Picha: Ofisi ya CCM Mbinga yachomwa Moto

Picha: Ofisi ya CCM Mbinga yachomwa Moto

Mbinga pale napo pana mwamko,,which is good. Ccm tumewachoka sana tu
 
Hebu acheni utani. Ofisi ichomwe moto halafu htundiata pazia na vitambaa vya mezani visiungue! Au ni vya chuma?

Unajua nini; hilo pazia linaonekana lilitolewa na kuchomewa nyumbani halafu likarudishwa na kutundikwa tena ndio maana vitambaa vya mezani viko ok.
 
Aaah! Mbona halijaungua? Haya macho ya uzee haya huyo bibi kafanana na MWICHEX a.k.a CHEZ NTEMBA.
 
Polisi wengi wanaofanya kazi Arusha pamoja na Traffic wamesikitika sana na wanatengwa na jamii.

Wengi wa Polisi wemepanga mitaani, wanaenda bar za mitaani, wamejenga pia..


Sasa kitendo cha kutumika na Nyinyiem kulipua mkutano wa chadema na kesho yake kupiga mabomu kumewatenga na jamii, wanaonekana kama magaidi.

Polisi wanajieleza sana na kuomba msamaha na kusema wao hawahusika, Polisi walioletwa kutoka Morogoro na Kibaha ndo walitumika.

Huu mtindo wa serikali kuhamisha polisi kwenda kuua mikoa mingine ni cha kukemewa na watanzania wote wapenda amani. Mashirika ya Haki za binadamu na vyama vya wafanyakazi mbona wako kimyaaa??

Kwa mfano chama cha waaalimu, chama cha madaktari, TUCTA, chama cha wanasheria tanganyika, viongozi wa dini, kwa pamoja wakemee vitendo vya polisi kutumika na mafisadi na pia kauli ya PM.

Natoa wito kwa Polisi na JWTZ, wawe wazalendo kama baadhi ya usalama wa taifa, ambao wanasaidia kuvujisha siri za vikao vya kuihujumu CDM.

Mie nashangaa, Polisi akistaafu hapewi hata ukuu wa wilaya, ukuu wa Mkoa ama ujumbe wa board!!!!!.....
 
JK.jpg


Kama unavyoona katika picha hapo ni ndani ya ofisi baada ya moto kuwaka


6.JPG

Huu ni mlango uliomwagiwa mafuta katika upenyo kisha kuwashamoto ambao haukuleta madhara kama ilivyo kusudiwa na wachomaji.
5.JPG

Katibu wa chama cha Mapinduzi wilaya ya Mbinga Anastasia Amasi anayeonekana katika picha akitoa maelezo kwa nje ambapo walimwaga mafuta aina ya petroli dilishani na kuwasha moto
WATU wasiojulikana wamechoma moto jengo la ofisi ya Chama cha Mapinduzi wilaya ya Mbinga mkoani Ruvuma..


Akithibitisha kutokea kwa tukio hilo katibu wa chama cha Mapinduzi wilaya ya Mbinga Anastasia Amasi amesema kuwa tukio hilo lilitokea usiku wa kuamkia Juni 21 mwaka huu ambapo watu wasiojulikana walichoma moto moja ya jengo la ofisi za chama hicho wilayani humo .


Moto huo ulielekelezwa katika chumba cha ofisi ya katibu ambapo walivunja vioo na kuchoma moto mapazia lakini kabla hawajachoma vitu vilivyokuwemo ndani walikimbia na kuacha dumu lililokutwa likiwa na mafuta aina ya petroli.


Alisema kuwa mpaka sasa hakuna hisia zozote zinazohusiana na tukio hilo ingawa uongozi wa chama cha mapinduzi wilayani humo umeshatoa taarifa kwenye vyombo ya ulinzi na usalama ambavyo vinaendelea na uchunguzi wa tukio hilo.


Katika hatua nyingine , hali ya sintofahamu imejitokeza katika uchaguzi wa viongozi wa halmashauri ya wilaya ya Mbinga baada ya halmashauri hiyo kugawanywa na kuzaliwa kwa halmashauri mpya ya wilaya Nyasa kwa kuibuka kwa vitendo vya hujuma vinavyodaiwa kufanywa dhidi ya mgombea mmoja wa nafasi ya mwenyekiti jina lake kuenguliwa katika mazingira ya kutatanisha na kuzua maswali mengi miongoni mwa madiwani wa halmashauri pamoja na wananchi na kutaka uchaguzi huo usifanyike mpaka majina yote matatu ya wagombea yawepo.


Mmoja wa wananchi wa halmashauri hiyo ya wilaya ya Mbinga ambaye pia ni katibu mwenezi wa chama cha mapinduzi wa kata ya Mbinga mjini Monika John alisema kuwa hizo ni dalili za kuwepo kwa njama za wazi za kupanga safu ya uongozi ambao siyo chaguo la walio wengi bali ni chaguo la baadhi ya viongozi wa halmashauri hiyo kwa masilahi yao.


Akizungumzia hali hiyo katibu wa chama cha mapinduzi wilaya ya Mbinga alisema kuwa uteuzi wa wagombea wa nafasi hizo hufanywa kwa kuzingatia kanuni za chama na wenye jukumu la mwisho la uteuzi ni uongozi wa chama ngazi ya mkoa na yeye si msemaji wa maamuzi ya ngazi mkoa ingawa amepokea tarifa ya kusitishwa kwa uchaguzi huo mpaka taarifa nyingine itakapotolewa na ofisi ya chama ngazi ya mkoa.

Kwa hisani ya MPEKUZI
 
Ikumbukwe kwamba majuzi tu kumekuwepo na mvutano kati ya baraza la madiwani na uongozi wa halmashauri katika wailaya ya mbinga juu ya uchauguzi wa ndani wa baraza la Madiwani, kwani madiwani walishinikizwa kumchagua yule wasiyemtaka kwa masilahi ya wakubwa.
 
Hakuna moto hapo watu washachukua chao mapema(ccm) sasa wanataka tu kupoteza ushahidi.
 
Mbona hijaungua vizuri?
Siku ingine wahakikishe wanamwaga mafuta mengi.
 
Back
Top Bottom