Ilitokea ghafla katika barabara ya Makongolosi kuelekea Rungwa mkoani Mbeya. Ghafla kwenye kona mnyama simba kakutwa kajipumzisha katikati ya barabara eneo la pori la simba.
Wakati magari yakiwa yamesimama, mara Bodaboda akatokea na bila kujua akataka kuyapita kwa kasi (kuchepuka) ndipo alipokutana uso kwa uso na mnyama huyo hatari. Hata hivyo aliweza kugeuka na kukimbia wakati na simba naye akanyanyuka na kuingia porini.
Wakati magari yakiwa yamesimama, mara Bodaboda akatokea na bila kujua akataka kuyapita kwa kasi (kuchepuka) ndipo alipokutana uso kwa uso na mnyama huyo hatari. Hata hivyo aliweza kugeuka na kukimbia wakati na simba naye akanyanyuka na kuingia porini.