Pengo: Nchi imeoza!

Pengo: Nchi imeoza!

Huku tunakokwenda hakufai. Nitatoa mfano.

Mie kama mtoto wa kiislam sitakiwi kula nguruwe, dini inasema ni haramu. Kuacha kwangu kula nguruwe sio kwa sababu niko allergic nayo, au ninaumwa. The decision is completely based on on faith kwamba nikila kiti moto ninapata dhambi. I stopped reasoning about manufaa ya kiti moto like bei yake rahisi kuliko mbuzi, au ng'ombe, pia kiti moto kina protein za kutosha. Hizo zote faida za kiti moto sizifikirii kwa sababu naogopa Jehanamu. Essentially my faith has hijacked my own reasoning power.

My point is, hawa viongozi wa dini wakianza kuongelea siasa--they are subliminally imposing faith mandate for their waumini to follow what they are preaching, in this time sio Yohana mtakatifu tena bali ni siasa. Wakatoliki are soon going to give up their reasoning power and vote for whoever Kardinali Pengo is endorsing between those lines. Not because they want to, but because Pengo said that is what GOD and Jesus wants to. That is what Waraka is intentionally supposed to be interpreted na waumini.

It is a very dangerous trajectory for our country because once the debate is shifted to udini, the risks for conflict will increase and we are already masikini--the last thing we want is people to be voting in 2010 because of dini au ukabila. Unfortunately when shit hit the fan kardinali Pengo anakwenda zake Vatican kutulia na kutuachia msala nchini kwetu.

Ya Kaisari muachie Kaisari Kardinali Pengo, huko unakotupeleka hatutaki.

Mfano wa kiti moto sio relevant. Waraka wa kanisa hauko dini-specific. Kama utakuwa umeusoma utaona unazungumzia kuwa na viongozi waadilifu. Shida yetu ni kuwa tunapenda sana kurukia mambo juu juu na kufanya conclusions based on who said what! Nani zaidi ya fisadi asiyekubaliana na ukweli kwamba nchi yetu imekosa uongozi adilifu? Hakuna popote katika waraka panapoelezea dini ya mtu mwadilifu. Kinachozungumziwa hapa ni wasifu wake.

Kama waraka, mwongoze, or any other document itakuwa ina-influence wananchi kumchagua kiongozi wa dini au dhehebu fulani, jua kwamba document hiyo na wanayoieneza ni wapotoshaji. Lakini kama inatuelimisha kuhusu sifa za watu safi wa kutuongoza jinsi ya kutawala raslimali zetu ili zitufae kwa usawa, hiyo document imechelewa sana kutufikia. Mimi siwezi kusema eti huu usanii ulioko kwenye utawala wa sasa unasababishwa na dini? Hata kidogo. Ni uongozi mbovu tu. Kama ndivyo tunahitaji nini basi? Dini bora zaidi? Hata kidogo! Tunahitaji viongozi wasafi, imara, shupavu wa kutawala na kuongoza kwa dira.

Hata kabla ya Pengo kusema tulishajua kuwa nchi imeoza. Itakuwa ni kujifanya vipofu kufanya ufisadi wetu mitaani huko halafu jumapili/ijumaa tunavaa suti/kanzu zetu na kujifanya tuko kanisani eti tunaabudu. Kidini tunaamini wenzetu tunaoishi nao ndio sura na mfano wa Mungu, kumbe ufisadi tunaowafanyia wenzetu tunamfanyia Mungu halafu tunajifanya tunampenda, si ndio unafiki huo? Sasa Pengo akilikemea hilo kuna ubaya gani?Maisha yetu ni pamoja na shughuli za siasa. Dini inaongoza maisha yetu yote. Hivyo siasa ni subset tu ya dini ingawaje iko huru kujiendesha yenyewe. Infact, uadilifu, upendo, kupenda usawa, huruma, na yote mazuri hutoka kwa roho wa Mungu. Kiongozi mwenye sifa hizo lazima awe mwumini wa dini fulani. Kama hana dini, ni wachache sana utakuta wenye ubinadamu.

