nngu007
JF-Expert Member
- Aug 2, 2010
- 15,862
- 5,797
|
Kambarage Wasira(Kulia) |
Bulaya alisema mtoto huyo aliyejulikana kwa jina la Kambarage, alikumbana na mkasa huo juzi kwenye Kata ya Kunzugu eneo la Bukore.
Alisema Kambarage akiwa na baadhi ya makada wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) na viongozi wengine, wakiwamo watumishi wa Serikali, walifungiwa ndani ya nyumba na wananchi na kutaka kuwachoma moto baada ya kugundua kwamba walitaka kuwapa baadhi ya vijana rushwa ili wafanye fojo kwenye mkutano wake.
Bulaya alisema wananchi wa Bukore baada ya kuwafungia watu hao ndani ya nyumba, kabla ya kuchukua uamuzi wa kuwachoma moto, baadhi yao walimpigia simu ndipo alipochukua askari na kwenda eneo hilo.
Kengete Blog