Pinda na kauli tata kuhusu gesi

Dingswayo

JF-Expert Member
May 26, 2009
4,019
2,923
Waziri Mkuu Pinda alinukuliwa katika vyombo vya habari kuwa serikali ilikuwa imekosea katika suala la gesi kwa sababu hawakutoa taarifa kamili kwa wananchi wa Mtwara kuhusu matumizi ya gesi. katika taarifa ya habari ya ITV, ameonekana akisema kuwa matukio ya Mtwara ni kutokana na uchochezi wa watu kadhaa. Taarifa yake hii inatoa kauli ambazo zinapishana, kwa vile kama serikali ilikosea na wakasema hivyo, hakuna haja ya kutupa lawama kwa wengine. Inashangaza ni jinsi gani serikali hii inataka kuonyesha kuwa kila mara iko sawa katika maamuzi hata kama sivyo.

Taarifa aliyoitoa Waziri Mkuu Pinda kwenye vyombo vya habari amepotosha uma kwa makusudi. Pinda ameenda Mtwara kusikiliza madai ya wana Mtwara,katika madai yaliowasilishwa na makundi mbali mbali hakuna hoja hata moja iliyojibiwa bali ni usanii uliendelezwa kama kawaida kwa mawaziri wake kuelezea mambo kwa mdomo bila vitendo.

Mh. Pinda ameleza vyombo vya habari kuwa amefanya mazungumzo na wananchi wa Mtwara na wamefikia maridhiano. Suala hilo si kweli Mh. Pinda amazungumza na makundi mbali mbali ya wawakilshi kwa wananchi hivyo kama ni kweli wale ni wawakilishi waliotumwa na wananchi inapaswa hao wawakilishi waende sasa kwa wananchi watoe taarifa/wawaeleweshe juu ya hayo mazunguzo kisha wananchi waamue/wapime hayo mazuri walioelezewa na Mh. Pinda. Alichokifanya Mh. Pinda ni kwamba anahalalisha kuwa madai yale sio ya Wananchi bali ni ya Wawakilishi wa makundi mbalimbali ya kijamii.

Kilichoshangaza kwenye serikali hii juu ya sakata hili ni kuwa wakati Mh. Pinda anazungumza na wawakilishi wa makundi mbalimbali huko Mtwara, kwa upande wa wizara yenye dhamana ya masuala ya Gas Waziri Prof. Muhongo anazungumza kwa kejeli kwenye kipindi cha nipashe Radio One na jioni yake Naibu Waziri Simbachawene (Kipindi cha Dakika 45 ITV) anawatisha wananchi kuwa ikiwezekana nguvu ya dola itatumika kupeleka Gas Dar.

Suala la Gas Mtwara ndio kwanza linaanza kwa mchezo mchafu serikali inaoufanya. Mh. Pinda kwenye mkutano ule ulijichanganya ukasema "Wananchi hawakueleweshwa vyema kwamba Kiwanda cha kusafishia GAS kitajengwa Madiba -Mtwara " ,Hapo ni kama uliwatusi tena wana Mtwara, Mh. Jk bosi wa Pinda alitamka wazi kiwanda kitajengwa kinyerezi na ndipo uzinduzi na sherehe ilifanyika. Kwa hiyo hilo la kujenga plant ya kusindika na kusafisha Gas Mtwara ni jipya.

Kwenye RCC ya Mtwara mwaka jana ,yalifikiwa maamuzi kuwa makao makuu ya TPDC yajengwe Mtwara hilo hujalizungumzia kwa kuwa unajiua fika Gas itapelekwa Dar/Bagamoyo so makao makuu yatakua huko huko.

Serikali ya JK imefanya usanii kwenye mengi sana ila kwa hili serikali isikurupuke kucheza na vyombo vya habari kupotosha uma ili wana Mtwara waonekane wabinafsi/wapuuzi. Kumbuka watu walioongea na waziri Mkuu Pinda kwa minajili ya kufikisha ujumbe kwa wananchi waliisii Serikali wasitishe kwanza mpango wao wa kupeleka Gas kwani mradi wenyewe umeonyesha una utata. Makundi hayo Maaskofu/wachungaji,Maimamu/Mashekh,Wafanyabiashara,WanaCCM(kamati ya Ushauri ya Mkoa) ,Wenyeviti wa Vijiji na Madiwani,Wawakilishi wa asasi za kirai na Viongozi waandamizi wa serikali pamoja na vyama vya upinzani. Makundi haya sio ya kupuuzwa kwa wewe kujitapa kuwa umepata suluhu ili hali hawajapeleka mrejesho.

