PINDA aingia rasmi mbio za urais CCM?

PINDA aingia rasmi mbio za urais CCM?

Mnajisumbua kutaka kujua nani atasimamishwa kiti cha urais hamlali hamli hamnywi khuu poleni sana pinda anatamani muda uishe haraka aondokane na kadhia hizi na alishatamka kamwe inatosha. Endeleeni kuchokonoa mnaweza kumjua muanze kujipima joto si mbaya
 
Kama u PM tu analia bungeni na kukurupuka kwenye maamuzi yanayoikiuka katiba aliyoapa atailinda, je akiwa rais itakuwa je? Ajifikirie mara mbilimbili kwani urais si kamasi kila mtu anazo

pinda anafikiri uraisi ni umonitor maana kwa maandamano haya ya chadema atakuwa anapandisha bp tu
 
Pinda hata ukuu wa wilaya hataweza sembuse uraisi?CCM wakimsimamisha chadema tutaanza kupanga baraza la mawaziri na safu nzima ya uongozi wala hakuna haja ya kampeni!

tena chadema ianze kuanzia sasa kupanga safu yake ya uwaziri maana kwa spidi ihi ya ulafi wa uraisi ndani ya chama cha mapinduzi, wanajimaliza wenyewe, :A S thumbs_up: chadema go go go magogoni 2015,
 
Hatutaki Pinda na UPinda kwenye nchi yetu
 
Mzee wa Rula asante sana kwa comments zako lakini kuna mambo unaweza kufafanua ama kujifunza.

Kwa mfano,Inawezekana kabisa Magufuri akawa mmoja wa machaguo ya Kikwete, lakini ni vipi Magufuri atapitishwa na CCM akawa mgombea urais wakati hana nguvu ndani ya CCM ya sasa?
Hivi unajua hata Nyerere Chaguo lake la kwanza lilikuwa Dr.Salim Ahamed Salim na sio Ally Hassan Mwinyi lakini bado Nyerere alishindwa kumpitisha Salim!!

Hata Mkapa mwaka 2005 chaguo lake la kwanza lilikuwa Dr.Abdallah Kigoda na chaguo la pili lilikuwa Sumaye, lakini bado hakufanikiwa.
Sijui kama unakumbuka kisa cha Dr.Salimin Amour 2000 kutaka waziri kiongozi wake Dr.Bilal kuwa mrithi wake Zanzibar na bado lilishindikana.

Kitu ninachokijua ni kuwa siku zote rais anayeondoka madarakani anakuwa na chaguo lake 'rasmi' (Mara nyingi chaguo zaidi ya moja) hivyo hata Kikwete ana chaguo zaidi ya moja, Membe akiwa ni mmoja wao.

Kwani mpaka sasa tena katika hali mbaya ya kisiasa ndani ya CCM kuna haja au uwezekano wa suala la mgombea wa CCM 2015 kubaki kama 'Top Secret' kwa rais Kikwete na watu wake wachache?

Kwa vyovyote ilivyo kwa CCM mgombea wa urais 2015 ni lazima atakuwa amejiandaa vya kutosha kufanikishwa hilo na sio kwa kubebwa tu na kwa sasa Lowassa yuko mbele sana na njia pekee labda ya kumshinda Lowassa ni makundi makuu yote kuungana dhidi yake na kutumia mfumo wa sasa wa serikali kufanikisha hilo na hapo ndipo Pinda amesimamia kwa sasa.

Keep my words, soon utakuja kuniambia.
TanganyikaTANU umezungumza kitu cha ukweli na wala sina pingamizi kwani ndiyo hali halisi, JK anamtaka Magufuli kwa sababu anauzika kirahisi kwa wananchi lakini si JK mwenyewe wala Magufuli mwenye mtandao wa kutosha kuweza kufanya jina lake likapita NEC bila shida au mizengwe mingi.

Chaguo la pili la JK kama ulivyosema ni Membe lakini ane anakabiliwa na tatizo kama la Magufuli hana mtandao mkubwa sana wa kumbeba. Pia naye hauziki sana sokoni maana ana haiba kama ya JK jambo ambalo wananchi wanaweza kumhukumu kwa kumnyima uraisi kutokana na hasira walizonazo kwa rais wa sasa.

Ikiwa ndiyo hivyo hali itakuwaje??

Kuna hatari Nchimbi ambye ndiye chaguo la mamvi yaani Lowasa kuchukua nchi kama afya ya Lowasa haitarusu kuhimili mikimiki ya kampeni na mengineyo. Swali je Lowasa anauzika kwa wananchi???

