Pinda: Dowans hatuirudishi bungeni

Huwa najiuliza swali moja kama Serikali awali iliambiwa na ICC ilipe Bilioni 185 wakasema hapana tutalipa Bilioni 94 hivi kuna ku-negotiate, halafu kwanini deni limepungua kutoka 185 mpaka 94 kama siyo watu wanapika mambo na kuwataka watanzania waamini kwamba kila kinachofanyika kinafuata sheria btw sijwahi kuona nchi inalazimisha kulipa deni tena kwa haraka sana nashangaa sana. Wonders will never end
 
Waandishi wa habari wa Tanzania wamejawa na ulimbukeni kwanini hawajauliza hatma ya wastaafu wa East Africa Community? Kwanini wasingeuliza mbona Valambia hajalipwa na Serikali licha ya mahakama ya rufaa kuamuzru alipwe? Something fishy here anyway nilikuwa napita tu nikasimama kidogo ngoja niendelee na misafara yangu...

Ungesema Waandishi wa Mafisadi maana mafisadi wana media what do you expect can you write against Rostam wakati yeye ndiyo anakulipa mkono uende kinywani
 
Good move mzee Pinda. Kama kisheria tunatakiwa kulipa tuwalipe otherwise deni litakuwa kubwa tutashindwa kulipa matokeo yake tutabakia kugawa rasilimali zetu kama pipi kwa mafisadi.

I am sorry to say this but it seems you are CRIPPLE MINDED
 
Good move mzee Pinda. Kama kisheria tunatakiwa kulipa tuwalipe otherwise deni litakuwa kubwa tutashindwa kulipa matokeo yake tutabakia kugawa rasilimali zetu kama pipi kwa mafisadi.

Hivi madeni ya wastaafu wa E.Africa community yamepungua eeh! Inawezekana kugawa rasilimali zetu kwakuwalipa hawa wazee pia au ni DOWANS peke yao?
 
JK na Pinda ndio Waamuzi wa Mwisho wa Taifa zima la Tanzania? Unajua hapo zamani za kare hata Nyerere alifanya haya makosa ya kuburuza wananchi na kutotegemea push back...Jk na Pinda wanafikiri hii generation yetu tutakaa kimya na kwenda kulala...I think Pinda is dream Mugabe's dream. Bunge will discuss Dowans and they are not going to choose venue for our fight.
 
Pinda kapinda! Hana jeuri ya kukaidi mafisadi...si ndiye alisema wanaweza kuyumbisha nchi? Kajamaa kaovyo haka!
 
Good move mzee Pinda. Kama kisheria tunatakiwa kulipa tuwalipe otherwise deni litakuwa kubwa tutashindwa kulipa matokeo yake tutabakia kugawa rasilimali zetu kama pipi kwa mafisadi.

Mi Nasema hivi. Kama Dowans waongelee wanaume, sio Pinda. Maswali mawili tu la tatu michozi na mikamasi. We subiri...
 
[
"Hatutalipeleka suala hili bungeni….kulipeleka huko itakuwa ni kwenda kujadili siasa na si sheria. Na kwa hili tayari kuna timu ya wabunge wa CCM ambao ni watalaamu wa sheria pamoja na timu itakayoundwa na serikali, timu hizo zitakaa na kupitia kwa makini suala hili ili twende tukatafute ufafanuzi huo wa kisheria," alisema Pinda.[/COLOR][/SIZE][/FONT]

PINDA. hapo kwenye quote ndo siasa yenyewe hiyo. Unaleta porojo za kukwepa kuwajibika na mnapozidi kulizamisha hili suala kwenye kapeti za sisiem hesabuni mpo kwenye fungu la kukosa. Sijawahi kuona utawala wa sheria unashabikia uhalifu kama serikali yako.. Kumbuka bunge hutunga sheria hivyo lina haki ya kujadili ishu yeyote ya kisheria inapobidi.
Au pinda hujui kazi ya bunge??????



