Picha: Miji ya Luanda nchini Angola

Picha: Miji ya Luanda nchini Angola

hii ni kawaida ya watawala wa kiafrica, kama ilivyo kwa mama Ngina alivyomiliki Kenya kupitia mme wake Kenyatta Sr. na huyu Isabel anamiliki Angola kwa kupitia baba yake, Dos Santos

Halafu baadhi yetu bila taarifa sahihi wanasifia hiyo Angola na kutamani tuendelee kwa staili hiyo......
 
barabara safi hadi raha.....barabara zetu zinatia kichefuchefu ....zimejaa michanga kibao....sasa unashangaa hiyo ni barabara ya rami ama barabara ya mchanga........uchafu umezagaa barabarani ....yani nasikia hasira tu hapa.........
 
bado hawajatambua kuwa Luanda inamilikiwa na wafanyabiashara kutoka portugal na spain wakishilikiana na rais wa nchi hiyo, wananchi wa kawaida hawanufaika na chochote japokuwa ni nchi ya madini, gesi na mafuta..

Exactly mkuu. Ni kikundi tu cha watu kinaendeleza Luanda kwa maslahi ya wachache. Ndo maana kote wanakoonyesha huoni watu hata kwenye makazi. Na wachache walioonekana sio 'watamu'.

Dar, japo haivutii kama huko Luanda, picha chache tu zilizowekwa unaona mishemishe kibao.

Ni bahati mbaya waTz wengi wanashobokea nje bila kujua wao hasa wanataka nini. Hivi Dar leo hii ikijaa mabarabara na maghorofa makubwa, wangapi kati yetu watayatumia?

Kuliko kufocus kwenye majumba na barabara za Dar pekee, kuna ya msingi kama vile ubora wa elimu, tija kwenye utumishi wa umma, madaraja mengi zaidi kuvusha mazao, tiba bora hospitali za umma, etc.

WaTz tuchukue fursa kwenye uchumi na rasilimali zetu. Sawa ccmscrow wanabana, basi na tuwatoe. Binafsi nawatoa Oktoba. Na nilianza tangu serikali za mitaa.

Tunavyozidi kukamata fursa na kuzitumia, hayo maghorofa na mabarabara ni derived demand.

Sasa hivi hapo Dar, wamatumbi wamekimbilia segerea, mabwepande, mbezi, yombo, mbagala mwisho, n.k. then haohao wanasifia maghorofa kwa wengine. Dar ya nini wakati watu hawayawezi?

Tung'ang'anie vipaumbele sahihi. Sio kila king'aacho dhahabu, na sio kila kizuri tunakihitaji sasa.

Btw, kimfaacho mtu chake.
 
bado hawajatambua kuwa Luanda inamilikiwa na wafanyabiashara kutoka portugal na spain wakishilikiana na rais wa nchi hiyo, wananchi wa kawaida hawanufaika na chochote japokuwa ni nchi ya madini, gesi na mafuta..
hat tz inamilikiwa na wahindi waharabu wakishirikiana na president huoni anavowekeza miradi ya mabilioni huko kwao haya bandari inajengwa Bagamoyo, gesi inaenda bagamoyo stand ya ubungo itagawanywa wale wa tanga moshi arusha na sehemu nyingine stand itakuwa tegeta kwa hio mabasi yatapitia bagamoyo, maroli yatapitia bagamoyo morogoro road yanaongeza foleni ,bado tu wanataka kujenga na airport bagamoyo
 
Wametuacha kwenye majengooç na hizo barabara tu na ni Luanda tu!
Mengine nenda huko ukayaone........!
 
Back
Top Bottom