DR. MWAKABANJE
JF-Expert Member
- Nov 7, 2012
- 1,986
- 3,150
Songea ipi unayoishi mkuu ya kuitetea CCM hivyo?? Hii yenye huduma mbovu kila mahali?? Barabara na vituo vya abirua katikati ya mji uchafu mtupu vinajaa maji, huduma za afya hovyo, usafiri ndo usiseme, kamji giza hata kuweka taa za solar hakuna lakini kura zote CCM. Ukweli ni kwamba Ruvuma hakuna wa kuisemea bungeni!Mtoa mada unanifanya niamini kuwa hukutoa mada hii kwa lengo jema bali una hasira zako tu na huyo unayedai kuwa Rais wa Chato. Uwanja huu ni kweli wa siku nyingi na tayari serikali imeuingiza kwenye mpango wa ukarabati mkubwa na soon tunategemea utafanyiwa ukarabati huo. Mbali na mpango huo mkubwa, ukarabati mdogomdogo wa mara kwa mara umekuwa ukifanyika kuhakikisha ndege zinatua bila matatizo. Ninavyokueleza haya niko Songea na nina uhakika na ninayoyasema. Acheni uchochezi usio na miguu wala kichwa!! Yote kwa yote Dkt John Pombe Magufuli ndiye Rais wetu na tunamkubali kwa kazi nzuri ya kuyaminya majizi na mafisadi na kututetea wanyonge. Pigeni kelele sisi hapa kazi tu!!