Pitia hapa kupata ujumbe wa Jumapili ya leo

Pitia hapa kupata ujumbe wa Jumapili ya leo

Chrismoris

JF-Expert Member
Joined
Oct 27, 2017
Posts
14,234
Reaction score
17,828
Habari ya jumapili mabibi na mabwana. Leo ni siku nyingine ya kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kutujalia uzima.

Napenda kuchukua wasaa huu kuwashirikisha ujumbe wa leo kutoka katika maandiko matakatifu.

Katika masomo ya leo tunakumbushwa kuhusu kuishi maisha yenye uwiano. Uwiano huu tunauzungumzia katika suala zima la kuhakikisha matendo yetu yaendane na maneno tunayoyaongea.

Katika Injili tumepewa mfano wa makuhani ambao walikuwa wanawabebesha waamini wao mizigo mizito ambayo wao wenyewe hawawezi kuibeba. Hivyo basi Bwana Yesu anatuambia tujiepushe na maisha yaliyojaa unafki, tuache tabia ya kuwahubiria wenzetu mambo ambayo sisi wenyewe hatuwezi kuyatenda.

Tunapofanya jambo lolote tuhakikishe dhamira zetu ni safi na zinasadifu yale tunayoyaongea.

Kwa leo ni hayo, aksanteni sana.

Muwe na jumapili njema.
 
Yesu aliwaambia makutano na wanafunzi
wake, akasema, Waandishi na
Mafarisayo wameketi katika kiti cha
Musa; basi, yoyote watakayowaambia,
myashike, na kuyatenda; lakini kwa
mfano wa matendo yao, msitende;
maana wao hunena lakini hawatendi.
Wao hufunga mizigo mizito na
kuwatwika watu mabegani mwao;
wasitake wenyewe kuigusa kwa kidole
chao. Tena matendo yao yote huyatenda
ili kutazamwa na watu; kwa kuwa
hupaua hirizi zao, huongeza matamvua
yao; hupenda viti vya mbele katika
karamu, na kuketi mbele katika
masinagogi, na kusalimiwa masokoni, na
kuitwa na watu, Rabi. Bali ninyi msiitwe
Rabi, maana mwalimu wenu ni mmoja,
nanyi nyote ni ndugu. Wala msimwite
mtu baba duniani; maana Baba yenu ni
mmoja, aliye mbinguni. Wala msiitwe
viongozi; maana kiongozi wenu ni
mmoja, naye ndiye Kristo. Naye aliye
mkubwa wenu atakuwa mtumishi wenu.
Na yeyote atakayejikweza, atadhiliwa; na
yeyote atakayejidhili, atakwezwa.
 
CCM hawamaanishi wanachokinena;
 
Habari ya jumapili mabibi na mabwana. Leo ni siku nyingine ya kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kutujalia uzima.

Napenda kuchukua wasaa huu kuwashirikisha ujumbe wa leo kutoka katika maandiko matakatifu.

Katika masomo ya leo tunakumbushwa kuhusu kuishi maisha yenye uwiano. Uwiano huu tunauzungumzia katika suala zima la kuhakikisha matendo yetu yaendane na maneno tunayoyaongea.

Katika Injili tumepewa mfano wa makuhani ambao walikuwa wanawabebesha waamini wao mizigo mizito ambayo wao wenyewe hawawezi kuibeba. Hivyo basi Bwana Yesu anatuambia tujiepushe na maisha yaliyojaa unafki, tuache tabia ya kuwahubiria wenzetu mambo ambayo sisi wenyewe hatuwezi kuyatenda.

Tunapofanya jambo lolote tuhakikishe dhamira zetu ni safi na zinasadifu yale tunayoyaongea.

Kwa leo ni hayo, aksanteni sana.

Muwe na jumapili njema.
Asante. Nashukuru hujataja neno kubatizwa.
 
Habari ya jumapili mabibi na mabwana. Leo ni siku nyingine ya kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kutujalia uzima.

Napenda kuchukua wasaa huu kuwashirikisha ujumbe wa leo kutoka katika maandiko matakatifu.

Katika masomo ya leo tunakumbushwa kuhusu kuishi maisha yenye uwiano. Uwiano huu tunauzungumzia katika suala zima la kuhakikisha matendo yetu yaendane na maneno tunayoyaongea.

Katika Injili tumepewa mfano wa makuhani ambao walikuwa wanawabebesha waamini wao mizigo mizito ambayo wao wenyewe hawawezi kuibeba. Hivyo basi Bwana Yesu anatuambia tujiepushe na maisha yaliyojaa unafki, tuache tabia ya kuwahubiria wenzetu mambo ambayo sisi wenyewe hatuwezi kuyatenda.

Tunapofanya jambo lolote tuhakikishe dhamira zetu ni safi na zinasadifu yale tunayoyaongea.

Kwa leo ni hayo, aksanteni sana.

Muwe na jumapili njema.
Asante mkuu
 
Back
Top Bottom