PINDA - Nitatoa Maamuzi yote Jumatatu

PINDA - Nitatoa Maamuzi yote Jumatatu

Our prime minister can never make any strong decision. So he needs to resign and his all cabinents members.
 
Hahaaaa, mbona Mbowe alimaliza hiyo juzi...kama bunge litakuwa legelege basi wataenda kwa wananchi kuwaeleza ili waiadabishe serikali...chaguo ni lao! Wajiuzuru au bunge liwafukuze au wasubiri kiama toka kwa wananchi!
 
wakati wa jairo mambo yalikuwa hivihivi. Huyu pinda hapati somo kabisa. Si ajictwalie tu madaraka tumuone kidume? Kazi kulia tu. :A S-cry:
 
Zitto alisema neno nzuri sana na la maana "ACCOUNTABILITY"

Serikali ya Kikwete ina miss accontability

Let them go to hell this way, M4C inachanja mbuga kama haina breki

usibague. Sema serikali chini ya ccm inakosa uwajibikaji
 
Hata yeye anachezea shilingi chooni vile vile. Kwa taarifa yenu hakuna mtu mwoga kama huyu mkw*re. Tukimchachamalia wiki moja tu haki ya nani ana toroka nchi! Nakwambieni mimi! Ooho, haya!

Kwa mwendo huu 2015 ni mbali sana kwa JK na CCM. Nahisi tutatakiwa kufanya uchaguzi mkuu kabla ya 2015. Mtaniambia.
Mnafikiri kitatokea nini kwa Mkw-ere? Mimi naona kama yupo safe sana. Maana hakuna kura ya kutokuwa na imani na Rais. Kama katiba ingeruhusu kupiga kura ya aina hiyo, kwa hakika Kikwete asingekuwa salama. Lakini kutokana na katiba yetu ilivyo, sidhani kama anaweza kuguswa na lolote, na ukizingatia uoga wa watanzania.
 
Pinda akijadiliana na wabunge wa upinzani wanaotaka kumwondoa madarakani Dodoma leo.

IMG_9138.JPG

siasa kitu cha ajabu sana. Mnachekeana na adui hivihivi!
 
Lowasa, Pinda, nanihi, nionavyo tunatibu kidonda cha kansa badala ya kukata mguu mzma, kansa ya tz ni JK.
 
Sijawahi kuona Waziri Mkuu bogus kama Pinda katika historia ya nchi hii

jamani siasa isitufikishe huko huyu mh pinda ni kama baba yako mzazi je waweza kumtusi baba yako kama ulivyofanya kwa PM kiukweli si busara ata kdg si vizuri ata kdg kuna namna ya kusema jambo kwa hisia na watu wakakuelewa lakini si lazima mpaka umtusi mtu huyu ni kama mzazi wako sasa sidhani kama waweza mtusi baba yako ata kama amekukosea!
 
jamani siasa isitufikishe huko huyu mh pinda ni kama baba yako mzazi je waweza kumtusi baba yako kama ulivyofanya kwa PM kiukweli si busara ata kdg si vizuri ata kdg kuna namna ya kusema jambo kwa hisia na watu wakakuelewa lakini si lazima mpaka umtusi mtu huyu ni kama mzazi wako sasa sidhani kama waweza mtusi baba yako ata kama amekukosea!

Panadol, nakuomba kwanza uelewe kuwa tupo wengi tu humu jamvini JF ambao Pinda ni kama mdogo wetu! Watanzania mnaniacha hoi, yaani Pinda kuwa kama baba kunampa kinga kwa mapungufu na udhaifu wake uliomganda kama kupe! Pinda ni Waziri Mkuu wa kwanza duniani kukiri mbele ya wananchi kuwa serikali inawaogopa wezi kwa sababu wana nguvu ya kuweza kuiyumbisha nchi! Pamoja na kukiri hivyo, ni ajabu ilioje kuwa Pinda bado ni Waziri Mkuu ikiwa na maana kwamba, sisi Watanzania, sote ni mateka wa mafisadi na ndio sababu wanalitafuna taifa wapendavyo na bila huruma. Waziri Mkuu Pinda, kama alivyosema mchangiaji Saas, ni bogus na mimi naongezea Pinda ni zaidi ya bogus, ni mpuuzi, asiyejua hata asilimia moja ya wajibu wake kama Waziri Mkuu.
 