Pia unaposema mmeunda kamati ya wabunge wa sisiemu kujadili na kushauri je tujue kwamba:
  1. hao wabunge wamechaguliwa na ccm au wananchi?
  2. Kamati ni kwa maslahi ya chama kama ulivyowafunda hapo blue pear kuwa mnaangalia maslahi ya chama kwanza. mnajitahidi kuficha nini hapo??? kumbuka kuwa sisi mererly people tunafehemu mengi ktk hili suala maana kimya chenu kimetusukuma kutafuta ukweli kwa njia tuzijuazo
  3. kwa nini DOWANS iundiwe kamati ya wabunge nje ya bunge na si ndani ya bunge???
  4. Kwa kuwa sakata la DOWANS lilianzia bungeni na serikali ikawajibishwa je kuna kigugumizi gani kurudisha hoja bungeni??? maana kwanza hakuna azimio hata moja la Bunge mlilotekeleza ingawa mlimtosa LOWASA na wenzake lakini mkabakia kukumbatia DHAMBI na inawatafuna...
PINDA, nimesoma mahala kuwa mmewafunda wabunge wa ccm kujibu hoja za wapinzani bungeni, je kwa nini basi msiwape uwaziri wabunge wooote wa sisiem? ina maana kumbe watoa hoja ni wapinzani na sisiemu kazi yenu ni kupangua hoja!!! Mawaziri kazi yao ni nini bungeni?? na ina maana mmewafunga mdomo wabunge wa ccm???

KWELI CHAMA SHIKA HATAMU
 
Nilishasema mara nyingi na leo narudia,pinda si chochote si lolote,yeye kama pm katoa wapi mamlaka ya kukataa au kukubali hoja ingiie au isiingie bungeni?huu ni uhuni na wendawazimu,ni mtu asiyekuwa mzalendo tu ndo anaweza kutetea malipo ya dowans,pinda katika hili hatutakusamehe
 
Pinda is just another fisadi.

wanaJF,

Leo hii Pinda amekuwa fisadi?
Juzi na jana mlisema ni mtu safi, mtoto wa mkulima..... sisi wengine tulisema ,jamani katika CCM ni tabu sana kupata mtu safi. Mulitung'akia.

System hapa Tz imejengwa kwa style ya ajabu ajabu, short cut ya kupata deals, kuganga njaa au kupata fursa zozote kwa urahisi basi ni lazima uwe mwanaCCM... sio wote walioCCM kuwa wanapenda CCM , lakini CCM ndio ufunguo wa maisha kwa TZ.

Sasa ukiwa mwanaCCM ni lazima uwe na sifa ya ukondoo, ukubali kuchakachuliwa au wenyeCCM watakunyamazisha kwa style za Kolimba, au watakuteua katika nafasi ambayo utang'angana fupa tu, ukipenda usipende.

CCM haina machanism ya kujisafisha, ni kuchafua na kujichafua tu!
Kama leo ,Pinda amekuwa "fisadi" basi ni kuwa amehitimu mafunzo ya uanachama wa CCM kama hamukulijua hilo kabla.

Kama kuna wengine munafikiri ni safi katika CCM subirini "surprises" za nguvu. Welcome to TZ, Nchi ya katiba ya Chama kimoja! Nchi ya amani na utulivu.
 
ivi Pinda anaweza kuzuia bunge kujadili kitu chochote? Chadema wapeleke mswada wa malipo kwa Dowans bungeni tuone kama watawazuia!!
Hii serikali inadhani ipo juu ya bunge?
 
