Candid Scope
JF-Expert Member
- Nov 8, 2010
- 11,883
- 6,884
Jambo moja muhimu ambalo linalalamikiwa na watu muda mrefu wabunge kupewa nyadhifa nyingine serikalini na hivyo kutokuwa karibu na wananchi ili kusaidia kuihimiza serikali kuleta maendeleo kwa wananchi. Waziri Nchimbi hapa atatoa utetezi gani, kwani ni mbunge wa Songea Mjini ambako ndiko kuliko hili soko kuu la Songea Mjini na papo hapo ni kiongozi mwandamizi serikalini, je ataendeshaje kofia hizo mbili kwa ufanisi huku zikikinzania na kusababisha maendeleo kudumaa?