Hili swala likilazimishwa litaleta madhara makubwa kwani wananchi Mtwara wanasema wazi kuwa makubaliano yale kama yalifanywa wao hawayatambui kwani hayajawafikia. Migogoro ya namna hii ikipuuzwa huwa ni sumu kwa maendeleo ya nchi na ustawi wa utawala bora.

Subira huvuta heri na pia Uhondo wa ngoma ingia ucheze. Prof. Muhongo alisema wana Mtwara wanacheza ngoma wasioijua akasahau ngoma nyingi za asili zinapatikana kusini na ni jadi yao(Ngoma ni utajiri wa wanakusini-Rejea Makuya festival).

Mungu ibariki Tanzania.
 
Hiki kigeugeu cha serikali kinaweza kuwageuza watu wa mtwara wakaanzisha timbwili tena kwa kuamini kuwa wanapakwa mafuta kwa mgongo wa chupa. Kama serikali imekosea isione aibu kukiri na kuomba radhi.

Kwani kuna ubaya gani kuwachochea wananchi kudai jaki yao? Mbona serikali yenyewe kila mara huwa inawachochea wananchi ili wajiletee maendeleo yao wenuyewe!
 
Ndo maana CHADEMA kupia Godbless Lema wameahidi kurudi Mtwara kuwahabarisha wanamtwara deal yote ya gesi na uhusika wa Kinana na CCM katika ufisadi huo wa Pinda na wenzake.
 
Waziri Mkuu Pinda alinukuliwa katika vyombo vya habari kuwa serikali ilikuwa imekosea katika suala la gesi kwa sababu hawakutoa taarifa kamili kwa wananchi wa Mtwara kuhusu matumizi ya gesi. katika taarifa ya habari ya ITV, ameonekana akisema kuwa matukio ya Mtwara ni kutokana na uchochezi wa watu kadhaa. Taarifa yake hii inatoa kauli ambazo zinapishana, kwa vile kama serikali ilikosea na wakasema hivyo, hakuna haja ya kutupa lawama kwa wengine. Inashangaza ni jinsi gani serikali hii inataka kuonyesha kuwa kila mara iko sawa katika maamuzi hata kama sivyo.

Waziri Mkuu anayeitwa Mizengo Kayanza Peter Pinda hajawahi kuongea jambo lilonyoka hata mara moja tangu awe Waziri Mkuu wa nji hii!!!Katika awamu zote tangu nji hii ipate uhuru huyu ndiye PM DHAIFU KULIKO WOTE!!!!

Ni huyuhuyu PM aliyemwaga mchozi akiwalilia MAALBINO badala ya kutoa maamuzi kama Mkuu wa shughuli za Serikali. Ni huyuhuyu PM aliyesema uongo Bungeni kuhusu MAUAJI YA WATANZANIA 2 na Mkenya 1 kule Arusha wakti wa maandamano ya AMANI!!!

Kawaida ya Pinda ni UNAFIKI,UONGO na UKINYONGA(kigeugeu)! Hii tabia hata Kikwete anayo. Kwamba anapozungumza hataki kuonekana anaumiza upande fulani hata akijua ukweli na uongo wa jambo lile. Pinda ni kama MPIGA RAMLI ambaye huanza kwa kusoma Tabia ya mhanga(mgonjwa wake) kwa kujua anataka nini na kuanza kuzungumzia shida zake na mahitaji yake ili kumridhisha na hatimaye kumtoa upepo(malipo).

Hii ni tabia ya Viongozi wa Serikali ya CCM almost wote (99.999%!) Kucheza na akili za Watanzania kwa kusoma hali ya hewa na mazingira ya wakti wa tukio husika!!Tabia ya kinyonga kubadili rangi kulingana na pale alipo kwa wakti husika ili kumhadaa adui yake!!!
 
This does not make sense to me. Kwa nini walitoa taarifa nusu?

Kwa nini basi mawaziri wake akiwemo wa wizara husika hakuitoa hiyo taarifa walipoulizwa?

Kwa nini walificha hiyo taarifa ya kujenga hicho kiwanda?

Halafu serikali hiyo hiyo inatuambia kuwa ipo kwenye global open governmnet partnerhip ya ku-promote transparency, empower citizens na kupambana na rushwa?