DUH !!!!!!!!! HAPA TUMEKWISHA
Nashindwa kupata jibu nani anazungumza kwa niaba ya nani, kwani wote waliotangulia kila mmoja anatoa kauli tofauti kama vile ndio kwanza jambo hili limifika mezani kwake. Naanza kwa kuzungumzia kauli ya waziri mwenye amana, mh Ngeleja ambaye alisikika akisema Dowans ni lazima ilipwe, kauli yake hii ilipingwa vikali na baadhi ya mawaziri wenye uchungu na kodi za watanzania akiwemo Mh. Sita pamoja na naibu waziri Mh.Mwakyembe ambao naweza kuwaita kwamba ni wawakilishi wa wananchi na sio wawakilishi wa matakwa yao binafsi. Baada ya hapo mawaziri wengine wengi waliwashambulia Sitta na Mwakyembe wakidai kwamba hawakuwa na haki ya kuzungumzia swala la Dowans eti kwa kuwa sio wizara yao.Leo hii tena Mh. Waziri Mkuu ndugu Mizengwe Pindwa naye kaja na jipya eti swala la kuilipa au kutoilipa Dowans halitapelekwa bungeni kwa kuwa ni swala la kisheria. Kinacho nichanganya hapa ni kwamba je huko mahakama kuu ni nani atakayekuwa mshtakiwa na ni nani mlalamikaji? Mahakama kuu walishasema kwamba hakuna kesi yoyote kuhusu Dowans iliyokwisha andikishwa na kwa taratibu za mahakama ni lazima kuwepo pande mbili, mdai na mdaiwa, mdai ni Dowans tunamfahamu je mdaiwa ni yupi wakati serikali ilisha ridhia kulipa deni? mbona hapa ni sawa na kesi ya nyani kuharibu mazao halafu jaji awe ni tumbili, kweli hapa haki itatendeka kweli !!!!!!!!! Hii ni danganya toto, serikali ituweke wazi kwa hili tumechoka kudanganywa kila kukicha. Kwanza hebu tujiulize, je serikali yetu haina madeni mengine kuancha hili la Dowans? na hayo madeni yana muda gani mpaka leo serikali haijalipa? Kwanini deni hili liwe livaliwe njuga na kila kiongozi wa nchi? Hapa panma utata mkubwa sana. Naamini kuna madeni mengi ya nyuma tangu enzi za Mwalimu Nyerere lakini mpaka sasa hivi hatujalipa. Achilia mbali madeni mengine ambayo mpaka sasa sasa hivi wananchi wazawa na walala hoi wa Tanzania waliokuwa wafanyakazi wa Shirikisho la Afrika Mashariki wazee wetu ambao hawana uwezo wa kujikimu kwa njia yoyote ile wanaishia kupigwa virungu na kumwagiwa maji ya kuwasha na jeshi la kuwalinda viongozi waserikali na kuwanyanyasa pamoja na kuwauwa wananchi. Je malimbikizo ya likizo za waalimu sio deni kwa serikali, mbona haya yote hayashikiwi bango na viongozi wa serikali? Inapotokea ni madai ya wananchi walala hoi serikali inasema kwamba hakuna pesa ila kwa hili la Dowans pesa zipo !!!!!!! Sisi wananchi watanzania tunazikataa kauli hizi za viongozi walafi wanaotaka kutubebesha mzigo huu mkubwa kwa masilahi yao wenyewe. Kwa kauli hii ya Mh. Pinda inaonyesha kwamba serikali yetu yote ni ya kisanii. Nilitegea kwamba mtoto wa mkulima ( Pinda ) angekuwa pamoja na wananchi wa Tanzania ktk kupinga hili. Sasa napata jibu kwamba huyu alikuwa mtoto wa mkulima kwa kipindi hicho lakini sio sasa. Sasa hivi ni sawa na tone la mafuta lililomwagwa baharini. Inawezekani kauli hii haikutoka kwa utashi wake mwenyewe bali ni kwa shinikizo la viongozi mapapa wa ufisadi. Ila kama ni kwa matakwa yake basi tunaweza kumuweka kwenye kundi la akina .............. tutaanza kuingiwa na uoga kwamba ni hata yeye pia sio mwenzetu (mlala hoi)
Hebu turudi nyuma kidogo, nakumbuka wakati Mh. Pinda anateuliwa kuwa waziri mkuu alianza kwa kasi ya hali juu kwa kuhoji ulali wa serikali masikini kama ya Tanzania kununua magari ya kifarahi na ya bei ya juu kwa ajili ya wabunge na mawaziri (Land Cruiser VX) kasi hii ilitugusa wengi na kuamini kwamba huyu PM atakaye tufaa. Baada ya uchaguzi tumemsikia tena eti ndugu yetu huyu amelikataa gari lake jipya eti kwa kigezo cha kwamba magari hayo ni ya bei kubwa na kwamba hata gari lake la awali bado linamfaa kutumia. Jamani, hebu nisaidiani hapa kwani nahisi kwamba uelewa wangu ni mdogo. Hapa nafananisha na baba aliyenunua chakuala halafu kimeshapikwa eti anagoma kula kwa kuwa ni cha gharama !!!!!!!!!! hivi hili linakuingia akilini kweli? Yeye kama mtendaji mkuu wa serikali alitakiwa kuzuia manunuzi ya haya magari na sio kukataa la kwake ambalo tayari limeshanunuliwa !!!!!!!!! Watanzania tunapatwa na wasiwasi kwa hili, haya ni mazingaumbu, mtoto wa mkulima Pinda amesha tutosa hivyo tunamuomba Mh. Sita pamaoja na Mwakyembe wasimame imara kuhakikisha kwamba Dowans halipwi kitu. Msiogope kutishiwa na viongozi mafisadi wanaojali maslai binafsi kuliko ya wananchi wao. Msifungwe midomo katika kuwatetea wananchi ambao ndio wamewapeleka bungeni kuwawakilisha, tunaamini kwamba kwamba mlicho kizungumza hamkuzungumza kama mawaziri au wana CCM bali mmezungumza kama wawakilishi wa wananchi wa Tanzania walio wapa kura zao. Sisi tutakuwa nyumba yenu, hata kama ni kwa maandamano ya nchi nzima kuhakikisha kwamba kodi na jasho la watanzania halipotelei mikononi wa hawa Dowans. Na hata kama ni lazima tuko tayari kuandamana tukiwa uchi wa mnyama kama vile walivyo ahidi baadhi ya wasanii katika kipindi cha jana Jumanne katika kindindi cha "Wanawake Live" cha chanel 5.
Jamani watanzania amkeni kutetea kodi zetu zisitumike vibaya.
 
