PICHA: Athari za mvua jijini Dar es Salaam

PICHA: Athari za mvua jijini Dar es Salaam

kaka watu8 hilo eneo jana limesomba daladala jioni,nilikuwa na jamaa zangu wametoka home walikuwa katika hiyo gari....
sasa huku kisarawe kuanzia pugu hadi vigama road imeharibika kwa maporomoko ya udongo

Duh!!!

Mkuu kulikuwa na vijana wanaongoza magari hapo kwa ujira mdogo, nadhani hao waliosombwa walipita nyakati ambazo vijana hao wameondoka
 
watu8 sikatai yote hayo ila nikweli Tanzania pekee ndio tunaathika na mvua? Mambo mengine hayakwepeki mkuu hii mvua ni kubwa sana, siku nne non stop

Mkuu nimeishi nchi ambayo ina mvua kubwa kuliko hizi lakini huwa hakuna madhara kama haya ya kwetu....

Miji yetu ina drainage mbovu hakuna mfano kaka, kuna ujenzi holela usio kifani halafu serikali ipo tu...
 
8.jpg


huyu dada sio munkari kakimbia ualimu vijijini ndio yuko mjini anatafuta kazi na mvua inamuharibia pozi????
 
Yaani"

hivi serikali inashindwa kuwabana kina NSSF na PPF wajenge maghorofa yenyenyumba za vyumba hata viwili wapangishwe Watu wa mabondeni, wakusanye kodi na wawape muda hata wa miaka mitatu au nne kuishi humo. Kisha wajipange kutafuta maeneo ya kujenga nyumba zao za kudumu Baada ya hiyo miaka minne. Badala ya kujenga mijumba ya mamilioni inayoweza kununuliwa na mafisadi.

Mashirika ya pensheni sawa na mabenki sio rafiki kwa masikini ndio maana ili ujiunge kuwa mwanachama lazima uwe mwajiriwa.
Hoja kubwa ya wanaoishi mabondeni kukataa kuondoka ni kutokana na wengi wao wanategemea sekta zisizo rasmi na vibarua visivyonauhakika maeneo ya kariakoo na Posta, hivyo kuondoka na kuhamia mabwepande kwao ni kufa njaa kwani hawatakuwa na uwezo wa hata kugharamia nauli ya mabasi mawili. Hivyo wameamua LIWALO NA LIWE bora kufa maji kuliko kuhama. NI mtazamo tuuuu.
 
Kuna wakati aliekuwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mzee Makamba aliwakemea watu wanojenga kwenye mabonde,namnukuu "hivi nyie watu mnaopenda kujenga kwenye mabonde ya mito mmekuwa vyura?" Tatizo hapa sio CCM, tatizo ni watanzania tumekuwa wabishi, hatuwasikilizi viongozi wetu mpaka maafa yatokee ndo tunaanza kuliaumu serekali! Walishaambiwa siku nyingi hawa lakini wamekuwa viziwi na sasa wanavuna walichokipanda. Ukweli ndo huo na unauma.

usiongee kama mkumbavu wewe mjinga! Serikali iliahidi kutoa viwanja kwa waliokumbwa na mafuriko ile 2011 na nina ndugu zangu ambao waliathirika pia. Kwa kuwa mimi ninaishi Bunju nikaamua kuchukua jukumu la kufuatilia hivyo viwanja ili vikipatikana walau tuwajengee nyumba. Nilianzia mabwe pande, nikaenda ofisi ya mtendaji mchikichini, nikatinga ofisi ya mkuu wa wilaya pale Boma halafu nikaelekezwa ofisi za jiji. Ambako mwishowe muhusika akaniweka wazi kuwa Viwanja hakuna na kuna watu wa tangu 2009 mpaka leo wako kwenye makambi.
Tusiwasikilize sana wanasiasa wanaodanganya watu kuwa wahanga wanakataa viwanja na kung'ang'ania mabondeni. Ni mwehu tu ndie anaeweza kung'ang'ania bondeni kama hali ile ya mafuriko imemkumba!
Huu ni wakati wa kuwasema watendaji wanaosingizia kugawa viwanja kumbe wanapeana
wenyewe. Siku nyingine usiropoke tena ---- we!!
 
hongera sana kwa mpiga picha!!!! endeleza fani. njia ya Goba ndio njia yangu kubwa mpaka KUNGURU.
 
Nikweli mkuu

Lakini hiivi ni kwanini kila mwaka ni mafuriko tu?

Mungu kama ananisikia ningeomba inyeshe mvua ambayo itasababisha mikoa muhimu yote nchini kuzama kabisa na asipatikane hata mtu mmoja ili angalau tujulikane vile ambavyo hatuna maana kwenye vichwa vyetu

Utadhani hatuna serikali!
Kiongozi hapo indirectly unamaanisha kuwa MUNGU ai-reform nchi hii pamoja na tunu zote alizotupa.Nadhani MUNGU wetu ana rehema nyingi tu na pengine kwa matukio kama haya anataka atufikishe kwenye 'breaking point yetu' ili tusimame na tulete mabadiliko sisi wenyewe katika ku-rebuild nchi hii ambayo ametupatia bure.
Na kwa ninavyoona taratibu tunajifunza. Kujifunza kwa kushiriki suala husika(learning by experience) ni namna nzuri sana ya kujifunza.
Wacha kwanza tuendelee kujifunza kwa kupitia haya majanga pamoja na uchungu tutakaopata kwa kupoteza tuwapendao basi tutaamka tu.
 
Kiongozi hapo indirectly unamaanisha kuwa MUNGU ai-reform nchi hii pamoja na tunu zote alizotupa.Nadhani MUNGU wetu ana rehema nyingi tu na pengine kwa matukio kama haya anataka atufikishe kwenye 'breaking point yetu' ili tusimame na tulete mabadiliko sisi wenyewe katika ku-rebuild nchi hii ambayo ametupatia bure.
Na kwa ninavyoona taratibu tunajifunza. Kujifunza kwa kushiriki suala husika(learning by experience) ni namna nzuri sana ya kujifunza.
Wacha kwanza tuendelee kujifunza kwa kupitia haya majanga pamoja na uchungu tutakaopata kwa kupoteza tuwapendao basi tutaamka tu.

Mkuu juzi tu mtoto wa Mgimwa ameshinda kwa "kishindo"
Juzi mtoto wa Mkuu wa nchi nae kashinda kwa kishindo

Wote hawa ni kutoka kwenye serikali hiihii ambayo kila mwaka kunatokea haya majanga na haifanyi lolote

Unatarajia tutajifunza kweli?

Mkuu hii sahau

Dawa ni kuitokomezea mbali hii nchi na wakazi wake
Ni aibu kwa ubinadamu haya ambayo yanatokea hapa nchini!
 
Back
Top Bottom