PISHI: Wali mixer by tambi

PISHI: Wali mixer by tambi

Mwachiluwi

JF-Expert Member
Joined
Mar 10, 2022
Posts
33,467
Reaction score
65,786
Hellow mchana mwema

Leo tupike hiki chakula asili yake Madam B atasema

Kwanza chukua tambi zako ulizo kataka ndogo ndogo kisha weka kwenye sufuria ya mafuta yalio chemka kisha anza kuzikaanga mpaka zibadirike rangi na kuwa kahawia zisiungue
1743328829929.jpeg

Baada ya hapo chukua mchele wako ulio uosha kisha tia kwenye sufuria anza kuukaanga na tambi
1743329028599.jpeg

Baada ya hapo weka maji yako kama una tui la nazi tumia mimi nazi nakuja kuweka baadae baada ya maji kupungua kidogo
1743329103434.jpeg
Kisha funika na upunguze moto moto weka mdogo kabisa na ukaee kwa muda mrefu
Baada ya hapo mm nikaweka nazi kisha nikageuza nikaacha nikaanza kupika mboga
1743329192358.jpeg

Mboga kwa mimi natumia kuku rosti na wewe unaweza tumia samaki au nyama mboga yoyote ulio nayo
Nilianza kukaanga kuku kwanza
1743329291035.jpeg

Kisha nikaweka vitunguu pamoja na hoho na karoti
1743329349582.jpeg

Kisha nikaweka nyanya nilio saga
1743329397452.jpeg

Baada ya nyanya kuiva nikaweka nazi
1743329538885.jpeg

Baada ya hapo nipo nakula karibuni sana wote
1743329734699.jpeg

Nipo tayari kwa kusimangwa 😂
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom