Pascal Mayalla
Platinum Member
- Sep 22, 2008
- 50,440
- 113,448
Mkuu Sikonge, asante sana kunifungua macho!, kusema ukweli usilolijua ni kama usiku wa giza!. Kwa akili yangu fupi, nilipoona imeandikwa "tester" "not for sale", nikajua kwa vile tester lengo lake ni ku taste tuu na sio chakula lenyewe, nikajua hizi tester, wameweka ladha tuu ya kuonjeshea, hivyo haiwezi kuwa tamu kama chakula yenyewe!.Pasco,
Basi naona hufahamu vizuri mambo ya PERFUME. TESTER siku zote ni kwa ajili ya Promotion na huwa wanazitengeneza chache kwa ajili ya kuzigawa/kuziuza kwa bei nafuu. Wakati mwingine Wasambazaji wanaziiba na kuziuza badala ya kuwauzia kwa bei nafuu wanunuzi wa JUMLA au Wasambazaji wengine.
Hizi TESTER ndiyo zenye QUALITY ya juu ili kuvuta mteja. Ndiyo maana majina makubwa unakuta hata TESTER hawana au wanazo chache sana. Ila kusema ukweli, ukiona mtu anauza TESTER basi ujuwe hizo zimeibiwa sehemu kwani hazitakiwi KUUZWA ila kwa ajili ya watu kujaribu. Na ili iwe hivyo, basi lazima iwe quality ya juu ili watu wazipende. Huwezi kumuwekea mtu SAMPLE mbaya maana akishaonja tu, anakimbia. Inabidi ujitahidi UPIKE vizuri sana chache kama kivutio na wakipenda, ndiyo wanakuja kwenye hizi MASS PRODUCTION ambazo wewe ndiyo unafikiri ni HIGH Quality.
Nirudie tena, upungufu wa bei haimaanishi ni ubaya wake kwa sababu kubwa kwamba hizo ni kwa ajili ya kujaribia na si KUUZA. Watu huwa wanazikwapua na kuuza. Ni sawa na SINGLE za miziki kwa ajili ya Promotion ambazo hupelekwa kwenye Maradio na kwa ma DJ kwenye Madisco. Wakati mwingine wengine huziuza kwenye minada wakati ni makosa. Na kuna watu hununua hasa wanaokusanya miziki kwani humo unaweza kukuta wimbo fulani ambao upo hapo tu na ubora wake upo juu kwani Mass Production haijaanza kufyatua.
Sasa nitazinunua hizo tester kwa moyo mkunjufu!.
P.