na yale malori yaliyokuwa yanasomba washabiki gharama zake zimejumuishwa?
Inasema malori yalianza kuleta watu saa 12 asubuhi.Malori mengi yalileta watu kutoka Rufiji,Kisarawe,Bagamoyo na kuna waliosombwa kutoka Lindi.
na yale malori yaliyokuwa yanasomba washabiki gharama zake zimejumuishwa?
Hakukuwa na haja ya kutumia fedha kiasi hicho kwa tukio kama hilo. Bora hata wangepewa wabunge wao kuchangia shughuli za maendeleo au wangetafuta kundi la vijana wakaanzisha miradi midogo midogo kupunguza tatizo la ajira naamini wangekitangaza chama chao maradufu kuliko hili tukio halina impact yeyote kwa uchumi wetu wala chama chao. mil 10 hadi 20 zinatosha tena nyingi.
feasibility study vijibweni 19 mil. Source aweda
rip cuf
Vyama vingi vya siasa, vina ujanja wa kuteka watu uwanjani na kuona kuwa wana watu wengi.Habari kutoka makao makuu ya chama cha wananchi CUF ni kuwa kimetumia milioni 150 kwa ajili ya kumpokea mwenyekiti wao prof Lipumba,matumizi inahusisha posho kwa viongozi mbali mbali,usafiri wa ndege kwa wajumbe kutoka Zanzibar na maeneo mengine ya Tanzania bara,wametumia pia kulipia Star tv matangazo ya live,pia pesa zingine wamepewa vijana na wazee wa chama hicho kwa ajili ya kujitokeza kwa wingi kumlaki prof Lipumba ili watu waone kuwa bado CUF inapendwa wakati ipo icu.
Hii ni sawa na kuficha uchafu uvunguni ili baba asione,wanasahau utakuja nuka soon,Lipumba angeachana na siasa uchwara aanzishe hata taasisi ya consultancy za uchumi na mipamboo ili atunusuru na balaa la omba omba,biashara ya magogoni haimfai tena asije akapata kura za mrema.
CUF bwana kweli ni CCM tupu!
Hata tabia ya kubeba watu kwenye malori!
Na afande Sele kweli na akili zake amepewa nini hadi kwenda kwenye chama kichovu hivi!?
Hukumbuki wangenga walisema palipo na miti mingi hakuna wajenzi? Kama umewahi kumwona Fundi uashi ana nyumba yake nzuri ujue sio fundi mzuri sana. Vile vile Mafundi seremala wengi hawana fernichers nzuri majumbani mwao. Umeshamwona fundi mshona nguo anavaa nguo bomba? Ukimwona basi huyo ni msimamizi tu sio fundi cherehani. Je, Umeona wapi Askofu watoto wake wakawa na tabia nzuri sana? Ulizia kama utakuta watoto wengi wa walimu wana akili sana. Only the exceptions which however, are very few!!!!
Tanzania imelaaniwa laana ambayo kina Mwakasege wanapigia kelele kila siku ili kuikemea ishindwe na kulegea ktk JINA KUBWA KABISA la YESU KRISTO, lakini laana hiyo haitoki kirahisi sababu wanaowazunguka katika maombi hayo nao wametingwa na dhambi kibao hata zinawasuta wakati wa maombi na hatimaye maombi yanazuiwa kufika JUU mbele ya Muumba, Kanchi katajiri sana lakini kananuka umaskini sababu wapo watu wanatambika sana kujilimbikizia utajiri kwa kuweka misukule kwenye ofisi zao, vitega uchumi vyao, uongozi wao......hata wengine huua watoto wao ili watajirike upesi lakini hawadumu sana, wenzao wanaobaki wala hawaoni hayo maana shetani anawasahaulisha. Hii ni vita ya kiroho. Bila kujali dini gani ni lazima watanzania wote tuamke, tutubu na kutakasika na ndipo tumwombe Mungu atuonee huruma. Hatupigani lakini nchi zinazopigana zinapaa kiuchumi. Sisi tunawaita wageni waje wale, wanye waondoke na kila wanachokitaka kutoka kwetu, nasi wanaturushia sumni kama vile makonda wanavyowafanyia wapigadebe, halafu tunafuraaaaaahi ajabu. Kama sio laana ni nini hiyo. Unaweza kuiona vizuri Tanzania ukitoka nje kidogo tu, itazame kutoka kule ndo utajua laaana hapa ndio amri ya kila siku tunaitumikia.
Aaghrrrr!!!
Message sent and delivered, I am not sure it is read. kila munu abena kwabo. Tusali sana sio mchezo, tena kwa kumaanisha.
Ni kweli mkuu wangu.Malori yamesharudisha watu kwao wamelipwa chao na bado chama kiko ICU
Inafurahisha sana kuona kiongozi aliyethaminiwa na dunia akipokewa na wafuasi wa chama chake kwa shangwe na furaha.
Inasikitisha sana kuona hii haikuwa Kitaifa.
looser! sema kingine
Inafurahisha sana kuona kiongozi aliyethaminiwa na dunia akipokewa na wafuasi wa chama chake kwa shangwe na furaha.
Inasikitisha sana kuona hii haikuwa Kitaifa.