Mama mbavu zangu... nimecheka mpaka nimepaliwa mkuu!
Na hizo comments ndiyo zimenimaliza kabisa...
Duh! kweli nchi yetu imemalizika kabisa, jembe na shoka vimewekwa chini, ngao inaungua, maandishi ya uhuru na umoja yamefutiliwa mbali huko... mzee wa tembo kabeba pembe yake anakimbia kivyake na mwenyekiti wa WAMA naye kabeba pembe ingine anakwenda kuihifadhi kwa ajili ya maslahi ya familia. Kweli, walichoshindwa kukiondoa hapo kwenye picha ni mlima Kilimanjaro tu, lakini ngao inavyoungua ikifika mwisho na mlima utawaka moto...
Chukua Chako Mapema...