  1. Walitingisha kiberiti kuwa uamuzi umetolewa na ICC eti Dowans walipwe 185 bilioni, tukaguna.
  2. Wakagutuka wakadai kuwa haikuwa 185 bilioni bali 95 bilioni, tukaanza kujiuliza kulikoni ?
  3. Wakati hatujakaa sawa wakasema ni lazima tulipe kwani hamna tena ujanja, tukataharuki.
  4. Wakaanza na vitisho na matusi kwa kudai Ikulu haihusiki na sakata la Dowans, tukaguna tena.
  5. Wakitisha kikao cha walaji (CCM) na kubariki malipo kwa matapeli, tukasema wakilipa hapatatosha.
  6. Wakaitisha kikao cha wabunge kuweka mkakati wa pamoja, Mungu si athumani, wakakwama.
  7. Wakaunda kamati ya wanasheria wao wabunge eti kutafuta muafaka, tukaguna kwa sauti kubwa.
  8. Mwanasheria moja, Mkono, fisadi aliyekubuhu ataka tujadiliane na wezi watupunguzie - iwe bil. 50 ?

Hapana Pinda, ujanja umekuishia kwani umegeuzwa kuwa tambala bovu na chafu la kupigia deki ! Dowans iende bungeni tuwajue kwa majina na sura watakaowatetea hawa wezi tu tuwashughulikie kama maadui wa taifa.

KAKA FORMULA TUNAZOTUMIA SISI WANYONGE HAPA MBONA NZURI SANA. jUST IMAGINE TULIAMBIWA DENI LA DOWANS NAFIKIRI NI MWEZI WA 11 NA ILIKUWA BILLIONI 185 NA TUMEJITAHIDI MPAKA SASA HIVI NI 90 NA HII NDANI YA MIEZI 3 TU, JE TUKITUMIA MBINU ZA KUGUNA NDANI YA MIEZI 6 SI TUTAKUWA TUMESHAMALIZA? TE TE TE
.
Walitingisha kiberiti kuwa uamuzi umetolewa na ICC eti Dowans walipwe 185 bilioni, tukaguna.
Wakagutuka wakadai kuwa haikuwa 185 bilioni bali 95 bilioni, tukaanza kujiuliza kulikoni ?
Wakati hatujakaa sawa wakasema ni lazima tulipe kwani hamna tena ujanja, tukataharuki.
Wakaanza na vitisho na matusi kwa kudai Ikulu haihusiki na sakata la Dowans, tukaguna tena.
Wakitisha kikao cha walaji (CCM) na kubariki malipo kwa matapeli, tukasema wakilipa hapatatosha.
Wakaitisha kikao cha wabunge kuweka mkakati wa pamoja, Mungu si athumani, wakakwama.
Wakaunda kamati ya wanasheria wao wabunge eti kutafuta muafaka, tukaguna kwa sauti kubwa.
Mwanasheria moja, Mkono, fisadi aliyekubuhu ataka tujadiliane na wezi watupunguzie - iwe bil. 50 ?
Tukiguna tena hela hiyo itapungua na kuwa billioni 25!
Tukiendelea tena kuguna itakuwa bilioni 12.5
Tukiendelea tena .........
tukiendelea tena....
Mwisho deni litakwisha ndani ya mwaka mmoja!!!!
!
 