Either kulikuwa hakuna mpango wa kujenga hicho kiwanda, ndo sasa wanataka kufanya hivyo baada ya wananchi kuja juu au ni danganya toto.

In either way, hapa wananchi wa Kusini wanapoozwa tuu.
 
Mzalendo2015

Natafuta kitufe cha LIKE sikioni, moderator naomba msaada tafadhali maana Mzalendo 2015 kaongea facts tupu hapa.
 
Last edited by a moderator:
kubali niliyosema kwamba,ccm na serikali yake kila wamachosema ni kwa hila hivyo wanazidi kujivua nguo,hawana uwezo tena wa kuongoza nchi hii
 
Umenena mkuu. Mods unganisheni hii thread na ile ingine ya Dingswayo, tafadhalini! Naomba radhi kama kuna niliowakwaza.
 
Mtu mzima anapofanya makosa na kuanza kumtupia mtu lawama kwa makosa yake ni upuuzi... Kwa kauli hii ya pinda maana yake ni kuwa wana mtwara hawana uwezo wa kutafakari yaliyo mema kwao.
 
Ndo maana CHADEMA kupia Godbless Lema wameahidi kurudi Mtwara kuwahabarisha wanamtwara deal yote ya gesi na uhusika wa Kinana na CCM katika ufisadi huo wa Pinda na wenzake.
hayo ndio maneno,alafu wananchi wa mtwara wakielewa ukweli,wakizidi kudai haki,itaundwa tume nyingine na pinda atakwenda tena mtwara
 
Serikali imeshindwa kusoma alama za nyakati long gone are the days za ndio mzee. Serikali ijiandee kujibu tena maswali ya Wanamtwara na Watanzania wengine and they better come with solutions and not anwers this time kwani jinsi ninavyoona picha ndo kwanza inaanza hili ni trailer!
 
Waziri Mkuu anayeitwa Mizengo Kayanza Peter Pinda hajawahi kuongea jambo lilonyoka hata mara moja tangu awe Waziri Mkuu wa nji hii!!!Katika awamu zote tangu nji hii ipate uhuru huyu ndiye PM DHAIFU KULIKO WOTE!!!!
Ni huyuhuyu PM aliyemwaga mchozi akiwalilia MAALBINO badala ya kutoa maamuzi kama Mkuu wa shughuli za Serikali. Ni huyuhuyu PM aliyesema uongo Bungeni kuhusu MAUAJI YA WATANZANIA 2 na Mkenya 1 kule Arusha wakti wa maandamano ya AMANI!!!

Kawaida ya Pinda ni UNAFIKI,UONGO na UKINYONGA(kigeugeu)! Hii tabia hata Kikwete anayo. Kwamba anapozungumza hataki kuonekana anaumiza upande fulani hata akijua ukweli na uongo wa jambo lile. Pinda ni kama MPIGA RAMLI ambaye huanza kwa kusoma Tabia ya mhanga(mgonjwa wake) kwa kujua anataka nini na kuanza kuzungumzia shida zake na mahitaji yake ili kumridhisha na hatimaye kumtoa upepo(malipo).

Hii ni tabia ya Viongozi wa Serikali ya CCM almost wote (99.999%!) Kucheza na akili za Watanzania kwa kusoma hali ya hewa na mazingira ya wakti wa tukio husika!!Tabia ya kinyonga kubadili rangi kulingana na pale alipo kwa wakti husika ili kumhadaa adui yake!!!
AKHSANTE,yaani ni hatari hawa jamaa hawaa!yaani WEKA MBALI EVRTHING & KAA MBALI EVRBODY.Ninadhani ndo hawa Babu yetu Mwal NYERERE alisema ni wa kuogopa kama ukoma.
 
Ninahisi/nadhani serikali itakuwa na mpango kutangaza 'hali ya hatari' nchini ili kuvuruga masuala mbalimabali yanayoendeala na kutarajiwa yaani mchakato wa kupata katiba mpya, uchaguzi wa serikali za mitaa 2014 na uchaguzi mkuu 2015. Kwani kwa kutangaza hali ya hatari itaamua kufanya itakavyo bila 'bughudha'. Ni nadhani namna hii kwa sababu kwa maelezo yote waliyopewa na ndugu zetu wa wanamtwara juu ya wanachokitaka sikutegemea tena serikali ije tena kauli za kutiliwa mashaka.
 
Back
Top Bottom