PICHA: Makamba hizi si kampeni za urais

PICHA: Makamba hizi si kampeni za urais

attachment.php
attachment.php
attachment.php
attachment.php
 
acheni vijana wale pesa za wagombea ila wao wanajua watampigia nani kura. Ila kwa ujumla tunakoelekea kama Taifa ni shimoni:cool2: maana tumefunika macho huku tunatembea halafu tunajifanya tunaona, ni aibu ilioje? MWENYE UFAHAMU NA AFAHAMU
 
Mababu wako wengi sana ccm na wote wamejaribu kuwania urais...mzee john aka baba le-mutuz,salim.a.salim wote hao ni babu ila hatuwadharau kama ww unavyomdharau mzee wetu..Mungu akubariki umalize mwaka salama pamoja na dharau zako

Wapi nilipoonyesha DHARAU kwa BABU?
 
Naibu wizara ya Nishati na madini,na huku bima ya Afya!Mbona sikuelewi Makamba?Ungekuwa naibu waziri wa Afya sawa au hata uchukuzi na usafirishaji,lakini Madini Makamba?Na kile kikao cha Wachungaji(viongozi wa dini) juzi usiku?Husijali kijana,tutakukumbuka 2015,ila hela hizo unazotumia unazitoa wapi??????!

Bodaboda zinatumia mafuta budaaaaaaa, hauoni kuwa yeye anahusika hapo.

ila kumbuka zitto alishatuambia tusiwaamini wanasiasa hata kama anatoka upinzani.

 
Watu wajinga mpka nashangaaa, mnaosema dogo anataka ursis mnashindwa tumia akil zenu za kuzaliwa mnaanza tumia mata4o, ana miaka mingap nao kufka 2015 je atakuwa kafkisha 45? N hvo tuuu
 
Hawa bodaboda wanatumika vibaya

Boda boda ghafla wamegeuka kuwa mtaji wa kisiasa! Machinga shauri yenu naona mnaanza kuenguliwa sasa Boda Boda wanachukua hatamu!!

Nchi hii ngumu kweli kweli yaani hawa Boda Boda sasa watakuwa hawagusiki kwani ukiwagusa tu utasikia acha kuwasumbua wapiga kura!! Wamachinga walipata viburi hadi kuanza kupanga bidhaa katikati ya barabara kwa kuwa tu ni kundi la wapiga kura sasa na hawa Boda Boda mtayaona matokeo yake kuna siku watazuia taxi na daladala zisifanye kazi na hakuna wa kuwagusa kwa kuwa ni wapiga kura!!
 
Boda boda ghafla wamegeuka kuwa mtaji wa kisiasa! Machinga shauri yenu naona mnaanza kuenguliwa sasa Boda Boda wanachukua hatamu!!

Nchi hii ngumu kweli kweli yaani hawa Boda Boda sasa watakuwa hawagusiki kwani ukiwagusa tu utasikia acha kuwasumbua wapiga kura!! Wamachinga walipata viburi hadi kuanza kupanga bidhaa katikati ya barabara kwa kuwa tu ni kundi la wapiga kura sasa na hawa Boda Boda mtayaona matokeo yake kuna siku watazuia taxi na daladala zisifanye kazi na hakuna wa kuwagusa kwa kuwa ni wapiga kura!!

vipi waendesha daladala na taxi wao sio wapiga kura
 
vipi waendesha daladala na taxi wao sio wapiga kura

Mkuu hata wewe ni mpiga kura. Ninachokisema ni kwamba kundi hili linaonekana lina influence kubwa sana kisiasa kushinda hata wamachinga kwa sasa pamoja na hao wa taxi na daladala.
 
Naibu wizara ya Nishati na madini,na huku bima ya Afya!Mbona sikuelewi Makamba?Ungekuwa naibu waziri wa Afya sawa au hata uchukuzi na usafirishaji,lakini Madini Makamba?Na kile kikao cha Wachungaji(viongozi wa dini) juzi usiku?Husijali kijana,tutakukumbuka 2015,ila hela hizo unazotumia unazitoa wapi??????!
Kuwa makini unadhalilisha jukwaa,Makamba toka lini akawa wizara ya nishati na madini?
 
Vijana nawasihi pokeeni hizo pikipiki, tumieni maana no hela walizotuibia, lakini piga chini mizigo wote
 
Ngoyai naye anatumia bodaboda kunyemelea urais. Alionesha udhaifu kwa kutowatahadharisha na ajali na ujambazi!
 
Hii TZ yetu inadhalilishwa kupita kiasi, hivi kuwa mwandishi wa hotuba za Rais ndo kunakufanya uvimbe kichwa kihasi hiki eti unaweza kuingoza TZ. kumbe hata mwanafunzi anayewaandikia wanafunzi wenzake notisi ubaoni anaweza kuwa mwalimu!!!! Huu ni upuuzi uliopitiliza . TZ amka.
 
NAIBU wa Waziri wa Wizara ya Sayansi na Teknolojia January Makamba ametaka ujio wake Jiji la Mwanza usihusishwe na Kampeni za chini kwa chini za Urais bali ni kutekeleza ombi la Umoja wa waendesha pikipiki Mkoa wa Mwanza kuwasaidia kupata Bima ya Afya baada ya kuwawezesha kupata pikipiki 1745 za FEKON na si vinginevyo.

Kauli hiyo ya Makamba ameitoa leo wakati wa kufungua kongamano kubwa la siku moja la Umoja wa Madereva wa pikipiki Mwanza lililofanyika katika uwanja wa michezo wa Nyamagana Jijini hapa, alisema kwamba kuna baadhi ya watu wameanza kuhoji ujio wangu Mwanza “Niko hapa kwa ajili ya shughuli hii mliyonialika bali kuja kushiriki Kampeni muhimu ya Bima ya Afya kwa ajili ya Usalama wa badae” na si vinginevyo.

Makamba amesema kwamba upatikanaji wa Leseni kwa urahisi na uharaka usiwe tiketi ya Kifo kwa wananchi.View attachment 129062View attachment 129063View attachment 129064View attachment 129065

LAU MASHA kajificha wapi? Kwahiyo January next trip ni ARUSHA BODABODA ?
 
Atakwenda lini Kigoma kwa Zitto kutoa hizi ajira?
 
Kuwa makini unadhalilisha jukwaa,Makamba toka lini akawa wizara ya nishati na madini?

Asante kwa kunikosoa mkuu,nilikuwa nimechukia hata sikuweza kuwaza sawasawa,nachukia wanasiasa wanaotumia umaskini wa Watanzania kama mtaji wao wa kisiasa!Hivi hizi hela wanazitoa wapi?Mheshimiwa Sumaye naye kasema kuna wajumbe wametumiwa kadi za Xmas zikiwa na kitita cha fedha ndani!Zinatoka wapi hizi hela na zitarejeshwa vipi?
 
Back
Top Bottom