Pinda afunguka sakata la Escrow

Pinda anasema watanzania watapewa taarifa sahihi kuhusu escrow muda ukifika! Anasubiri nini kutoa tarifa hiyo? bwawa limeelemewa na maji yanataka kuvunja bwawa eti anasubiri muda. Au ndo kusubiri uchakachuaji wa taarifa ya CAG?

Hata mimi hapo kanishangaza ............................ huo muda utafika lini?? Kama kweli anaona uvumi ukiendelea mwisho utakuwa ukweli kwa nini serikali bado inaendela kukaa kimya. Na kwa nini akasemee makanisani!!? Off course Taifa letu limekuwa la uvumi kwa kuwa serikali huwa inanyamaza mambo kama haya yakitokea. Sasa ameona pressure imezidi anataka kuleta longolongo.....................!!
 
Pm ananiudhi kutumia kanisa kama jukwaa la kisiasa.
shame on you!
 
Mwiziiiiiiiii mkubwaaaaaaaaa....jizi kweliiiiiiii.....!!!!


Kila mtu anajua huyu mwizi alivyokuwa siku hizi....muongo mkubwa....!!!
 

Nothing new!?
 
spencer, Kimbunga, ocampo four na wengine wote,
Hii inaitwa jaza jaza thread na yeye aonekane ameandika uzi uliochangiwa na watu wengi.
Mmejitahidi kumjazia komenti lakini si mbaya
 
Last edited by a moderator:
Wkati upi ukifika? Labda anamaanisha wakikamilisha uchakachuaji ndio muda utakuwa umefika
 
Mwizi mkubwa huyo.

Mbona umeongea kiushabiki mkuu,ebu jaribu kujenga hoja ni kwa namna gani PINDA amehusika na uwizi huo?Kwani tunakumbuka wakati wa ufisadi wa Richmond uliofanywa na Edward Lowassa ripoti ya kamati ya Mwakyembe ilizungumza kwa kina namna ambavyo Edward Lowassa alivyokuwa anashinikiza watendaji wa serikali walio chini yake kufanikisha mchakato wa Richmond na Kuiba pesa za umma mpaka ikapelekea jamaa kujiuzulu kwa lazima
 
Tunakuaminia Waziri mkuu wetu wakati ukifika wekeni wazi ukweli wa yote kuhusu sakata la ESCROW tunajua siasa imeingia kwenye suala hilo Edward Lowassa na team yake wanatumia nafasi hiyo kuihujumu na hatimaye kuiangusha serikali ya J Kikwete njama zao hizo zinajulikana na muda si mrefu wataumbuka.
 
Wkati upi ukifika? Labda anamaanisha wakikamilisha uchakachuaji ndio muda utakuwa umefika

Nani achakachue wakati kila kitu kipo wazi tusubiri ripoti isomwe mkuu acha kuwa na mawazo hasi kwa kila kitu akili ya kuambiwa changanya na za kwako!
 
Pinda muda wa kuumbuliwa unakaribia,unajifanya mtoto wa mkulima kumbe ni walewale wachumia tumbo


Unanichekesha mkuu. Hivi nani kakuambia kuna kiongozi msafi ndani ya CCM? Kile chama kimejawa na wasanii na wanaotaka kuja madarakani nao pia mawazo yao ni kuja kuiba na kulipiza visasi kwa wenzao huku wakisahau maendeleo ya nchi na mahitaji ya wananchi wao.
 
Kakimbilia chachi? Kweli simba akizidiwa hunywa hata supu ya kabeji.
 
''umeongezwa chumvi na wakati ukifika Watanzania watatolewa taarifa kamili''
Mheshimiwa Pinda anafanya kosa kubwa sana hapa......
 
Mwiziiiiiiiii mkubwaaaaaaaaa....jizi kweliiiiiiii.....!!!!


Kila mtu anajua huyu mwizi alivyokuwa siku hizi....muongo mkubwa....!!!

Ebu tujadiri hii hoja kisomi tuache ushabiki wa kisiasa,naoma utuambie ni kwa namna gani Mizengo Pinda anahusika na uwizi huo?manake tukikumbuka kwenye sakata la Richmond ripoti ya Mwakyembe ilidadavua vizuri kwa ushahidi uliojitosheleza namna Bw. Edward Lowassa alivyohusika kukwapua fedha za umma bila huruma zaidi shilingi mil.152 kwa siku iwe umeme umezalishwa au haujazalishwa kwenda kwenye gridi ya Taifa.Ebu piga mahesabu kwa mwaka ingekuwaje na je ingekuwa miaka mitano ingekuwaje pia? Edward Lowassa na mafisadi wenzake wangeweza kukwapua kiasi gani cha fedha kama mkataba usingesitishwa baada ya ripoti ya Mwakyembe kuibua uwizi huo.Hiyo ni moja ya mikataba mibovu ya kinyonyaji aliotuingiza Edward Lowassa muda mfupi baada ya kuteuliwa kuwa waziri mkuu.Huyo ndiyo Edward Lowassa kamwe huwezi kumfananisha na Mizengo Pinda katika uaminifu wao,uadilifu wao na weledi wao katika utekelezaji wa majukumu ya serikali.
 
Makanisa sasa yanatia kinyaa kusafisha Majizi... hapo ndo amefunguka? Ukanjanja katika uandishi sasa yanafikia kilele cha ujinga...
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…