kandidus
Member
- Feb 6, 2012
- 70
- 17
Watanzania wenzangu,
Kimsingi fikirini kwanza kabla hamjatoa mada katika jamii forum ili tuzijadili. Jeshi la Polisi Tanzania kupitia kikosi cha Usalama Barabarani linapaswa kupongezwa kabisa. Mtoa mada uliyepiga picha hii, ebu tafuta takwimu za ajali kwa miaka miwili tu ilyopita, utakuja kukiri kuwa kwa miaka miwili iliyopita katika barabara ya dsm-morogoro - iringa kulikuwa na ajali nyingi zilizosababisha vifo vya watanzania wengi, na wengine kubaki kuwa tegemezi baada ya kukatwa viungo vyao vya mwili. Hii ni kwa sababu magari hayo uliyoyapiga picha hayakuwa yanafanya kazi barabarani kuthibiti wavunja sheria za barabara hususani mwendo kasi ambao siku zote umekuwa chanzo cha ajali zilizowaua watanzania ambao ndo nguvu kazi ya taifa letu.
Kutokana na sababu hiyo basi, Kwa mwaka huu 2012 kamanda Mpinga amekuja kivingine kwa kushirikiana na wakuu wa vikosi vya Usalama Barabarani wameweka mikakati ya kuongeza vithibiti mwendo na magari ya high-way patrol ili kuhakikisha wanafikia malengo ya kuthibiti ajali za barabara kuu kama sio kuzuia kabisa. Kutokana na ukweli huu basi, kwa madereva na wananchi wasiotii na kujua athari za ajali mf. aliyetoa mada hii, hawatambua hata kidogo utendaji wa trafic wakiwa barabarani. Kwa ujumla picha hii haina uhusiano hata kidogo na mazingira ya rushwa. Kwani gari la polisi katika picha hii hapo juu linaonekana limepaki barabarani inawezekana ikawa kwa sababu mbalimbali: 1. wameharibikiwa 2.kunataarifa wanaisubiri, 3. wanangoja msafara maana ndo kazi zao hizo, 4. wanawangoja askari wenzao ambao wamekwenda kuarest kwani hawawezi kwenda mpaka eneo la kuarest wakiwa na gari kwani mtuhumiwa angeweza kukimbia, 5. wapo katika taratibu zao za kazi n.k
Ushauri kwa mtoa mada:
Askari polisi wanafanya kazi katika mazingira magumu sana, na hivi wanapaswa kupongezwa kwa kazi wazifanyazo. Amani inayoonekana nchini kwetu ni kwa sababu ya utendaji wao kwa kushirikiana na vyombo vingine vya dola. Askari hao utambue ni binaadamu kama wewe. Ili kuwarahisishia utendaji wao yatupasa sisi wananchi hasa madereva tutambue kwanza wajibu wetu tukiwa tunatumia vyombo vyetu vya usafiri katika barabara wanayoitumia watu wengi. Tukiwa na desturi ya kutii sheria tutawaepuka hao askari ambao kwa kupaki gari zao tu, wewe umewaona kana kwamba wanapokea rushwa. Mada yako ni nzuri isipokuwa haina nguvu kisheria kwa sababu imekosa uthibitisho wa utata unaoonekana! Hapo askari hao hawana kosa lolote kaka. Ni mimi mpenda haki: Kandidus
Kimsingi fikirini kwanza kabla hamjatoa mada katika jamii forum ili tuzijadili. Jeshi la Polisi Tanzania kupitia kikosi cha Usalama Barabarani linapaswa kupongezwa kabisa. Mtoa mada uliyepiga picha hii, ebu tafuta takwimu za ajali kwa miaka miwili tu ilyopita, utakuja kukiri kuwa kwa miaka miwili iliyopita katika barabara ya dsm-morogoro - iringa kulikuwa na ajali nyingi zilizosababisha vifo vya watanzania wengi, na wengine kubaki kuwa tegemezi baada ya kukatwa viungo vyao vya mwili. Hii ni kwa sababu magari hayo uliyoyapiga picha hayakuwa yanafanya kazi barabarani kuthibiti wavunja sheria za barabara hususani mwendo kasi ambao siku zote umekuwa chanzo cha ajali zilizowaua watanzania ambao ndo nguvu kazi ya taifa letu.
Kutokana na sababu hiyo basi, Kwa mwaka huu 2012 kamanda Mpinga amekuja kivingine kwa kushirikiana na wakuu wa vikosi vya Usalama Barabarani wameweka mikakati ya kuongeza vithibiti mwendo na magari ya high-way patrol ili kuhakikisha wanafikia malengo ya kuthibiti ajali za barabara kuu kama sio kuzuia kabisa. Kutokana na ukweli huu basi, kwa madereva na wananchi wasiotii na kujua athari za ajali mf. aliyetoa mada hii, hawatambua hata kidogo utendaji wa trafic wakiwa barabarani. Kwa ujumla picha hii haina uhusiano hata kidogo na mazingira ya rushwa. Kwani gari la polisi katika picha hii hapo juu linaonekana limepaki barabarani inawezekana ikawa kwa sababu mbalimbali: 1. wameharibikiwa 2.kunataarifa wanaisubiri, 3. wanangoja msafara maana ndo kazi zao hizo, 4. wanawangoja askari wenzao ambao wamekwenda kuarest kwani hawawezi kwenda mpaka eneo la kuarest wakiwa na gari kwani mtuhumiwa angeweza kukimbia, 5. wapo katika taratibu zao za kazi n.k
Ushauri kwa mtoa mada:
Askari polisi wanafanya kazi katika mazingira magumu sana, na hivi wanapaswa kupongezwa kwa kazi wazifanyazo. Amani inayoonekana nchini kwetu ni kwa sababu ya utendaji wao kwa kushirikiana na vyombo vingine vya dola. Askari hao utambue ni binaadamu kama wewe. Ili kuwarahisishia utendaji wao yatupasa sisi wananchi hasa madereva tutambue kwanza wajibu wetu tukiwa tunatumia vyombo vyetu vya usafiri katika barabara wanayoitumia watu wengi. Tukiwa na desturi ya kutii sheria tutawaepuka hao askari ambao kwa kupaki gari zao tu, wewe umewaona kana kwamba wanapokea rushwa. Mada yako ni nzuri isipokuwa haina nguvu kisheria kwa sababu imekosa uthibitisho wa utata unaoonekana! Hapo askari hao hawana kosa lolote kaka. Ni mimi mpenda haki: Kandidus