Nchi imeoza, someni waraka na muufanyie kazi kwa manufaa ya nchi. Acheni ubinafsi, watu wanateseka na umaskini, wanakufa kwa kukosa huduma muhimu kwa sababu ya wachache kujilimbikizia utajiri - ndio ufisadi huo.

Hivi mbona hamkupinga wakati viongozi wa dini walipomfagilia Kikwete alipochaguliwa kuwa ni chaguo la Mungu? Chaguo la Mungu limebadilika baada ya mtumishi kushindwa kuwatumikia watu wake sasa hamtaki tena kuupokea ufunuo huo, kulikoni??
 
all in all...mie nafurahia hili vuguvugu la NYARAKA na MIONGOZO....natamani sana UDINI uote mizizi kisha TUPIGANE VITA vya udini au hata usiasa na ukabila ...KISHA MAENDELEO YA KWELI YAJE NCHINI MWETU KWA WATAKAOBAKI...kuliko kuendelea kuchekacheka na wapuuzi wachache wananufaika na rasilimali zetu.

NDIOOOO....kwani ni nchi gani iliyoendelea duniani ukianzia hiyo USA ambayo haikuwaua/kuuana/ kumwaga damu NDIPO IKAPATA MAENDELEO YA KWELI?

WATANZANIA acheni uoga wa kitoto...RWANDA NA BURUNDI WALITIANA ADABU NA WAMEANZA KUENDELEA KWA KASI...sie tunajivunia uhuru/amani na upendo ambavyo ki-halisia ni NIDHAMU YA WOGA NA KUOGOPANA...matokeo yake wapuuzi wachache aka MAFISADI wanatufanya watz wote wapumbafu na wapuuzi.

NO WAR...NO REAL PC N HARMONY..NO CIVILISATION/MAENDELEO YA KWELI at all.

nb:- ni maoni yangu na nasikitika kuwaambieni UKWELI na UKWELI TUPU watanzania wenzangu...EHEE MWENYEZI MUNGU NISAIDIE.

Unachokizungumza hukijui ndugu yangu, Mungu akusamehe. Ingekuwa kuuana kunaleta maendeleo sisi ndio tungekuwa wa kwanza. Hivi unajua ni watu wangapi wanakufa nchi hii kwa matatizo mbalimbali ya kushindwa kujikimu? Njaa, maradhi, ajali, na uzembe mbalimbali? Kumuua mwenzio sio lazima umpige risasi tu ndugu. Ukiteka kilicho halali yake ukajitwalia, yeye aka-starve akafa, hujamwua?

Nakuomba ufikirie tena.
 
Ni kweli Pengo kasema ukweli na kukemea ufisadi hapa hakuna siasa ni kila mtu sasa hasa kumbuka maskini ambao every day wanaomba washushiwe baraka na huyo mungu wakati watu waitafuna nchi na kukimbilia makanisani kusali. Hatuwezi kuombea nchi wakati maskini wanaibiwa.
 
Wadau;
Tuna matatizo ya utawala bora na sera zilizopitwa na wakati au potofu. Huo ndio ukweli na wala sijapingana nao. Na waraka sijausoma ila katika kuuperuzi na kubaliana na nyie kwamba Kardinali hajachagua farasi katika mbio. Kanisa is simply outlining hali ya kisiasa nchini kwetu. Ukiangalia juu kwa juu, yeah waraka looks clean and ni mwongozo kwa waumini. I get it. Kanisa sio wapumbavu, they will not directly choose and endorse chama fulani. Wanachofanya ni kuwapeleka wakatoliki mtoni, washindwe wenyewe kunywa maji and that is exactly what they are doing. And if you disagree with that then u have to be so naive'.

Kanisa and Pengo knows that SOME waumini will took waraka as mwongozo kutoka kwa Baba mtakatifu not to vote for mafisadi. And that is the intent of it. Tatizo sio kwamba nakumbatia mafisadi, our democracy is too fragile to start incorporating faith in it. Watu wapige kura sio kwa sababu ya imani zao za kidini bali kwa matakwa yao ya duniani.
 
Muadhama Cardinal Polycarp Pengo ... tuna separation of church and state ... remember?