"Hatutalipeleka suala hili bungeni….kulipeleka huko itakuwa ni kwenda kujadili siasa na si sheria. Na kwa hili tayari kuna timu ya wabunge wa CCM ambao ni watalaamu wa sheria pamoja na timu itakayoundwa na serikali, timu hizo zitakaa na kupitia kwa makini suala hili ili twende tukatafute ufafanuzi huo wa kisheria," alisema Pinda.

Kwa nini wabunge wa CCM peke yao kwani hela ni ya CCM?
 
DUH !!!!!!!!! HAPA TUMEKWISHA
Nashindwa kupata jibu nani anazungumza kwa niaba ya nani, kwani wote waliotangulia kila mmoja anatoa kauli tofauti kama vile ndio kwanza jambo hili limifika mezani kwake. Naanza kwa kuzungumzia kauli ya waziri mwenye amana, mh Ngeleja ambaye alisikika akisema Dowans ni lazima ilipwe, kauli yake hii ilipingwa vikali na baadhi ya mawaziri wenye uchungu na kodi za watanzania akiwemo Mh. Sita pamoja na naibu waziri Mh.Mwakyembe ambao naweza kuwaita kwamba ni wawakilishi wa wananchi na sio wawakilishi wa matakwa yao binafsi. Baada ya hapo mawaziri wengine wengi waliwashambulia Sitta na Mwakyembe wakidai kwamba hawakuwa na haki ya kuzungumzia swala la Dowans eti kwa kuwa sio wizara yao.Leo hii tena Mh. Waziri Mkuu ndugu Mizengwe Pindwa naye kaja na jipya eti swala la kuilipa au kutoilipa Dowans halitapelekwa bungeni kwa kuwa ni swala la kisheria. Kinacho nichanganya hapa ni kwamba je huko mahakama kuu ni nani atakayekuwa mshtakiwa na ni nani mlalamikaji? Mahakama kuu walishasema kwamba hakuna kesi yoyote kuhusu Dowans iliyokwisha andikishwa na kwa taratibu za mahakama ni lazima kuwepo pande mbili, mdai na mdaiwa, mdai ni Dowans tunamfahamu je mdaiwa ni yupi wakati serikali ilisha ridhia kulipa deni? mbona hapa ni sawa na kesi ya nyani kuharibu mazao halafu jaji awe ni tumbili, kweli hapa haki itatendeka kweli !!!!!!!!! Hii ni danganya toto, serikali ituweke wazi kwa hili tumechoka kudanganywa kila kukicha. Kwanza hebu tujiulize, je serikali yetu haina madeni mengine kuancha hili la Dowans? na hayo madeni yana muda gani mpaka leo serikali haijalipa? Kwanini deni hili liwe livaliwe njuga na kila kiongozi wa nchi? Hapa panma utata mkubwa sana. Naamini kuna madeni mengi ya nyuma tangu enzi za Mwalimu Nyerere lakini mpaka sasa hivi hatujalipa. Achilia mbali madeni mengine ambayo mpaka sasa sasa hivi wananchi wazawa na walala hoi wa Tanzania waliokuwa wafanyakazi wa Shirikisho la Afrika Mashariki wazee wetu ambao hawana uwezo wa kujikimu kwa njia yoyote ile wanaishia kupigwa virungu na kumwagiwa maji ya kuwasha na jeshi la kuwalinda viongozi waserikali na kuwanyanyasa pamoja na kuwauwa wananchi. Je malimbikizo ya likizo za waalimu sio deni kwa serikali, mbona haya yote hayashikiwi bango na viongozi wa serikali? Inapotokea ni madai ya wananchi walala hoi serikali inasema kwamba hakuna pesa ila kwa hili la Dowans pesa zipo !!!!!!! Sisi wananchi watanzania tunazikataa kauli hizi za viongozi walafi wanaotaka kutubebesha mzigo huu mkubwa kwa masilahi yao wenyewe. Kwa kauli hii ya Mh. Pinda inaonyesha kwamba serikali yetu yote ni ya kisanii. Nilitegea kwamba mtoto wa mkulima ( Pinda ) angekuwa pamoja na wananchi wa Tanzania ktk kupinga hili. Sasa napata jibu kwamba huyu alikuwa mtoto wa mkulima kwa kipindi hicho lakini sio sasa. Sasa hivi ni sawa na tone la mafuta lililomwagwa baharini. Inawezekani kauli hii haikutoka kwa utashi wake mwenyewe bali ni kwa shinikizo la viongozi mapapa wa ufisadi. Ila kama ni kwa matakwa yake basi tunaweza kumuweka kwenye kundi la akina .............. tutaanza kuingiwa na uoga kwamba ni hata yeye pia sio mwenzetu (mlala hoi)
