Pengo: Nimesamehe


Kama hayana uhusiano kwani wito wa mchungaji gwajima polisi ulikuwa wa nini? si walisema kwa kumtukana pengo sasa mtukanwa amesema amesamehe polisi watamuhoji wa tuhuma zip unless Kama wana kitu nyuma ya pazia
 
Hata kama hajatoa since ameishamsamehe anajukumu la kwenda kuifuta ,ili kujiweka katika nafasi nzuri zaidi.Hasa kwa vile yeye kama kiongozi wa dini na anajua umuhimu wa kusamehe mara sabini wa sabini.

well said maana lolote litalotokea kwa gwajima lazima jamii itamhusisha mwadhama
 
je amesamehe tuuu ... Vipi mpango wa kuwaunga mkono maaskofu wenzake katika msimamo wa katiba mpya.
 
hata kama hajatoa since ameishamsamehe anajukumu la kwenda kuifuta ,ili kujiweka katika nafasi nzuri zaidi.hasa kwa vile yeye kama kiongozi wa dini na anajua umuhimu wa kusamehe mara sabini wa sabini.

anafutaje
 
Pengo anatakiwa asamehewe sio asamehe, mimi ni mkatoliki lakini huu unafiki we Pengo nimeukataa. amekuwa msaliti kwa waumini wake, Pesa ambazo zingetumika kuwahudumia maskini zimeibiwa na watu wachache kupitia benki yake na bila shaka kuna baraka yake.

Sasa wananchi wanataka katiba itakayowaondoka kwenye utumwa huu wa viongozi dhalimu yeye akiwa kama askofu anatengana na wenzie anaungana upande wa wanyonyaji.

Kwa mawazo yangu Pengo ni kama wale maaskofu waliounga mkono mauwaji ya kimbari kule nchi jirani. badala ya kuwahurumia wananchi yeye anaangalia maslahi.

HUYU ANATAKIWA AOMBE MSAMAHA KWA USALITI WAKE, SIO UNAFIKI WA KUSEMA AMESAMEHE
 

Kweli kabisa!
 

Kaiyaibisha madhabau kabisa
 
Kama hayana uhusiano kwani wito wa mchungaji gwajima polisi ulikuwa wa nini? si walisema kwa kumtukana pengo sasa mtukanwa amesema amesamehe polisi watamuhoji wa tuhuma zip unless Kama wana kitu nyuma ya pazia



Kwani Aliyepeleka Kesi mahakamani ni nani?

na kama PENGO Hajashtaki Sasa GWAJIMA Anatuhumiwa na nini? au anahojiwa kwa lipi?

Something bhind the Scene
 
Gwajima or whatever he calls himself ni kumdharau na kumpuuza. Amepatwa na dengue baada ya kuambiwa aeleze chanzo cha utajiri wake. Kuna kitu zaidi ya sadaka.

mpiga tumba yule alijua wale wajinga anaowakusanya nakuwapiga fix watakuwa na impact kumbe hakuna,mtu anajiita askofu hata theology haijui,ujinjilisti wasiku mbili nakukariri vifungu vya biblia wajiita maaskofu mara Mungu kawaotesha,sasa mbona Mungu hakumtumia malaika waje wamrescure huko,eti anajitapa na kujifananisha na Yesu eti haogopi mahakama..Sasa mtu haja selo hajaiona kasha zimia
 

JAKAYA nae amekosea kuipamba KATIBA YAO eti ni nzuri hivyo wananchi wasifanye makosa waipigie NDIO. Na maaskofu kuipigia debe la HAPANA je ni kosa?
 
kwanza niheshimu hoja yako. Pia nimshukuru cardinal pengo kwa msamaha wake, ameonesha mfano mwema kama kiongozi wa kiroho, tofauti na pale kama azngekaa kimya. Serikali inamajukumu yake ya kuweka usalama na mtangamano baina wananchi na jamii kwa ujumla. Mie nadhani serikali iendelee na taratibu zake ila bila kumuonea, imtendee haki kwa kile aliicho fanya.
 
sio kusamehe tu na yeye ameomba msamaha wakristu kwa kutusaliti??..yeye ni msaliti,awaombe msamaha maaskofu wenzie kwa usaliti huu mkubwa na kufanya kazi isiyo yake
mwenzio kazimia wewe unaendelea! Shauri yako.
 
Gwajima kadinali pengo ni baba wa kiroho dunia nzima inatambua hivyo sio kama wewe ambaye hata huo uaskofu ulijipa mwenyewe. Angalia sasa umepigwa fimbo na mungu. Hata kama kad pengo alikosea kwa mtazamo wako hakustahili kutukanwa hadharani namna ile. Jifunze kuwa si kila mtu unaweza kumtukana na huo uaskofu wa kujipa. Mshukuru sana pengo ametoa msahama kwako vinginevyo ingekuwa kwaheri. Usimchezee mungu gwajima...ugua pole.
 
Halafu kumbe hata Cardinal Pengo ,Gwajima mwenyewe hamfahamu....(nimem quote kutoka kwenye kauli yake ya kumsamehe) so Gwajima ni opportunistic anataka kupanda chati kwa kumtukana Pengo
Katika hali ya kawaida maneno ya Gwajima kwangu ni uthibitisho tosha kabisa wa busara zake na tukio la kumkula mke wa mbasha
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…