Pinda hafai tena kugombea urais !

Pinda hafai tena kugombea urais !

Kwa kauli aliyotoa Pinda jana bungeni, inatosha kabisa pasi na shaka kukosa vigezo vya kugombea nafasi ya juu kabisa ya kuongoza nchi hii.

Nasema hivyo kwa sababu ameonekana wazi wazi kutoka kuzima jambo hili kwa maslahi binafsi ama yeye mwenyewe au kulinda kundi la watu waalifu na wezi.

Kwa nchi yenye watu makini swali ni moja tu, kama kwa nafasi yake kwa waziri mkuu na matarajio yake ya urais ameweza kudiriki kufanya vile je akipewa nafasi hiyo kubwa ataficha maovu mangapi na wakati huo atakuwa na rungu la kufanya hivyo?

Pinda umeshindwa kabisa kusoma alama za nyakati kweli? Natamani ungejua sisi wananchi tunakuonaje huku kitaa.

Hakika umekosa sifa, umekosa upako, umekosa weledi na zaidi umekosa wofu ya Mungu!

Pinda umejitoa mwenyewe katika kinyang'angiro cha urais.
Pinda sasa hata ubunge si halali yako kwani ukifika bungeni unaweza kukosa nafasi ya uwaziri na si hekima kwa mtu aliyekuwa waziri mkuu!

Pinda jana ilikuwa tarehe 20/11/2014 hutasahau tarehe hii!



Aliyekuwa mwanasheria mkuu wa serikali Andrew Chenge alipewa dola milioni 1 za ESCROW sawa na bilioni 2 kasoro za kitanzania imefahamika.-

Chenge ambae alikua mwanasheria mkuu wa serikali wakati mkataba wa IPTL unasainiwa miaka ya 1990 amekiri kupokea kiasi hicho cha pesa kutoka kwa mwanahisa wa IPTL Rugemalila ambae alikua na hisa 30%. Chenge ambae ni mbunge wa Bariadi amekiri kupokea pesa hizo akidai kuwa ni malipo ya kazi ya ushauri aliyoifanya kwa Rugemalila. Hata hivyo hakuna ushahidi wa kuwepo kwa mkataba wowote baina ya mwanahisa huyo na Chenge. Mwanasheria aliyekuwa anaishauri na kuiwakilisha IPTL kwa ujumla akiwemo mwanahisa Rugemalila ni Dr. Ringo Tenga ambae alilipwa pesa zake.-

Chenge ambae ni mtu wa karibu sana na waziri mkuu wa zamani Edward Lowassa ndiye mtu anayetajwa kuwa chaguo la nafasi ya waziri mkuu ikiwa Lowassa atakua Rais wa Tanzania. Hii ni kutokana na urafiki na mchango mkubwa wa mali na maarifa anaoutoa Chenge katika kusaidia harakati za Lowassa.-

Andrew Chenge ndiye mwalimu wa mwanasheria mkuu wa sasa Jaji Frederick Werema. Wakati Chenge akiwa Mwanasheria mkuu wa Serikali, Jaji Werema alikua afisa wa sheria wa serikali "State Attorney".
Haijajulikana kama malipo hayo ni ya Chenge mwenyewe au ni nani aliye nyuma ya Andrew Chenge. Aidha Haijajulikana kama Chenge hakuwa mchoraji mkuu wa namna gani uporaji huu ufanyike ikizingatia kuwa kashfa nyingi zilizotokea miaka ya karibuni zilitokea yeye akiwa mwanasheria mkuu wa serikali. Hizi ni kama ununuzi wa Rada na Buzwagi.
 