[video]http://m.youtube.com/index?desktop_uri=%2F&gl=US#/channel/UC4KSfbi1Z9NNrh7Ea13Wk4w[/video]
 
muda mfupi uliopita waziri mkuu mheshimiwa mizengo pinda kamaliza mazungumzo na waandihi wa habari wa vyombo mbalimbali na kusisitiza kuwa taarifa kamili kuhusu mawaziri wanaodaiwa kujiuzuru atazitoa rasmi jumatatu atakapokuwa akiahirisha kikao cha bunge.

Maswali ni mengi kwa kila nayeisikia kauli hii:

  1. nini kimejitokeza hapa
  2. kuna aliyezuia maamuzi haya yasipate baraka?
  3. pm kashikwa na kigugumizi gani?
  4. mbona kila jambo katika kiako cha jana yalishafahamika mpaka maazimio?
  5. kikao cha leo kilikuwa na agenda gani?
  6. ni kweli anasubiri baraka za rais?
  7. ilikuwa sanaa?
  8. au ni mchezo gani unataka kufanyika hapa?
  9. kwanini spika kaahirisha bunge bila kuusoma muongozo uliohusu ufafanuzi wa serikali juu ya suala hili?
  10. kwanini wameiacha nchi katika sintofahamu kiasi hiki?

ahadi yake ni jumatatu

tunaendelea kusubiri


adios


mizengo pinda ni mwadilifu,shida yuko ndani ya mfumo 'corrupt'kwa busara mi nashauri pinda ajiuzuru amwachie zigo kikwete,mananaona alijitahifi huko nyuma jk akiwa brazil,lakini sasa anarudishwa nyuma,hivyo basi ili aheshimike atoke ndani ya mfumo unaolinda majambazi wanaokwiba fedha za umma mchana kweupe,ripoti ya mkaguzi wa serikali inaonyesha wazi ni ufisadi wa kutisha na rais anaona ni kama mchezo tu.pinda tafadhali jiuzuru.
 
Katika kufitikia uamuzi jumatatu,analazimika kueleza,pamoja na mambo mengine, hatma yake kisiasa na iwapo tunaweza kuendelea kutumia mfumo wa utawala wa kuwa na Waziri Mkuu asiye na madaraka makubwa kiutawala,wakati huo huo,akihitajiwa kueleza masuala ya ndani kabisa ya serikali,na kufanya maamuzi muhimu ya kiserikali kuhusu watendaji wake waandamizi ,huku Rais akirundikiwa mamlaka makubwa ya kiutawala na akiwa pia ni Mwenyekiti wa Chama Tawala.
 
Mnafikiri kitatokea nini kwa Mkw-ere? Mimi naona kama yupo safe sana. Maana hakuna kura ya kutokuwa na imani na Rais. Kama katiba ingeruhusu kupiga kura ya aina hiyo, kwa hakika Kikwete asingekuwa salama. Lakini kutokana na katiba yetu ilivyo, sidhani kama anaweza kuguswa na lolote, na ukizingatia uoga wa watanzania.

TAHRIR SQUARE, PERIOD! Hakuna katiba au sheria yenye nguvu kuliko NGUVU YA UMMA!
 
Katika kufitikia uamuzi jumatatu,analazimika kueleza,pamoja na mambo mengine, hatma yake kisiasa na iwapo tunaweza kuendelea kutumia mfumo wa utawala wa kuwa na Waziri Mkuu asiye na madaraka makubwa kiutawala,wakati huo huo,akihitajiwa kueleza masuala ya ndani kabisa ya serikali,na kufanya maamuzi muhimu ya kiserikali kuhusu watendaji wake waandamizi ,huku Rais akirundikiwa mamlaka makubwa ya kiutawala na akiwa pia ni Mwenyekiti wa Chama Tawala.

Huwezi kuwa na executive president na hapo hapo ukawa na executive pm. Moja kati ya hizo nafasi mbili lazima iwe ceremonial. Je Pinda ni ceremonial pm?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom