kandidus
Member
- Feb 6, 2012
- 70
- 17
Haya wanajamii!
Inanishangaza kusikia kwamba walewale askari wa usalama barabarani waliosemekana kubuni mbinu mpya ya kupokea rushwa kwa mtindo wa kutega gari likiwa linaoshwa kama iilivyopigwa picha na mtaalam wetu (njele) wiki tatu zilizopita, traffic hao hao wameonekana tena laivu wakikataa kitita cha pesa shilingi milioni 7 za kitanzania walizokuwa wanashawishiwa kupewa na dereva mmoja aliyekamatwa na maelfu ya kilo za nyara za serikali (pembe za ndovu) juzi tarehe 08/02/2012 eneo hilo hilo la maseyu mikese morogoro. Pembe za ndovu hizo zilikuwa katika gari aina ya land cruiser iliyowekwa namba za DFP. Sasa WATANZANIA WENZANGU TUJIULIZE akiwemo mtoa mada iliyopita (NJELE), juu ya VITA DHIDI YA RUSHWA kuwa askari hao wa usalama barabarani kama kweli huchukua rushwa, wangeziacha mamilioni hayo ya pesa ambazo dereva alikuwa akizitoa tena kwa siri ili ajinasue na tatizo alilokamatwa nalo? Watanzania mnasemaje?
Na Kandidus
Inanishangaza kusikia kwamba walewale askari wa usalama barabarani waliosemekana kubuni mbinu mpya ya kupokea rushwa kwa mtindo wa kutega gari likiwa linaoshwa kama iilivyopigwa picha na mtaalam wetu (njele) wiki tatu zilizopita, traffic hao hao wameonekana tena laivu wakikataa kitita cha pesa shilingi milioni 7 za kitanzania walizokuwa wanashawishiwa kupewa na dereva mmoja aliyekamatwa na maelfu ya kilo za nyara za serikali (pembe za ndovu) juzi tarehe 08/02/2012 eneo hilo hilo la maseyu mikese morogoro. Pembe za ndovu hizo zilikuwa katika gari aina ya land cruiser iliyowekwa namba za DFP. Sasa WATANZANIA WENZANGU TUJIULIZE akiwemo mtoa mada iliyopita (NJELE), juu ya VITA DHIDI YA RUSHWA kuwa askari hao wa usalama barabarani kama kweli huchukua rushwa, wangeziacha mamilioni hayo ya pesa ambazo dereva alikuwa akizitoa tena kwa siri ili ajinasue na tatizo alilokamatwa nalo? Watanzania mnasemaje?
Na Kandidus