Makanisa na Misikiti inakemea maovu (dhambi) Kwa kuwa ufisadi ni dhambi na imeandikwa kwenye vitabu vitakatifu ni dhahiri Makanisa na Misikiti wanaowajibu wa kukemea Ufisadi(Dhambi) hapo hakuna cha separation other wise haina maana ya kuwa na makanisa na misikiti
 
Kulingana na gazeti la Majira la leo ASKOFU wa Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, Muadhama Polycarp Kardinali Pengo ameibuka tena na kutangaza mapambano mapya dhidi ya mafisadi huku akidai nchi imeoza na kamwe kanisa halitakaa kimya na kulea hali hiyo.

  • Asema kamwe kanisa halitakubali kunyamaza.
  • Asema watapambana na ufisadi hadi mwisho.
  • Aapa kupambana na yeyote anayetetea uovu.
  • Asema Katoliki haliandai mgombea Urais mwaka 2010.
  • Adai anayeogopa waraka wa Kanisa ni Fisadi.



MI naona Pengo agombee ubunge maana kaamua kuingia kwenye siasa, amesahau there must be separation of power between state and other institution though kuna check and balance lakini si kuingia ndani kiasi kwamba unaonekana unachochea malumbano kwa kigezo cha misimamo ya dini, kama mnataka kanisa kuingilia mambo ya siasa pelekeni mswada bungeni basi ujadiliwe, harakati zake can take him no where coz they lack merits
 
Makanisa na Misikiti inakemea maovu (dhambi) Kwa kuwa ufisadi ni dhambi na imeandikwa kwenye vitabu vitakatifu ni dhahiri Makanisa na Misikiti wanaowajibu wa kukemea Ufisadi(Dhambi) hapo hakuna cha separation other wise haina maana ya kuwa na makanisa na misikiti


thats gud, lakini dhambi hiyo ina maeneo yake ya kukemewa kama dini inaingia hapa, kemea kanisani au msikitini au hata hadharani mambo ya kutoa miongozo na waraka that is beyond your jurisdiction, na kuanzisha malumbano na wana siasa kwakweli haileti maana kwa kiongozi wa kiroho kama pengo, hata wakati wa mitume ufisadi ulikuwepo lakini hukusikia mtume yeyote kutoa waraka au mwongozo zaidi ya kutumia maandiko ya vitabu vitakatifu..mi naamini Injili imebeba kila kitu vilevile Quran hata Torati vyote vimekataza mambo ya ufisadi,kwanini wasivitumie vitabu mpaka waje na yao mengine, je tuseme hawavielewi vitabu hivi vimeshuka kwa kazi ipi..tafakari mkuu
 
Mkuu ni kweli kuna separation ya politics na religious matters. Sina hakika kama maana yako ya Church and State, ina maana Mosque yenyewe haiwi separated na state matters, which in many cases it may seems so.

Lakini where do you draw that line. Mambo ya dini yanaishia wapi na ya siasa yanaingia wapi, ukiangalia kwa undani utaona kuwa ni mstari ambao umechorwa hewani tu. Sioni ubaya kwa kiongozi wa msikiti au kanisa kusema hatutaki viongozi wabovu, mtu akiwa mwenyekiti wa serikali ya mtaa, diwani, mbunge,waziri au rais anaongoza watu wote bila kujali yeye ni mwanadini au la. Kwa hiyo kama uongozi wake haufai unamwathiri moja kwa moja hata mtu wa dini. Kama serikali inalinda na kupalilia maovu, misikiti na makanisa yatakuwa yanafanya kazi bure, yaani kufinidhs amorals wengine wanafanya tofauti. Wakati wao misikitini na makanisani wanapreach honesty, itakuwa ni upuuzi kama watachekelea ufisadi.

Makamba most of the time amekuwa akiquote Qoran na Biblia anapokuwa kwenye kazi za siasa. Alipokuwa RC hata alikuwa anakwenda misikitini kama RC, kumbuka mwembechai au pale kwa mtoro wakati wanachapana bakora ndani. Mbona yeye hakuwahi kukosolewa kuwa anachanganya siasa na dini?

Are we being hypocritical, or is our system hypocritical? Why should politicians mix politics and religion and why shouldn't clergymen mix religion and politics. Inawezekana Pengo hajui kama dini na siasa haviwezi kuchanganywa?