Hebu turudi nyuma kidogo, nakumbuka wakati Mh. Pinda anateuliwa kuwa waziri mkuu alianza kwa kasi ya hali juu kwa kuhoji ulali wa serikali masikini kama ya Tanzania kununua magari ya kifarahi na ya bei ya juu kwa ajili ya wabunge na mawaziri (Land Cruiser VX) kasi hii ilitugusa wengi na kuamini kwamba huyu PM atakaye tufaa. Baada ya uchaguzi tumemsikia tena eti ndugu yetu huyu amelikataa gari lake jipya eti kwa kigezo cha kwamba magari hayo ni ya bei kubwa na kwamba hata gari lake la awali bado linamfaa kutumia. Jamani, hebu nisaidiani hapa kwani nahisi kwamba uelewa wangu ni mdogo. Hapa nafananisha na baba aliyenunua chakuala halafu kimeshapikwa eti anagoma kula kwa kuwa ni cha gharama !!!!!!!!!! hivi hili linakuingia akilini kweli? Yeye kama mtendaji mkuu wa serikali alitakiwa kuzuia manunuzi ya haya magari na sio kukataa la kwake ambalo tayari limeshanunuliwa !!!!!!!!! Watanzania tunapatwa na wasiwasi kwa hili, haya ni mazingaumbu, mtoto wa mkulima Pinda amesha tutosa hivyo tunamuomba Mh. Sita pamaoja na Mwakyembe wasimame imara kuhakikisha kwamba Dowans halipwi kitu. Msiogope kutishiwa na viongozi mafisadi wanaojali maslai binafsi kuliko ya wananchi wao. Msifungwe midomo katika kuwatetea wananchi ambao ndio wamewapeleka bungeni kuwawakilisha, tunaamini kwamba kwamba mlicho kizungumza hamkuzungumza kama mawaziri au wana CCM bali mmezungumza kama wawakilishi wa wananchi wa Tanzania walio wapa kura zao. Sisi tutakuwa nyumba yenu, hata kama ni kwa maandamano ya nchi nzima kuhakikisha kwamba kodi na jasho la watanzania halipotelei mikononi wa hawa Dowans. Na hata kama ni lazima tuko tayari kuandamana tukiwa uchi wa mnyama kama vile walivyo ahidi baadhi ya wasanii katika kipindi cha jana Jumanne katika kindindi cha "Wanawake Live" cha chanel 5.
Jamani watanzania amkeni kutetea kodi zetu zisitumike vibaya.
 
Kwanini kuwe na kamati ya wanasheria wa CCM na serikali tu? Kwani ilo suala ni la chama?

Mahala pazuri kwa suala ilo kujadiliwa na kutolewa maamuzi na bungeni. Ambapo mawazo ya waTZ wote yatawakilishwa.

Hiyo timu ya CCM haitawakilisha interests za waTZ wote.

Suala la umeme; kama TANESCO imezidiwa na mahitaji,basi serikali iruhusu watu na mashirika binafsi yaingie rasmi katika uzalishaji na usambazaji wa umeme,bila kuwepo conditions kama vile TANESCO kua main supplier na mahala ambapo inataka watu na mashirika hayo yawekeze. Serikali has to liberalise the energy sector as it did with the telecommunication sector. Si tunakumbuka namna TTCL walivyokua na nyodo na maringo,angalia sasa wanaheshima na adabu haooo!!

I stand to be corrected.
 
Very interesting kumbe haman kitu, hatuna viongozi tunaishi kwa kudra za Mwenyezi-mungu.

Pinda ole wako
 
Back
Top Bottom