Just Pray
JF-Expert Member
- Nov 7, 2023
- 2,142
- 4,779
Watu wasiofahamika Wamefariki Dunia kwa kuteketea kwa moto na kubakia majivu baada ya magari mawili kugongana uso kwa uso na kisha kuwaka moto na kuteketea na kusababisha vifo hivyo.
Akizungumza na Mwandishi wa habari hizi katika eneo la tukio Mei 29,2025 Mkuu wa wa Polisi Wilaya ya Mufindi SSP Anthony Gwandu, amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo huku akisema chanzo chake ni kuendesha kwa uzembe gari hilo.
SSP Gwandu amesema ajali hiyo imetokea Mei 28 , 2025 saa 19:05 usiku huko kata ya Sao hill Shamba la miti ya kupandwa la Serikali , barabara kuu ya Iringa - Njombe baada ya magari hayo mawili kugongana na kisha kuwaka moto na kusababisha uharibifu huo.
Amelitaja gari lenye namba za usajili AID 4830 ZM/ AID 4831 ZM aina ya IVECO Tenki ikiendeshwa na dereva Gimson Lungu (32) raia na mkazi wa Lusaka Zambia , ikiwa imebeba mzigo wa mafuta aina ya diesel likitokea Dar es Salam kwenda Congo (DRC) iligongana uso kwa uso na gari dogo.
Gari hilo dogo Toyota double Cabin ambayo namba zake na dereva bado kujulikana likitokea Makambako kuelekea Iringa liliungua na kuteketea kwa moto baada ya magari hayo kugongana uso kwa uso.
Hata hivyo Mkuu wa Polisi Wilaya ya Mufindi SSP Gwandu alisema uchunguzi zaidi unaendelea kubaini gari hilo dogo Toyota Double cabin kulikuwa na Watu wangapi zaidi ya dereva.
Aidha katika gari hilo dogo hakuna mabaki yoyote ya Binadamu yaliyoonekana zaidi ya majivu na kwamba chanzo kinachunguzwa zaidi huku dereva wa gari kubwa akiwa anashikiliwa na Polisi kwa mahojiano zaidi.
Akizungumza na Mwandishi wa habari hizi katika eneo la tukio Mei 29,2025 Mkuu wa wa Polisi Wilaya ya Mufindi SSP Anthony Gwandu, amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo huku akisema chanzo chake ni kuendesha kwa uzembe gari hilo.
SSP Gwandu amesema ajali hiyo imetokea Mei 28 , 2025 saa 19:05 usiku huko kata ya Sao hill Shamba la miti ya kupandwa la Serikali , barabara kuu ya Iringa - Njombe baada ya magari hayo mawili kugongana na kisha kuwaka moto na kusababisha uharibifu huo.
Amelitaja gari lenye namba za usajili AID 4830 ZM/ AID 4831 ZM aina ya IVECO Tenki ikiendeshwa na dereva Gimson Lungu (32) raia na mkazi wa Lusaka Zambia , ikiwa imebeba mzigo wa mafuta aina ya diesel likitokea Dar es Salam kwenda Congo (DRC) iligongana uso kwa uso na gari dogo.
Gari hilo dogo Toyota double Cabin ambayo namba zake na dereva bado kujulikana likitokea Makambako kuelekea Iringa liliungua na kuteketea kwa moto baada ya magari hayo kugongana uso kwa uso.
Hata hivyo Mkuu wa Polisi Wilaya ya Mufindi SSP Gwandu alisema uchunguzi zaidi unaendelea kubaini gari hilo dogo Toyota Double cabin kulikuwa na Watu wangapi zaidi ya dereva.
Aidha katika gari hilo dogo hakuna mabaki yoyote ya Binadamu yaliyoonekana zaidi ya majivu na kwamba chanzo kinachunguzwa zaidi huku dereva wa gari kubwa akiwa anashikiliwa na Polisi kwa mahojiano zaidi.
