Leo nimeamka asubuhi nikaona nitoe kitu geto kama
Mwachiluwi
Nilienda dukani kununua mahitaji na mengine yalikuwepo ndani
Nikachemsha nyama wakati inaiva nikaandaa viungo kama vinavyoonekana hapo chini
View attachment 3317600View attachment 3317601
Nyama haikua nzuri sana sababu sio fresh ila pilau lazima linoge,
Msela geto la jirani aliandaa breakfast ya ugali na mayai tukagonga wakati naanza kupika, ilikua saa tano asubuhi
View attachment 3317602
Nikaanza kupika kwa kukaanga viungo kwenye mafuta hadi kuiva, baada ya kuiva nilitwanga viungo vya pilau kwenye glass kwa kutwanga na mwiko(geto hamna kinu)(Saumu, pilau masala na tangawizi) kisha nikaviongeza kwenye mchanganyiko
View attachment 3317603
Kitu kikabadilika rangi kuwa brown nikaongeza njegere hicho kifuko kinauzwa buku tu, kisha nikaongeza supu na maji kipimo cha mchele kilo moja
View attachment 3317613
Nyama na viazi nilikaanga pembeni nikaweka baada ya maji kuchemka ili viazi visitengeze uzito kwenye maji ya mchele, baada ya kuviweka kwa maji nikaweka na mchele kitu kikafunikwa vizuri
View attachment 3317614
View attachment 3317619
Ndani ya dk ishirini geto pakaanza kunukia nikafungua madirisha na mlango kumuumiza roho demu mpangaji mwenzangu aliyenikataa kisa nakunywa pombe
View attachment 3317621View attachment 3317623
Wakati naandaa viungo nilikata pia viungo vya salad nikatia kwa fridge vipate baridi hapa nimetoa naongeza limao pilipili manga na mayonise, leo tunakula pilau na french salad
View attachment 3317628
Chini kuna ice cubes, smirnof ice, glass zina passion, sprite, limao na juice ya rosela kwa ajili cocktail ya kushushia pilau letu la kibunge,
Glass zipo tatu nilimpigia simu mwana aje kula pamoja na msela tuliyekula nae ugali asubuhi alikua mpiga picha wangu hivyo tupo watatu
View attachment 3317639
Niambie umependa part gani kwenye comments uje kula pilau
View attachment 3317642