Ivonya-Ngia
JF-Expert Member
- Jul 16, 2009
- 703
- 385
Tangu sasa hadi 2015 tutasikia na kuona mengi, msimu wa viroja hasa.
Mushrooming ya vijarida, magazeti, blogs, programme elekezi za Tv na radio, kuibuka vyama vya msimu, kuibuka wanasiasa wa msimu, kuibuka wale wajiitao "wachambuzi mahiri" wa msimu na waishio bila itikadi kuama vyama. Ni msimu wa wale wanasiasa wajionao "wateule" kupamba kurasa za mbele za magazeti na habari za Tv/Radio kwa kununua fursa. Ni msimu hasa wa wale wajanja wa mjini wanaojifanya mabingwa wa mikakati kutengeneza pesa kwa "kuwashika wateule".
Kwa sisi wafuatiliaji wa siasa za ushindani Tanzania tangu mwaka ule wa 1995 hatushangazwi na haya. Ni msimu tu kama ile ya hali ya hewa kwa mwaka...vuli, masika na hata kiangazi. Tofauti ni kuwa msimu huu wa harakati nyingi za kutwaa madaraka huwaacha wengine na enzi huku wengine wakiingia jehanamu.
Kila la heri washiriki wote, kipyenga ndo kimepulizwa hicho!!!
Mushrooming ya vijarida, magazeti, blogs, programme elekezi za Tv na radio, kuibuka vyama vya msimu, kuibuka wanasiasa wa msimu, kuibuka wale wajiitao "wachambuzi mahiri" wa msimu na waishio bila itikadi kuama vyama. Ni msimu wa wale wanasiasa wajionao "wateule" kupamba kurasa za mbele za magazeti na habari za Tv/Radio kwa kununua fursa. Ni msimu hasa wa wale wajanja wa mjini wanaojifanya mabingwa wa mikakati kutengeneza pesa kwa "kuwashika wateule".
Kwa sisi wafuatiliaji wa siasa za ushindani Tanzania tangu mwaka ule wa 1995 hatushangazwi na haya. Ni msimu tu kama ile ya hali ya hewa kwa mwaka...vuli, masika na hata kiangazi. Tofauti ni kuwa msimu huu wa harakati nyingi za kutwaa madaraka huwaacha wengine na enzi huku wengine wakiingia jehanamu.
Kila la heri washiriki wote, kipyenga ndo kimepulizwa hicho!!!