Waufukweni
JF-Expert Member
- May 16, 2024
- 4,393
- 14,498
Peter Madeleka, amekosoa utendaji wa Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP) na jeshi la polisi, akidai kuwa mchakato wa utoaji haki nchini umejaa migongano ya kisheria na matukio yanayovunja utu wa binadamu.
Soma: PostGE2025 - Rais Samia: Huko Mahabusu kuna watu hawana hatia, wanafungwa kwa kesi ya kubambikiwa tu
Akizungumza na Jambo TV leo, Januari 14, 2026, Madeleka amerejea kauli ya Rais Samia Suluhu Hassan aliyoitoa jana Jijini Dodoma kuhusu kukerwa na kesi za kubambikiwa. Madeleka amesema kama kauli hiyo ingechukuliwa kwa uzito wa kiutendaji, watu wote wenye kesi za uongo wangepaswa kuwa wameachiwa huru kufikia leo asubuhi.
Wakili huyo ametoa mifano ya kustaajabisha ya ukiukwaji wa taratibu, akitaja tukio la polisi kumpima mkojo mtuhumiwa wa kosa la "uchochezi," jambo ambalo amesema halina uhusiano wowote wa kisheria wala wa kitaalamu.
Soma: PostGE2025 - Rais Samia: Huko Mahabusu kuna watu hawana hatia, wanafungwa kwa kesi ya kubambikiwa tu
Akizungumza na Jambo TV leo, Januari 14, 2026, Madeleka amerejea kauli ya Rais Samia Suluhu Hassan aliyoitoa jana Jijini Dodoma kuhusu kukerwa na kesi za kubambikiwa. Madeleka amesema kama kauli hiyo ingechukuliwa kwa uzito wa kiutendaji, watu wote wenye kesi za uongo wangepaswa kuwa wameachiwa huru kufikia leo asubuhi.
Wakili huyo ametoa mifano ya kustaajabisha ya ukiukwaji wa taratibu, akitaja tukio la polisi kumpima mkojo mtuhumiwa wa kosa la "uchochezi," jambo ambalo amesema halina uhusiano wowote wa kisheria wala wa kitaalamu.