Crocozilla
JF-Expert Member
- Oct 17, 2012
- 469
- 335
Kwa kauli aliyotoa Pinda jana bungeni, inatosha kabisa pasi na shaka kukosa vigezo vya kugombea nafasi ya juu kabisa ya kuongoza nchi hii.
Nasema hivyo kwa sababu ameonekana wazi wazi kutoka kuzima jambo hili kwa maslahi binafsi ama yeye mwenyewe au kulinda kundi la watu waalifu na wezi.
Kwa nchi yenye watu makini swali ni moja tu, kama kwa nafasi yake kwa waziri mkuu na matarajio yake ya urais ameweza kudiriki kufanya vile je akipewa nafasi hiyo kubwa ataficha maovu mangapi na wakati huo atakuwa na rungu la kufanya hivyo?
Pinda umeshindwa kabisa kusoma alama za nyakati kweli? Natamani ungejua sisi wananchi tunakuonaje huku kitaa.
Hakika umekosa sifa, umekosa upako, umekosa weledi na zaidi umekosa wofu ya Mungu!
Pinda umejitoa mwenyewe katika kinyang'angiro cha urais.
Pinda sasa hata ubunge si halali yako kwani ukifika bungeni unaweza kukosa nafasi ya uwaziri na si hekima kwa mtu aliyekuwa waziri mkuu!
Pinda jana ilikuwa tarehe 20/11/2014 hutasahau tarehe hii!
Nasema hivyo kwa sababu ameonekana wazi wazi kutoka kuzima jambo hili kwa maslahi binafsi ama yeye mwenyewe au kulinda kundi la watu waalifu na wezi.
Kwa nchi yenye watu makini swali ni moja tu, kama kwa nafasi yake kwa waziri mkuu na matarajio yake ya urais ameweza kudiriki kufanya vile je akipewa nafasi hiyo kubwa ataficha maovu mangapi na wakati huo atakuwa na rungu la kufanya hivyo?
Pinda umeshindwa kabisa kusoma alama za nyakati kweli? Natamani ungejua sisi wananchi tunakuonaje huku kitaa.
Hakika umekosa sifa, umekosa upako, umekosa weledi na zaidi umekosa wofu ya Mungu!
Pinda umejitoa mwenyewe katika kinyang'angiro cha urais.
Pinda sasa hata ubunge si halali yako kwani ukifika bungeni unaweza kukosa nafasi ya uwaziri na si hekima kwa mtu aliyekuwa waziri mkuu!
Pinda jana ilikuwa tarehe 20/11/2014 hutasahau tarehe hii!