk D.N.A ya jamii zote .

Hivyo Waafrika wamatumbi tuache "kulilia" tupendwe, tutukuzwe au imani na tamaduni zetu zikubalike na wengine.

Tunachopaswa kufanya ni kuienzi jamii yetu pamoja na hadithi zake zinazotuasa kuwachukulia kwa tahadhari wale wote wasio kama sisi "waswahili " wanaokuja kwa njia ya majahazi kwetu na kushuka pwani au wanaokuja huku wakiendesha farasi toka nchi za ughaibuni na kuvamia ardhi zetu na kututaka tuabudu Miungu yao, Mitume yao na Tamaduni zao badala ya Mizuka yetu ya Milima ya Kolelo ya Uluguru, tambiko zetu na miti yetu mikubwa tunapo weka tambiko zetu kuwasiliana na wahenga wetu tulioowazika ktk ardhi yetu.

Mfano M- Turuki huwa siku zote kwa watoto na wajukuu zake anamsimulia vibaya Mwarabu na mwarabu vivyo hivyo kwa wanae na wajukuu wana hadithi za kutisha za kuogofya juu ya M-Turuki The Long Struggle for Supremacy in the Muslim World

B3-CE294_SaudEr_JV_20181025184422.jpg

EDEL RODRIGUEZ

Kubwa sisi wamatumbi/waafrika/waTanzania tusilazimishe "kupendwa" bali tujipende wenyewe. Na walimwengu waarabu, M-Turuki, wazungu , waChina, waJapani n.k wataona jinsi tunavyojinasibisha kwa mapenzi makubwa na Mahoka Zolele wetu mizuka ya mababu zetu wa karne na Karne ya Matombo Morogoro au Vibwengo wa Handeni n.k hivyo wakuja hao wageni kutuacha kutushawishi kwa hadaa kubwa kuwa sisi ni 'washenzi ' 'wasiostaarabika' kwa vile tumekataa kukumbatia Miungu yao ya Kigeni isiyotaka kumiminiwa pombe adhimu ya Rubisi, Kimpumu au Kayoga ya Kasulu Kigoma na kuchezewa ngoma zetu za Sangura toka Mahenge Kilombero n.k

Waafrika wote tutembee vifua mbele na kujivunia vya kwetu na kupuuza yale yote mageni ya kuja kwa majahazi, farasi na sasa ndege aeroplane. Tukifanya hivyo tutajitambua na kujiona tu bora kuliko jamii zingine maana jamii zingine pia hujiona bora kuliko wengine na hapo ndipo heshima itarudi.
 
Afrika kila nchi kuna ubaguzi wake wengine wanabaguana kwa ukabila wengine kidini mfano mzuri Bongo wakristo wakizidi kwenye vyeo huko serikalini inakuwa poa kama ilivyo sasa lakini ikitokea waislamu wakawakaribia tu hata kama wasiwazidi wakristo basi inakuwa Nongwa,hapo utaona hata upinzani wa ccm na chadema unawekwa pembeni wakristo wa pande zote mbili wanaungana kuwasakama waislamu.
1000% correct,
Na lengo la uzi huu ni kuusema huohuo uislamu hawana lolote kutaja waarabu ndio kutaja waislam ila wanavyobaguluwa na wazungu wenzao kimya kabisa
"hawatawadhuru ila maudhi tu"
 
Msuguano baina ya jamii ki-Imani, Kitamaduni na hata level ya mapambano kujikomboa kifikra, kitamaduni, kiimani na kuondokana na utumwa na Ukoloni mambo leo

Are Conflicts In The Middle East And Afghanistan The Result Of A “Clash Of Civilizations?”​

March 18, 2017 in Asia / Canada / Iran / Iraq / Middle East / North America / United States by Lina Na Gyoung Lee (updated on March 19, 2017)

The intensifying military confrontation between the West and the Arab world has spread instability and fear throughout the international community. There has been a controversial debate on whether the conflicts in the Middle East and Afghanistan are the result of a natural collision between cultures and values or the consequences of Western imperialist interference in the region. This essay sits on the latter end of the spectrum and argues that the ‘clash of civilization’ dispute is an attempt to justify Western dominance in the Middle East, which serves as a self-affirming prophecy that manifests further turbulence in the area.

The essay will scrutinize the above argument in three stages. Firstly, understand Huntington’s hypothesis and identify aspects of Israel-Palestine conflict and war in Afghanistan that resemble features of ‘clash of civilizations.’ Secondly, illustrate how the conflicts have been falsely depicted as the result of nonalignment between Western and Middle Eastern values, which rationalizes Western dominance as a natural confrontation of the two worlds. Thirdly, explain why this misrepresentation of clashing civilizations is a powerful political apparatus used by the West and a dangerous self-fulfilling prediction that may have real consequences that change the trajectory of contemporary politics.

Turmoil and bloodshed has engulfed the Arab world. A noticeable trend was emerged across the series of cross-continent conflicts. States rallied support from other states within close proximity. These states stimulated public support by appealing to common culture and identity. As a result, fundamentalism developed in the region. These features resemble Samuel P. Huntington’s “clash of civilization” hypothesis. Huntington explains that conflicts are inevitable in a world with two civilizations of similar economic and military strength. The predominate civilization will be pressured to maintain its power and protect its values and interests that are irredeemably different.

