Plot inauzwa fasta kwa Million4.1 tu!!!!!

Plot inauzwa fasta kwa Million4.1 tu!!!!!

Nimeku PM mvaa tai! Naomba unijibu tafadhali.
Asante.

Sent from my BlackBerry 9900 using JamiiForums
 
Wadau mwenzenu nina shida ya fedha ya haraka nimepungukiwa kama Million nne, nipo Dar nimeamua kuuza Plot yangu fasta, Ipo Dodoma ni kiwanja cha mradi kilitolewa na CDA katika mradi wa April 2006, nilinunua kwa mtu Mwaka 2008 na kupata hati miliki kwa jina langu March 2009. Ni eneo lililokwisha endelea kwani Tayari kuna mitaa ya watu wanaishi, nimekilipia kodi ya ardhi mpaka mwaka wa fedha 2013/14.
Ukubwa wa kiwanja ni Sq Metre 631. Kipo Chidachi West, block 'F' ni walkable distance kutoka St John University, Bei ni
Tshs Million 4.1 Hatimiliki ninayo hapa Dar sitaki dalali, kwa mnunuzi wa kweli ani-PM ili utaratibu wa kukiona ufanyike akiridhika tufanye biashara, kwa aliye Dodoma nitamuelekeza akakione mwenyewe kwani ni rahisi kufika nikimpa namba ya Kiwanja, akiridhika anistue.

Mvaa Tai, sasa tukikutana na kunionyesha hati si utakuwa verified user, huogopi?
 
Mvaa Tai, mkuu umeuza au bado?

Sijauza bado watu kama watatu wamekuja ofisini kwangu wameona hatimiliki na site map wamekubali ila mchakato wa kwenda kukiona unaendelea wote wamesema wanaenda Dodoma Wikiendi hii kwa maana kuanzia kesho, kwasababu mimi nipo tight hapa ofisini (Dar) nimetoa time kila mtu afanye awezavyo akakione kwa mda wake pale Dom ikiwezekana akawaone na watu wa Ardhi au CD.

Atakayeridhishwa tumalize biashara. Tumia PMs kwa mawasiliano ambayo ni personal kama namba za simu na kadhalika kwasababu sipo mda wote JF, Wakati wa wikiendi nashinda vilabu vifuatavyo, Kibo Complex, Isaje na Fairway. Mmoja nimeshindwana naye anataka kukilipia bila kukiona ila ana ma-complication mengi sana ya kisheria mimi niliyakubali ila kwa ghalama zake, akagoma anataka ghalama za wanasheria ziwe zangu, nimecheka sana ki-deal cha M4 nilipie na mighalama ya Wanasheria walio aghali.

Ila ikifika Ijumaa ya tarehe 26/07/2013 nafunga biashara bila kujali kimelipiwa au bado maana lengo langu ni ku-trade off na deal moja ina-expire ijumaa.
 
Mvaa Tai, sasa tukikutana na kunionyesha hati si utakuwa verified user, huogopi?

Mimi siogopi kila ninacho kipost JF naweza kukitetea mahakamani, alafu usije ukamkosea mtu kisheria humu JF ukidhania huwezi kupatikana kwasababu unatumia Anonymous name, mbona nimeonana na akina Zagazaga TEMPOLALE na hata Mfichua siri Japo limfichua siri limekaa kama jitu la Usalama wa Taifa.....lol
 
Nimeku PM mvaa tai! Naomba unijibu tafadhali.
Asante.

Sent from my BlackBerry 9900 using JamiiForums

Nimeiona PM yako lakini nilikujibu kwa wakati ila nilikushauri um-PM Chelsea maana yeye ndo anamiliki cha Nkuhungu
 
Asante mvaa tai, nilipata PM yako. Chelsea hajanijibu. Siku njema ndugu.

Sent from my BlackBerry 9900 using JamiiForums
 
Nakitamani sana, ikiwa ridhiki yangu nitakutafuta mkuu
 
Mimi siogopi kila ninacho kipost JF naweza kukitetea mahakamani, alafu usije ukamkosea mtu kisheria humu JF ukidhania huwezi kupatikana kwasababu unatumia Anonymous name, mbona nimeonana na akina Zagazaga TEMPOLALE na hata Mfichua siri Japo limfichua siri limekaa kama jitu la Usalama wa Taifa.....lol

Ha ha haaa hili liMfichua siri ndio anataka kuharibu picha yote
 
Back
Top Bottom