Bongolander thank you for a very well good point. Tunaposema tutofautishe dini na siasa haina maana kwamba kwamwe dini isikemee maovu hata kama ni ya kisiasa. Vile vile tunaposema siasa isiletwe kwenye dini hatuna maana dini ziachiwe uhuru kabisa bila kuingiliwa hata katika mambo ya kipuuzi. Kama tunavyosema there is no complete freedom of expression na hapa mantiki ni hiyo hiyo there can not be complete separation of religion and politics. Hakuna. Historia ya Biblia hasa agano lake inaonyesha muingiliano mkubwa wa dini na siasa

Tunaambiwa kwenye miaka ya 1960 au 1970 Mwalimu Nyerere alilipiga marufuku shirika la dini moja lililokuwa linawaambia waumini wake wasifanye kazi sehemu za Sumbawanga! Juzi juzi masalia wasabato became a nuisance at the airport and the authorities had to intervine. Ufisadi wa pesa na ule wa kura pamoja na uchoyo usio kifani na ulafi ni dhambi. Hakuna dini yoyote inayoshabikia mambo haya inagawa dini nyingine hazikemei uovu huu. Kwa nini? Your guess is as good as mine. Dini hazipaswi kushabikia vyama vya siasa au mtu, n.k

Anochokifanya Pengo na kanisa lake ni kukemea uovu katika jamii na kama alivyosema jana kiongozi yeyote aliye muadilifu waraka wa kanisa au kelele dhidi ya uovu wowote ule "haumusu". Ni wale tu wanaojishuku wanaopiga kelele za kuchanganya dini na siasa.
 
Hapa naona siasa inatumiwa kama kivuli cha kuficha uovu wa wachache na kuwakandamiza/kunyonya walio wengi.

Kila mara tunaambiwa tusichanganye siasa na dini, siasa isichanganywe na utumishi wa umma, siasa isiingizwe kwenye taasisi za elimu ya juu n.k. Kubwa la kujiuliza ni kuwa hao wanaojihusisha na siasa wanatoka kwenye jamii ipi?

Je wanasiasa wanapokuwa na mienendo ambayo ni kinyume na matarajio ya jamii wataulizwa ama kukemewa na nani?

Matarajio ya wengi ni kuona wanasiasa wanajishughulisha na mambo yanayohusu uboreshaji wa maisha ya watu wa kawaida lakini kwa Tanzania imekuwa ndivyo sivyo na hapo ndipo makundi yanayotakiwa kujitenga na siasa yanapolazimika kuingilia kati na kuwapigia kelele wahusika vinginevyo nchi itateketea
 
Sasa nani aliyoiozesha hii nchi kama si kanisa?. kwani kanisa ndio linalotawala tanzania kwa nyuma ya pazia
 
Ni kweli nchi imeoza kiasi cha akinapengo kushindwa kuendesha ibada na kuingia katika ulingo wa kisiasa.mafisadi wamekuwa mbele wakidai kupambana na ufisadi ambao kimsingi hawaonekani wanaopambana nao.Inawezekana wanapambana na vivuli vyao.kwani kila tukiwauliza tajeni mafisani wananyamaza.ama kweli nchi imeoza
Nakuunga mguu kwani Pengo kashindwa kuendesha ibada kama ulivyosema,kwa taarifa nyepesi nilizonazo sasa anajiandaa kugombea ubunge mwaka 2010,mambo hayo!
 
Nakuunga mguu kwani Pengo kashindwa kuendesha ibada kama ulivyosema,kwa taarifa nyepesi nilizonazo sasa anajiandaa kugombea ubunge mwaka 2010,mambo hayo!

Ha ha ha..mi niliskia anakitaka kiti cha Kikwete, labda kashachukua fomu za CCM maana naskia zimeshatolewa..😀
 
Kulingana na gazeti la Majira la leo ASKOFU wa Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, Muadhama Polycarp Kardinali Pengo ameibuka tena na kutangaza mapambano mapya dhidi ya mafisadi huku akidai nchi imeoza na kamwe kanisa halitakaa kimya na kulea hali hiyo.