Pinda ni janga, wala hajitambui;ni baadhi ya watu wachache walijisemea tu kuwa pinda hana kashfa hivyo anauzika kumbe hawajui Mungu humfichua mnafki,leo huyu jamaa kajidhiirisha kuwa hafai,hafai hata kidogo, nchi kama hii inahitji viongozi wenye msimamo usio yumba yumba kama siyo kupinda pinda kama Pinda, nadhani hata sita amemzidi Pinda kwa point chache kama siyo wanalingana. Sasa basi nani anaweza uzika huko ccm,kwanza wanaogopana hii itatoa watu roho,sisi tusubiri.
 
ya kwa tiketi ya CCM anafaa.ila kwa ajili ya kulitoa Taifa lilipo hatufai
 
Nimuda sasa watanzania na ulimwengu mzima ukijiuliza nani anayehusika na hali hii ya sitofahamu ya IPTL na wengi wetu tukiwa na hamu kubwa ya kutaka kujua nani wa kufungwa kengere kwa hili.ila wasi wasi wa watanzania tuliowengi ni kwamba tusije pigiwa ngoma tusiyoijua mapingo yake kisha tukaaza kufunga vibwebwe na kucheza.hapa nikiwa naama kuwa swala hili tusije changanyiwa na harakati za uraisi 2015.kwani hili limejitokeza baada ya kuona jinsi gani mh mizengo pinda anavyotupiwa makombora na wanasisa wenzake ndani na nje ya chama je wanasiasa wetu wanajua wanachofanya kuwa hakina mashiko ndani na nje ya chama coz watanzania wa sasa nitofauti sana na wale wa miaka 5 iliyopita.kwani tonao uwezo wa kuhoji na kufafanua jambo hivyo nivyema wanasiasa wetu wakalijua hili na kuacha moja kwa moja tabia ya kitoto kama wanayofanya sasa.kwani hili naamini haliwezi kumjumbisha mh pinda na chama chake kwa ujumla kwani naamini wamejipanga vizuri kwa hili .na wale wanayumba kimawazo kama mh kagasheki ni watu wanaopaswa kuombewa na kwenye chama kuchukukiwa hatua kali za kisheria.kwani watanzania wanajua yote yanayoendelea ndani ya nchi yao hivyo kama wanasisa au mtanzania yoyote ambaye hana la kusema nibora wakae silent nasio kulipotosha taifa.kwa mimi naona sasa kinachomfanya pinda kunyooshewa mikono sio kuhusika na iptl bali ni kutokana kuwa kaa la moto katka harakati za kugombea uraisi ila mimi naamini kuwa uongozi hutolewa na mungu hivyo hata tumpinge vita kwakila njia kama mungu amemuandikia awe katka nafasi yoyote atakuwa tu.na nivyema watanzania tukajitambua na kutambua mambo kabla ya hawa wanasisa wetu wa maji taka hawajaaza kutupotosha .namalizia kwakusema naipenda nchi yangu na naipenda serikali yangu ya jamhuri ya muungano wa tanzania.na pia mungu ambariki waziri wetu mkuuu na viongozi wandamizi wa serikali yetu ya muungano wa watanzania.
 
Miradi mnayopewa ya kusafisha mafisadi fanyeni kwa mama zenu na watoto wenu sio humu. Subiri mjadala wa ripoti ukamilike then tutaona cha kufanya. Msianze kuharisha kabla ya kufika chooni
 
