TANMO
JF-Expert Member
- Apr 12, 2008
- 11,511
- 11,271
Wakuu,
Katika pita pita yangu hapa JF leo nimekutana na hii taarifa kuhusu Pinda akiwa anahutubia huko Kagera. Kwa mujibu wa maelezo yake (kulingana na habari) inajidhihirisha wazi kuwa anajaribu kuwa-intimidate watu ili waiache haki yao ya kikatiba ya kuandamana. Kutokana na ukweli kwamba haya maandamano yalipata kibali na Baraka zote kutoka Polisi (chombo cha dola) basi Pinda hakutakiwa kutoa maneno ya vitisho kiasi hicho. Pia kutokana na vitisho hivi, ni dhahiri kuwa itafika kipindi Polisi (kwa kufuata amri kutoka Juu) itasitisha kuendelea kutoa vibali na kwa mantiki hiyo kusababisha uvunjifu wa amani iwapo raia watakaidi. Hii ni kauli inayodhihirisha wazi tabia ya viongozi wetu kupenda kuburuza raia wao kwa kutumia vyombo vya Dola.
Kwa mantiki hiyo basi, nimepata wazo kwamba inawezekana kabisa kuanzisha utaratibu wa kumshtaki huyu mtu kwenye Mahakama za kimataifa kwa ku-violate haki za Binadamu kulingana na Universal Declaration of Human Rights (1948).
Wataalamu wa sheria hapa JF mnaombwa kutoa mwongozo juu ya hili.
Wakuu wangu, naomba kuwasilisha hoja.
Katika pita pita yangu hapa JF leo nimekutana na hii taarifa kuhusu Pinda akiwa anahutubia huko Kagera. Kwa mujibu wa maelezo yake (kulingana na habari) inajidhihirisha wazi kuwa anajaribu kuwa-intimidate watu ili waiache haki yao ya kikatiba ya kuandamana. Kutokana na ukweli kwamba haya maandamano yalipata kibali na Baraka zote kutoka Polisi (chombo cha dola) basi Pinda hakutakiwa kutoa maneno ya vitisho kiasi hicho. Pia kutokana na vitisho hivi, ni dhahiri kuwa itafika kipindi Polisi (kwa kufuata amri kutoka Juu) itasitisha kuendelea kutoa vibali na kwa mantiki hiyo kusababisha uvunjifu wa amani iwapo raia watakaidi. Hii ni kauli inayodhihirisha wazi tabia ya viongozi wetu kupenda kuburuza raia wao kwa kutumia vyombo vya Dola.
Kwa mantiki hiyo basi, nimepata wazo kwamba inawezekana kabisa kuanzisha utaratibu wa kumshtaki huyu mtu kwenye Mahakama za kimataifa kwa ku-violate haki za Binadamu kulingana na Universal Declaration of Human Rights (1948).
Wataalamu wa sheria hapa JF mnaombwa kutoa mwongozo juu ya hili.
Wakuu wangu, naomba kuwasilisha hoja.