PhD ya Musukuma yazua gumzo, Chuo kilichomtunuku hakitambuliki

Kingine ambacho wachunguzi wamekifuatilia ni vigezo ambavyo vimezingatiwa ili kumpa heshima hiyo Musukuma, yadaiwa ni mchongo mwanzo mwisho.
kanunua kwa dola 200, kweli huyu mtu ni mshamba kama ...................lilivyo 🤣
🤣 🤣
 
, nchi ngumu hii
Screenshot_20211208-124759_Chrome.jpg
 
Watanzania tumekua watu wa ajabu sana. watu wanapewa degree za heshima wanaona kitu kikubwa sana. Haya mambo huwezi kuyasikia nchi nyingine duniani. Ukitaka degree ya maana si uende ukasome.
 
Umeandika uharo. Hadi sasa nchini Tanzania sifa ya mtu kuwa mbunge ni kujua kusoma na kuandika. Sasa unatuambiaje hapa ?
Msukuma ni mtanzania mwenzetu ila amepotoka sana kuhusu swala la elimu kwake yeye anahisi kuwa na pesa ndio kuwa na akili nyingi. Siwezi kumlaumu coz psychologically an entertain defense mechanism ili aweze kusurve bungeni ambako kuna wasomi wengi. Asichokijua Mganga wa kienyeji king msukuma kuwa elimu ni mwanga wa jamii ni chungu kinachopika wataalamu wa fani mbalimbali ambao ni treasures of the nation. Mfano madaktari, walimu, marubani, wanamahesabu na wengine wengi. Ukisikiliza mijadala yake bungeni anavyo underrate wasomi utagundua tatizo lake kuwa ni "shule hamna kichwani'' ana attacks watu badala ya mifumo yenyewe ya elimu. Kuwa ni mbunge kama msukuma kwenye chombo cha kutunga sheria ni janga la kitaifa coz hawezi kufanya analysis badala yake atapiga majungu tu kama tulivyomzoea. Tunaomba wanazuoni wenye nia njema na taifa letu wapaze sauti zao za hekima kukemea kuwa na wabunge aina ya msukuma ni hatari kwa maendeleo ya elimu na taifa kwa ujumla
 
Wachunguzi wanadai kwamba eti Chuo hicho kiko India na kwamba kina matawi yake Uingereza na Marekani bali uchunguzi unaonyesha kwamba hakijawahi kusajiliwa Uingereza wala Marekani na wala hakipo huko.

Kingine ambacho wachunguzi wamekifuatilia ni vigezo ambavyo vimezingatiwa ili kumpa heshima hiyo Musukuma, yadaiwa ni mchongo mwanzo mwisho.

Baba Askofu Bagonza amenukuliwa kwamba aliombwa dola 500 na chuo hicho ili aingizwe kwenye mchakato wa watakaopewa PhD hiyo na hicho chuo cha Musukuma ila yeye akagoma na akawaambia wahusika kwamba anazo ofa kadhaa kutoka kwenye vyuo vikubwa duniani vinavyomuomba akubali kupewa PhD za heshima, tena kwa vyuo vyenyewe kumlipa hadi USD Elfu 10, siyo kwa yeye kuvilipa vyuo kama chuo cha Musukuma kinavyodai.

Swali ni hili, ni nani anafaidika na vyuo vya uongo kama hiki cha Musukuma na ili iweje?

Pia, soma=> Dkt. Joseph Kasheku Msukuma: Napitia post za wanaonibeza mitandaoni, kuanzia Ijumaa nitaanza kuwajibu

Mbona kama mavazi alijibebea mwenyewe toka Bongo to USA? Au alitunukiwa huku huku Buza??
 
Back
Top Bottom