Lukolo
JF-Expert Member
- Dec 2, 2009
- 5,143
- 3,196
Ninaamini kwamba wengi wenu mtanipinga kwa kuwa mnamwona Pinda ni mpole, mwenye hekima na asiyependa kupayuka hovyo. Lakini kwa mtizamo wangu, baada ya nchi kuwa na Rais asiye mtendaji, tulipaswa kuwa angalau na waziri mkuu anayeziba mapungufu ya Rais. Lakini huyu waziri mkuu alivyo, ni bora hata ya Kikwete mwenyewe. Ni waziri mkuu asiye na maamuzi, kila jambo atajibu "nafikiri" (nafikiri kuna haja ya kupunguza matumizi serikalini - majibu yake haya) hana majibu na mamlaka ya kuagiza kama waziri mkuu. Hajitambui wala hajui kama yeye ndiye msimamizi mkuu wa mawaziri wote. Hana sauti wala hawezi kuwakemea mawaziri wake. Wakati tunalalamikia utendaji wa baadhi ya mawaziri wa Kikwete, ni vema pia tukasema ule ukweli kwamba huo utendaji mbovu wa mawaziri wengine unaanza na Pinda mwenyewe.
Ukiangalia serikali zote zilizopita, kulikuwa angalau kuna mmojawapo kati ya Rais au waziri mkuu ambaye alikuwa na nguvu sana kumshinda mwenzake na alikuwa na uwezo mkubwa wa kufanya maamuzi ya haraka kwa niaba ya serikali. Sasa hawa tulionao hakuna mwenye unafuu kuliko mwenzie. Huyu ni waziri mkuu aliyeshindwa kusimamia project yoyote ya serikali. Ameanzisha Kilimo kwanza kwa gharama kubwa, akawaacha mawakala wanaiba pembejeo matokeo yake project imekufa bila kuleta mafanikio yoyote. Jana tumesikia wilaya 56 zina upungufu wa chakula. Hicho kilimo kwanza kimetusaidiaje? Kama JK anataka kufanya mabadiliko yoyote ya mawaziri, basi na waziri mkuu pia amuondoe. Huyu bwana ni mzigo mwingine kwa serikali.
Ukiangalia serikali zote zilizopita, kulikuwa angalau kuna mmojawapo kati ya Rais au waziri mkuu ambaye alikuwa na nguvu sana kumshinda mwenzake na alikuwa na uwezo mkubwa wa kufanya maamuzi ya haraka kwa niaba ya serikali. Sasa hawa tulionao hakuna mwenye unafuu kuliko mwenzie. Huyu ni waziri mkuu aliyeshindwa kusimamia project yoyote ya serikali. Ameanzisha Kilimo kwanza kwa gharama kubwa, akawaacha mawakala wanaiba pembejeo matokeo yake project imekufa bila kuleta mafanikio yoyote. Jana tumesikia wilaya 56 zina upungufu wa chakula. Hicho kilimo kwanza kimetusaidiaje? Kama JK anataka kufanya mabadiliko yoyote ya mawaziri, basi na waziri mkuu pia amuondoe. Huyu bwana ni mzigo mwingine kwa serikali.