However, what appears to be pure rivalry between the West and the Middle East based on differences in values is instead deeply embedded in the historical account of Western intervention in the Middle Eastern region. For instance, the purported religious war between Israel and Palestine was triggered by Britain committing to three promises regarding the division of Ottoman Palestine after WWII. The British issued the 1917 Balfour Declaration to the Zionists, the 1916 Sykes-Picot agreement and the League mandates to the French and also to the ruler of Mecca, Sharif Hussein. Thus, the conflict that claims to be a clash of civilizations is in fact a battle over territory that was sparked by the “imaginative geographies” of the British imperialists.

Similarly, the American invasion of Afghanistan was justified in the name of a ‘war on terror.’ This is an extension of the ‘clash of civilizations’ argument. On the surface, the conflict resembles aspects of Huntington’s prediction as both actors mobilize alliance from states that share ‘similar’ political attitudes. Saddam Hussein invoked Islamic appeal, Ayatollah Ali Khamenei and King Hussein of Jordan called for unification of the Arab world to fight a holy war against the West. The U.S. pleaded “every nation in every region” to decide if they were on their side, or with the terrorists. The U.S. also claimed that the ‘war on terror’ was triggered because their enemies do not value freedom. This presents America as the defender of freedom and liberty and the Middle East as the patron of violence and terrorism. As a result, the U.S. is given global legitimacy to carry out its main goals in the Middle Eastern region.

Since obtaining access to oil and promoting pro-Western states in the Arab world are much more achievable with the support of local autocrats, the U.S. has supported authoritarian regimes with the expansion of the ‘war on terror.’ The U.S. was able to fight the threats imposed on autocrats in the Middle Eastern region in the name of its anti-terrorism campaign, which disguised interventions as humanitarian rescues.

In essence, the clash of civilization argument is a self-affirming prophecy that serves as a powerful political apparatus. It justifies Western imperialism in the Arab world. Huntington’s belief that people of different ethnicity and religion will eventually collide violently due to irredeemable difference has been made into a reality by policy makers for their own interests. Thus, the clash of civilizations argument serves not only as a manipulation tool of the West, but also as a self-fulfilling prophecy that fuels the vicious cycle of misrepresentation and resentment.

Huntington’s hypothesis underestimated the presence of Western dominance that exists throughout contemporary politics. It simultaneously underestimated the difficulty in enabling non-Western societies to move and shape history alongside powerful actors of the West. Conflicts in the Middle East and Afghanistan may reflect certain images of Huntington’s hypothesis, but these conflicts are actually more complex. This shows the importance of legitimizing the historical narratives of these countries.
Source : Are Conflicts In The Middle East And Afghanistan The Result Of A “Clash Of Civilizations?”
 
Wimbo huu maarufu wa kizalendo ktk video wa enzi za wazazi wangu kuhusu kujitambua wewe ni nani. Kongole na Hongera kwa vijana wa Bagamoyo kuuimba tena ili kukomboa bongo na fikra zetu.

Na bila aibu lazima sisi kizazi kipya tuwe tunaurithisha kwa vizazi vyetu . Ama sivyo tutabaki tegemezi na kulalama kwa vile fikra zetu zimeshindwa kumuelewa au tunaona haya kusema bila kupepesa macho aliyeleta ukoloni, utumwa , ubaguzi wa rangi na ubeberu ni nani na tunalilia "watupende" miaka hii ya Twenty Twenty !

Wimbo wa Kizalendo toka kwa Kwaya ya Bagamoyo juu ya Bara la Afrika:



Bara la Afrika, Lahitaji Ukombozi,

Ukoloni Mbaya na Ubaguzi Wa Rangi,

Mataifa Haya Ya Ulaya ndiyo, Afrika kuivamia,

Wahenga Wetu Zamani Walikataa,


Ubeberu, Ukoloni, Utumwa , Walikataa

Wazungu waliwatesa,Waarabu waliwatesa,

Ni Vigumu sana kusahau Kweli walivyowatendeea

Ni Vigumu Sana Kusahau Kweli walivyowatendea

Wahenga Wetu Zamani Walikataa

Bara La Afrika Lalilia Ukombozi

Umoja wa Afrika Unatutia Moyo,

Kufagia huo Ukoloni wote na Ubeberu Wote

Wahenga Wetu Zamani Walikataa

Ubeberu walikataa, Ukoloni walikataa Utumwa Walikataa

Waafrika Tujipange Kupambana, Tuungane Na Kuacha Kulalala

Wahenga walipambana Kwanini Sisi Tushindwe

Ni wajibu wetu kukumbuka Ubeberu upo hai....

Source : D'jarell Messa
24 Apr 2011
People singing a african choral in Bagamoyo, Tanzania
 
Kwanini usiitwe mtumwa wakati dini zao na zenu mnaita uchawi,tamaduni mnaiga zao m, zenu ushamba,uvaaji mnaiga wao,elimu yao zenu mnaita ushamba usio na manufaa,.

Sasa km kila kitu mnaiga chao,kipi chenu walichoiga?kipi chenu wawaige?waafrica mna kipi ambacho mnajivunia???

Mnadhani neno utumwa lina maana moja????You have nothing to offer sasa you are useless igaiga,wa kujidharau wa ku copy na kupaste.

Mnadhani wao ni wajinga kulinda utamaduni wao na kukuaminisha wako mbaya..we call it mental slavery...kichwani kwanza.
 
Back
Top Bottom