Mhache
JF-Expert Member
- Jun 20, 2008
- 345
- 24
Nimejiuliza mengi kuhusiana na hizo fedha zinazorejeshwa serikalini bila kupata jibu la matumizi yake. Je hizi fedha zinatumika kwa shughuli gani au kwa manufaa ya nani? Isije ikawa zinaingia mifukoni mwa wachache wajanja. Kama ndio hivyo sioni haja ya kuzirudisha nchini. Naomba mwenye kujua matumizi ya fedha hizo anijuze.
Ushauri wangu ni kuwa ili kuondoa dukuduku, fedha hizi zingeweza kutumika kujenga kipande cha kilomita kadhaa za barabara ili iwe ni kumbukumbu, hata mtu akiuliza jinsi fedha hizo zilivyotumika inakuwa rahisi kujibu. Mimi binafsi nina hamu ya kujua matumizi ya fedha hizo.
Mkereketwa wa kujua ukweli.
Ushauri wangu ni kuwa ili kuondoa dukuduku, fedha hizi zingeweza kutumika kujenga kipande cha kilomita kadhaa za barabara ili iwe ni kumbukumbu, hata mtu akiuliza jinsi fedha hizo zilivyotumika inakuwa rahisi kujibu. Mimi binafsi nina hamu ya kujua matumizi ya fedha hizo.
Mkereketwa wa kujua ukweli.