Pinda: Dowans hatuirudishi bungeni

Pinda: Dowans hatuirudishi bungeni

Wabunge walikomalie lijadiliwe tena. Pinda mwenyewe awambie wabunge ni sababu zipi zilizoifanya serikali ikapuuzia maazimio/mapendekezo karibu yote ya kamati ya bunge.
 
Spika wa Bunge Anna Makinda amesema hoja ya Kafulila kuhusu Dowans iko mahakamani kwa hiyo haitaingia bungeni. (Mlimani TV)

Tusubiri ya Mnyika nayo kupigwa chini.

Ni hilo tu, Asanteni.
 
Spika wa Bunge Anna Makinda amesema hoja ya Kafulila kuhusu Dowans iko mahakamani kwa hiyo haitaingia bungeni. (Mlimani TV)

Tusubiri ya Mnyika nayo kupigwa chini.

Ni hilo tu, Asanteni.
Asante mama, lazima uheshimu walokupa cheo!!!
 
Spika wa Bunge Anna Makinda amesema hoja ya Kafulila kuhusu Dowans iko mahakamani kwa hiyo haitaingia bungeni. (Mlimani TV)

Tusubiri ya Mnyika nayo kupigwa chini.

Ni hilo tu, Asanteni.

na ndio walichokuwa wanakitaka hiki ccm lakini al in all tumejiumiza na tunaumia wenyewe kwa kuwapa ccm viti vingi bungeni so hapa suala ni kikulacho.............:car:
 
I'm sorry to say it lakini me Pinda huwa namfananisha na mbwa mzee asiye na meno atabweka tu hawezi kuuma! (Nadhani cjamtusi)
 
Pinda sura ya kondoo kumbe damu ya Chui.. Dah hawa jamaa noma kama wameshamchakachua Mtoto wa Mkulima sasa nae anajiona mtoto wa kishua.

Ila nasikia jamaa wameingia nae mkataba wa kumwakikishia kuwa atakaa mbele ya jengo jeupe pale na sio tena kwa nyuma alipo sasa mwaka 2015. So lazma akubaliane na Waendesha nchi.
 
yaani natamani huyu pinda nimpige na manati
 
Huyu Pinda anabore tu. kwanza alisema atamtuma CAG aende UDOM je ameshamtuma?
 
Hapo kwenye Mgao wa UMEME ndo kaongea nini sasa???? Tatizo bado lipo, hajatoa solution......Sijui koz yeye ni mtoto wa Mkulima then haoni umuhimu wa Umeme??????? Aache sound atoe solutions.......
 
Pinda kweli kapinda!!! Bunge ndo chombo cha kufanya miswada kuwa sheria, leo anasema jambo hilo likipelekwa bungeni litajadiliwa kisiasa??? Huyu mzee duara kweli!!!
 
Pinda nae anaongea kama mwanaume! Asubiri kulia bungeni.
 
Pinda alishaingizwa kundini ila kimsingi hakuwa ametoa makucha, nadhani imebidi kutoa makucha kwa wakati huu akiwa kama msemaji mkuu wa serikali haswa linapokuja swala kama hili ambalo inaonekana bunge na haswa baadhi ya wabunge kutaka kutumika kama wakombozi wa wananchi kutoka kwenye makucha ya serikali yenye uchu na vijisenti vichache vya watanzania wengi walio masikini. Tukumbuke kwamba Pinda akiongea ndio msimamo halisi wa serikali hii dhaifu na yenye woga mwingi ya mkwere, mawaziri wengi wa mkwere wamepishana lakini sitarajii Pinda kupishana na mkwere vinginevyo hiyo haitakuwa serikali ingawa serikali yenyewe imejaa udhaifu unaoifanya iwe na woga mwingi.

Shughuli itakuja pale atakapolia tena mambo yakiwa magumu maana huku tuendako itabidi akaze kucha zake kweli, kimsingi ngozi za watanzania zimeanza kuwa ngumu na hawachuniki kirahisi sana sasa hivi. Hata kama akisema kulia ni unafiki lakini hautasaidia tena na sasa nahisi akilia wadanganyika hawatasikitika tena ila kwa sasa watazomea, kama yeye ni jasiri basi mambo yakiuma alie halafu tuone itakuwaje..!
 
"Kaona mamba jamani..... Ndio tamko la waliomweka, tanzania tuna bora viongozi na sio viongozi bora..." .....TUNISIA hyoooooooo au bado usingizi mtam, tutashtuka nchi ishakuua jangwa washasepa na hvi wakubwa wana uraia wa nchi 2.....
 
PINDA: “Hatutalipeleka suala hili bungeni….kulipeleka huko itakuwa ni kwenda kujadili siasa na si sheria. Na kwa hili tayari kuna timu ya wabunge wa CCM ambao ni watalaamu wa sheria pamoja na timu itakayoundwa na serikali, timu hizo zitakaa na kupitia kwa makini suala hili ili twende tukatafute ufafanuzi huo wa kisheria,” alisema Pinda.

Source: Tanzania Daima

Mwanasheria wa Serikali anasubiri nini kuachia ngazi?? - maana alishasema kwamba kaipitia hukumu yote, hakuna cha kujadiri na mjadala ameufunga rasmi
 
hivi hawa jamaa wapo kutuwakilisha au kutuamulia? wananchi kama waajiri wao inakuwaje tunakataa jambo halafu wao kwa kiburi bila hata kuonesha ushawishi wa kwa nini ni lazima kulipa na hiyo pesa inatoka wapi wao wanalazimisha tu tuwalipe mafisadi wenzao? kwa nini wasijiuuzulu?
 
hivi hawa jamaa wapo kutuwakilisha au kutuamulia? wananchi kama waajiri wao inakuwaje tunakataa jambo halafu wao kwa kiburi bila hata kuonesha ushawishi wa kwa nini ni lazima kulipa na hiyo pesa inatoka wapi wao wanalazimisha tu tuwalipe mafisadi wenzao? kwa nini wasijiuuzulu?

Mwalimu Mkuu, hizi hasira zinahitajika kwa vitendo kama Tunisia vile. Sihamasishi watawaliwa kuandamana, nahamasisha wadanganyika kujifunza kuweka taratibu muafaka na kuchukua hatua katika kuhakikisha wanajinasua kutoka kwenye makucha ya watawala. Tukumbuke tu kwamba kama tukijitoa kwa nguvu tutaacha baadhi ya nyama zetu kwenye makucha yao. Lazima tuwe wajanja tuhakikishe tunajitoa bila kuacha mabaki yetu, hata hivyo inapobidi basi tutumie akili maana inawezekana.

Nashangaa Serikali inapolalamika kwamba kauli za wapinzani zitafanya Tanzania isitawalike, hii inaonyesha waziwazi uchu wao wa kutaka kuendelea kutufanya sisi watumwa wao. Hatupaswi kutawaliwa, tunahitaji kuongozwa na viongozi wenye busara za kutosha kutupeleka kunakofaa.
 
Back
Top Bottom