Hii itategemea sana na CDM nao watatoa mgombea yupi kwa kiti hicho. 2015 CCM ikivuka basi haiwepata mtihani mwingine tena mgumu kuliko iliyonao saizi wa makundi na kashfa kubwa kubwa kila kukicha.
 
Waziri mkuu Mizengo Pinda kwa sasa amezidi kujipambanua na kudhihirisha kuwa hakuna wa kumzuia katika mbio za Urais kutokana na utendaji wake,utulivu wake katika kufanya maamuzi,uzalendo na uadilifu
Twendeni na mtoto wa mkulima kwa Uadilifu na maendeleo ya taifa
 
Waziri mkuu Mizengo Pinda kwa sasa amezidi kujipambanua na kudhihirisha kuwa hakuna wa kumzuia katika mbio za Urais kutokana na utendaji wake,utulivu wake katika kufanya maamuzi,uzalendo na uadilifu
Twendeni na mtoto wa mkulima kwa Uadilifu na maendeleo ya taifa

Utakuwa unaumwa wewe. Twende naye wapi sisi, hana maamuzi yoyote, tutaliangamiza Taifa
 
Sura ni kigezo cha kupitisha mgombea mwaka huu..kwa hiyo Pinda ajipime
 
Japokuwa ni wazi kuwa mgombea urais wa CCM 2015 huenda akawa ni Edward Lowassa kutokana na nguvu za kisiasa alizonazo ndani ya CCM kwa sasa, kitisho kipya kimeingia kwa kasi dhidi ya kambi hiyo baada ya mikakati ya Mizengo Pinda kutaka kugombea urais 2015 kuanza kuwekwa hadharani na baadhi ya watu hususani mawaziri wa serikali ya Kikwete.

Jambo hili limekuja baada ya Pinda kuwa na ziara za mara kwa mara za kichama mikoa mbalimbali na kufanya vikao vya ndani vya CCM na kiserikali visivyo na Agenda za wazi na huku pia akiendesha harambee kadhaa kwenye taasisi mbalimbali za kijamii na kikanisa kama vile ambavyo wanasiasa wengine wa CCM wanaowania urais wamekuwa wakifanya kila mara.

Na taarifa za karibuni kabisa zinasema kambi ya Pinda inayoongozwa na mawaziri kadhaa imepanga kuzivuta kambi ya Membe na Sitta ili kuungana na Pinda ili kupambana na Lowassa.

Mkakati huu unapangwa chini ya agenda ya kuhakikisha rais ajaye ni lazima atoke kwenye baraza la mawaziri la sasa kwa lengo la kulinda mfumo na maslahi ya Kikwete mara atakapo achia madaraka ya urais.
Huu ni utamaduni umekuwepo kuanzia kwa Nyerere, Mwinyi na Mkapa, na unasisitizwa kuendelezwa pia kwa Kikwete.

Kuna tetesi pia, hata kelele za kutaka Pinda ashtakiwe mahakamani kwa kauli yake ya ''Watapigwa tu, tena nasema wapigwe'' huenda pia zikazidi kuchochewa chini kwa chini na wafuasi wa kambi ya Lowassa ili kuvunja nguvu za kisiasa za Pinda kuelekea 2015.
Mpaka sasa limeanza kupelekea na litazidi kupelekea 'Wateule' wa Pinda wazidi kujitokeza hadharani kuanza kumtetea kwa hali na mali ili asishtakiwe mahakamani.

Swali, Pinda ameingia rasmi kwenye kinyang'anyiro cha urais CCM 2015?

Team EL do something....!
 
Mi huwa nashangaa sana pale ambapo watu tunakuwa tunamuona Pinda kama hawez urais ilihali katuongoza kwenye uwaziri mkuu miaka saba sasa. Hii nchi inahitaji rais ambaye anaijua vizuri Local government. Chachu kubwa ya maendeleo iko Local governments. Mngejua ni mangapi mazuri amefanya msingethubutu kusema madhaifu yake machache. Kikwete sio mjinga kumuacha mtu huyu mpaka leo. Tuache siasa chafu tubaki kwenye ukweli. hakuna asiyekosea lakin tusihukumiane kwa makosa madogi kabla hatujahukumiwa. waacheni watanzania waamue na sio kuwapa Propaganda chafu. najua wengi humu mpo kwa maslah ya watu wenu lakin lazima kuna muda tuangalie maslahi ya nchi. Amekuwa Waziri mkuu bila tatizo, leo mmeskia Urais ndio mnaanza maneno.
 
Mchqngueni tu bahati nzuri sitakuwepo nchini baada ya kupata limama mamtoni.
 
Sasa ukiranja mkuu analialia...huo ualimu mkuu si ndo atajinyea.???
 
Back
Top Bottom