Nimuda sasa watanzania na ulimwengu mzima ukijiuliza nani anayehusika na hali hii ya sitofahamu ya IPTL na wengi wetu tukiwa na hamu kubwa ya kutaka kujua nani wa kufungwa kengere kwa hili.ila wasi wasi wa watanzania tuliowengi ni kwamba tusije pigiwa ngoma tusiyoijua mapingo yake kisha tukaaza kufunga vibwebwe na kucheza.hapa nikiwa naama kuwa swala hili tusije changanyiwa na harakati za uraisi 2015.kwani hili limejitokeza baada ya kuona jinsi gani mh mizengo pinda anavyotupiwa makombora na wanasisa wenzake ndani na nje ya chama je wanasiasa wetu wanajua wanachofanya kuwa hakina mashiko ndani na nje ya chama coz watanzania wa sasa nitofauti sana na wale wa miaka 5 iliyopita.kwani tonao uwezo wa kuhoji na kufafanua jambo hivyo nivyema wanasiasa wetu wakalijua hili na kuacha moja kwa moja tabia ya kitoto kama wanayofanya sasa.kwani hili naamini haliwezi kumjumbisha mh pinda na chama chake kwa ujumla kwani naamini wamejipanga vizuri kwa hili .na wale wanayumba kimawazo kama mh kagasheki ni watu wanaopaswa kuombewa na kwenye chama kuchukukiwa hatua kali za kisheria.kwani watanzania wanajua yote yanayoendelea ndani ya nchi yao hivyo kama wanasisa au mtanzania yoyote ambaye hana la kusema nibora wakae silent nasio kulipotosha taifa.kwa mimi naona sasa kinachomfanya pinda kunyooshewa mikono sio kuhusika na iptl bali ni kutokana kuwa kaa la moto katka harakati za kugombea uraisi ila mimi naamini kuwa uongozi hutolewa na mungu hivyo hata tumpinge vita kwakila njia kama mungu amemuandikia awe katka nafasi yoyote atakuwa tu.na nivyema watanzania tukajitambua na kutambua mambo kabla ya hawa wanasisa wetu wa maji taka hawajaaza kutupotosha .namalizia kwakusema naipenda nchi yangu na naipenda serikali yangu ya jamhuri ya muungano wa tanzania.na pia mungu ambariki waziri wetu mkuuu na viongozi wandamizi wa serikali yetu ya muungano wa watanzania.

wakati wa porojo umeisha sasa ni wakati wa FACTS; hatuwezi kukaa chini na kuanza kujadili mambo ya urais wakati kuna swala zito la wizi...wakati mwingien tumia akili yako hata kidogo...
 
Miccm yote hakuna hata mmoja anaefaa kuugombea Uraisi ,kiufupi miccm haifai kugombea hata ubunge wacha uraisi.
 
Kwa kauli aliyotoa Pinda jana bungeni, inatosha kabisa pasi na shaka kukosa vigezo vya kugombea nafasi ya juu kabisa ya kuongoza nchi hii.

Nasema hivyo kwa sababu ameonekana wazi wazi kutoka kuzima jambo hili kwa maslahi binafsi ama yeye mwenyewe au kulinda kundi la watu waalifu na wezi.

Kwa nchi yenye watu makini swali ni moja tu, kama kwa nafasi yake kwa waziri mkuu na matarajio yake ya urais ameweza kudiriki kufanya vile je akipewa nafasi hiyo kubwa ataficha maovu mangapi na wakati huo atakuwa na rungu la kufanya hivyo?

Pinda umeshindwa kabisa kusoma alama za nyakati kweli? Natamani ungejua sisi wananchi tunakuonaje huku kitaa.

Hakika umekosa sifa, umekosa upako, umekosa weledi na zaidi umekosa wofu ya Mungu!

Pinda umejitoa mwenyewe katika kinyang'angiro cha urais.
Pinda sasa hata ubunge si halali yako kwani ukifika bungeni unaweza kukosa nafasi ya uwaziri na si hekima kwa mtu aliyekuwa waziri mkuu!

Pinda jana ilikuwa tarehe 20/11/2014 hutasahau tarehe hii!

Ina maana alikuwa anafaa machoni pako na wakwe zako?mimi naona atafaa tu,mbona Lowassa alijiuzulu kwa kashfa ya Richmond,lakini leo hii tafiti zinasema ndiye kipenzi cha watanzania.Shame on them.
 
Hela za Escrow ndio zilizokuwa zinampa kiburi cha kuanza kampeni sasa ngoja ngoja ang'olewe meno bila ganzi bungeni
 
Ebu toeni maelezo kwa namna gani PINDA anahusika katika ufisadi huo?

Wewe kweli nanga unataka maelezo gani? Hujui nafasi ya waziri mkuu katika serikari?rudi darasani usome Civics ya kidato cha pili,siyo kusumbua watanzania wakati kama huu wa msiba.
 
Back
Top Bottom