Picha: Ziara ya Kinana Geita

Picha: Ziara ya Kinana Geita

huku shinyanga halmashauri ya manispaa imeamua kuwa gari ndogo hiace zipaki eneo la stendi ya zamani lakini cha kushangaa eti viongozi uchwara wa ccm eti mmoja anaitwa shigino na mwingine anaitwa mseti na tumbo lake kuuuuuuubwa wamesimama na kuwatukana traffic wasihamishe magari eti wao ni chama tawala na eti wanaisimamia serikali kuisimamia gani huko mnaingilia maamuzi ya baraza la madiwani tena wengi wao wakiwa haohao wa ccm!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!iWANATAKA KULETA FUJO MJINI
 
naambiwa watu walikuwa kiduchu wengi walikuja kwa mabasi ya mwenyekiti wa mkoa aitwae msukuma na watumishi ndio maana anaona style ya picha zilivyopigwa ....watu walifuata ngoma namziki tu hapakuwa na jipya ni ahadi tu .....yaani hata mkutano wa diwani sio hivyo

Duh! inaonyesha amedoda. Kwanini sasa watu wanasusa au taharabu hakunaga!
 
Katibu wa Chama anatoa leseni ya uchimbaji...!!!???? Only in Tanzania

Huu umbumbumbu sijui tutauacha lini, huyu ilitakiwa ashushwe jukwaani na kutandikwa hadharani!! mambo ya kipumbavu kabisa
 
Jamani soma vizuri kilichoandikwa. Leseni hazikutolewa na Kinana, leseni zimetolewa na serikali Kinana alichofanya ni kuzikabidhi kwa wenye nazo tu.

Tiba

Agawe yeye kama nani kwenye hili la leseni? Ni structure ipi hiyo inayosema kawamba kazi ya wizara ni kutoa leseni na kuzigawa kwa wamiliki ni kazi ya katibu wa CCM. So alipewa za wanaccm peke yao na wanachama wa vyama vingine vingine waligawiwa na makatibu wakuu wao? Hivi kinana alisoma Havard ipi ni ya kata nini maana ingekuwa Havard ya ukweli asingekuwa anafanya upuuzi kama huu ambao uko so obvious.
 
miaka 35 bado mnafungua matawi, je cck wafanye nini? nyie kwisha habari yenu. mia

i was asking myself the same Q naona wanaomba urafiki kama watoto wa zamani kuwatembea machinga hawana jipya hawa watu wanawachora tu hata mimi wakija kwangu unafikiri sitawachekea nitawachekea sana lakini najua lililopo moyoni mwangu sasa kama mtu kakuvamia kama huyo machinga unategemea kuanza kumrushia ngumi
 
Agawe yeye kama nani kwenye hili la leseni? Ni structure ipi hiyo inayosema kawamba kazi ya wizara ni kutoa leseni na kuzigawa kwa wamiliki ni kazi ya katibu wa CCM. So alipewa za wanaccm peke yao na wanachama wa vyama vingine vingine waligawiwa na makatibu wakuu wao? Hivi kinana alisoma Havard ipi ni ya kata nini maana ingekuwa Havard ya ukweli asingekuwa anafanya upuuzi kama huu ambao uko so obvious.

Bahati mbaya siko kwenye nafasi ya kujibu maswali yako. Mimi nilijaribu tu kufafanua maelezo yaliyo andikwa kwenye hizo picha. Tusubiri wenye majibu na maswali yako waje.

Cheers,

Tiba
 
Ulikuwepo huoni Mh anacheza na kutuza ; vaa miwani usitusumbue bure

Lkn ulitakiwa kujibu hilo swali la msingi ' msaada tutani.....kiongozi wa chama kukabidhi leseni?'
 
msaada tutani.....kiongozi wa chama kukabidhi leseni? or is it me???

Mambo kama hayo utayaona Tanzania tu mkuu! Nchi yetu ni ya maajabu mengi na hili ni moja wapo, labda ikiwezekana na lenyewe liwekwe kwenye ule mchakato wa kupigia kura maajabu saba pamoja na kilimanjaro, serengeti n.k.!
 
Mkuu asigwa, nakuunga mkono. Kwa mtindo huu, Waziri wa Nishati na Madini, Katibu Mkuu au Kamishna wa Madini hawana kazi tena !!! Maombi ya leseni yalifanyika wapi ?

Hapa ndipo utajua hii nchi inaongozwa kama ataasisi fulani.....kwani hakuna mipaka ya kiutendaji kati ya chama na watendaji wa serikali??
 
Kwani Katibu mkuu wa CCM ana mamlaka yapi kisheria ya kutoa leseni za uchimbaji madini? Ni sheria ipi imempa mamlaka hiyo? Na kwanini wawagaiwie sasa? Kweli nchi hii bado ina wadanganyika wengi sana.

Hii ni kinyume kabisa cha sheria! Wanaosimamia vyama vya siasa wako wapi?? Huu ni ubovu usiolezeka na ukiukwaji wa makusudi wa sheria za nchi. Hii ni hatari!!
 
Kuna tofauti kubwa sana kati ya "kukabidhi leseni" na "kutoa leseni" anayekukabidhi leseni si lazima awe na mamlaka ya kutoa leseni kwa maana nyingine kisheria anayetoa leseni ni lazima atambulike kisheria lakini sheria iko kimya kama ni lazima mamlaka inayotoa leseni iwe ndiyo mamlaka pekee ya kukabidhi leseni. Hapa ni lazima turekebishe sheria au tutunge sheria ya kuzuia wanasiasa kukabidhi leseni zinazotolewa na mamlaka za serikali zinazotambulika kisheria

Inawezekana inakereketa lakini kiukweli hili suala ulalamishi wake usipopewa maana na sheria ni kazi bure. Ndiyo maana tulitaka Zombe aadhibiwe lakini sheria ikahoji "yuko wapi Koplo Saad?"
 
Back
Top Bottom