Bibianna
JF-Expert Member
- Jun 6, 2025
- 400
- 135
===
Akiongea na wanahabari Mkuu wa Mkoa wa Kagera amesema Chini ya Rais Samia Serikali imetoa jumla ya TZS 103,376,838,198 kwa sekta ya nishati mkoani humo, ambapo vijiji vyote 662 sawa 100% na vitongoji 1,763 kati ya 3,665 (48%) vimeunganishwa na umeme, Miradi hii minne mikubwa ya umeme wa maji yenye jumla ya MW 221.8 imetekelezwa na hivyo Tanzania kuwa na ziada ya umeme.
Mradi wa Rusumo (Ngara) – MW 80, umekamilika.
Murongo/Kikagati (Kyerwa) – MW 14, umekamilika.
Kakono (Missenyi) – MW 87.8, upo hatua ya upembuzi yakinifu.
Nsongezi (Kyerwa) – MW 40, maandalizi ya awali yanaendelea.
Mafanikio haya yamewezesha Mkoa wa Kagera kuunganishwa na Gridi ya Taifa, hivyo kuondokana na utegemezi wa umeme kutoka Uganda na jenereta kama ilivyokuwa awali na sasa umeme unauzwa nje.