Petro kalete jiwe!!

Nimecheka sana. Hii stori niliisikia zamani kwa mtindo mwengine kama ifuatavyo:

Siku moja Yesu alikuwa na wanafunzi wake wanapanda juu ya Mlima Sinai, walipofika juu hoi bin taabani kwa machofu na jua kali wanafunzi wake walihisi njaa. Yesu alifahamu mawazo yao akasema, "Petro kalete jiwe", Petro alinyanyuka na baada ya muda alirudi akiwa na jiwe mkononi. Alipompa Yesu akalibariki likawa mkate, akawagawia wanafunzi wake wakala. Lakini hawakushiba,hivyo wakaanza kumlaumu Petro, "mbona umeleta jiwe dogo?", Petro akawajibu, "msikujua kama atalibadilisha kuwa mkate!".

Siku nyengine tena wakiwa katika Mlima Sinai, baada ya mafundisho marefu na jua kali, wanafunzi walihisi njaa.Yesu alifahamu mawazo yao, akasema "Kila mtu alete jiwe". Basi wanafunzi walinyanyuka wakaenda kuleta mawe, kila mmoja akarudi na jiwe dogo kiasi chake isipokuwa Yuda (msaliti). Yeye alibingirisha mzinga wa jiwe huku akiwaza jinsi siku ile atakavyovimbiwa. Alipolifikisha Yesu alilikalia jiwe la Yuda na kuamrisha, "Petro, toa mikate mkobani mwangu uwagawie wenzako".
 

Hahahahahahaha hiyo kali mkuu
 

Ha ha ha haaaaa
 
Ni ukweli ama?

Its NOT true.
Imeandikwa, usiongeze wala kupunguza neno lolote.

Revelation 22
18 I testify to everyone who hears the words of the prophecy of this book: if anyone adds to them, God will add to him the plagues which are written in this book; 19 and if anyone takes away from the words of the book of this prophecy, God will take away his part from the tree of life and from the holy city, which are written in this book. 20 He who testifies to these things says, "Yes, I am coming quickly." Amen. Come, Lord Jesus.…
 

Yuda alikuwa mroho tangu utoto wake.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…