  • Asema kamwe kanisa halitakubali kunyamaza.
  • Asema watapambana na ufisadi hadi mwisho.
  • Aapa kupambana na yeyote anayetetea uovu.
  • Asema Katoliki haliandai mgombea Urais mwaka 2010.
  • Adai anayeogopa waraka wa Kanisa ni Fisadi.
Kwa akili yako mtu ambaye amechaguliwa na waishio nje ya Tanzania atawezaje kufundisha demokrasia hapa Tz?Hao mapengo,ooh samahani namaanisha maaskofu,makadinali wa raia wa roma(roman catholic) wote wanachaguliwa/kuteuliwa na papa ambaye haijui vyema Tz,kwahiyo utaona hilo kanisa lenyewe halina demokrasia waumini wake wanaletewa mamluki tuu toka Roma bila ridhaa yao leo eti hao mamluki waje kufundisha demokrasia hapa bongo watawezaje wakati huko kanisani hakuna demokrasi?Acheni kushabikia mambo ya kijinga kwani hao mamluki sorry naamanisha maaskofu na makadinali raia wa roma(roman catholic) wanatetea unga wao tuu na si kuwatetea watz kama kweli wanataka demokrasi basi wajivue huo ulaji na waanze sasa kuchaguana hapa Tz!
Aibu,ningekuwa huko ningetoka mapema!Yaani watu wanaletewa watawala na watu walio nje ya nchi yao,maskini yaani Dogmaship imewatawala maskini.
 
Muadhama Cardinal Polycarp Pengo ... tuna separation of church and state ... remember?

Unaujua umuhimu wa vyombo vya dini katika kuendesha serikali iliyopo madarakani?.
 
Hamna ubaya wowote wa Pengo alichofanya.Tusisahau mapinduzi ya Madikteta huko Philipine yaliyokuwa yanafanywa na Kanisa Katoliki.
Kwangu ni hatua nzuri ili serikali ijifunze kuwajibika zaidi na ione jinsi gani nchi ilivyoharibika.
Ni muhimu na lazima kanisa nalo lishiriki katika ujenzi wa taifa.
 
Kwa akili yako mtu ambaye amechaguliwa na waishio nje ya Tanzania atawezaje kufundisha demokrasia hapa Tz?Hao mapengo,ooh samahani namaanisha maaskofu,makadinali wa raia wa roma(roman catholic) wote wanachaguliwa/kuteuliwa na papa ambaye haijui vyema Tz,kwahiyo utaona hilo kanisa lenyewe halina demokrasia waumini wake wanaletewa mamluki tuu toka Roma bila ridhaa yao leo eti hao mamluki waje kufundisha demokrasia hapa bongo watawezaje wakati huko kanisani hakuna demokrasi?Acheni kushabikia mambo ya kijinga kwani hao mamluki sorry naamanisha maaskofu na makadinali raia wa roma(roman catholic) wanatetea unga wao tuu na si kuwatetea watz kama kweli wanataka demokrasi basi wajivue huo ulaji na waanze sasa kuchaguana hapa Tz!
Aibu,ningekuwa huko ningetoka mapema!Yaani watu wanaletewa watawala na watu walio nje ya nchi yao,maskini yaani Dogmaship imewatawala maskini.

Pole sana mkamua kinyesi maiti. Najua mzizi wa yote haya ni kukataliwa kwenu kwa free lunch..ha ha ha

Jazba na chuki hazitatua matatizo yenu na zaidi yatayaongeza tu.

Kwa juhudi kubwa umejaribu kujadili mtu badala ya ujumbe anaouleta. Kuishiwa hoja kwako kwa namna hii kunaitwa ad hominem.

Pili unasahau kuwa msingi wa hoja zote hizi ni waraka wa wakatoliki kuelekea uchaguzi wa 2010. Waraka huu umeandaliwa na wataalamu wakatoliki, na sio maaskofu kama kichwa chako kidogo kinavyoshindwa ku-grasp, hivyo wote mnaoushambulia waraka na kuuhusisha na Pengo au yeyote kwa namna moja mnadhihirisha mlivyo na vichwa vigumu na mlivyo mahodari wa kudandia matreni kwa mbele, ila sisi wenye busara tunawaangalia tu mkipiga makasia pasipo na maji.

Pengo anakemea ufisadi ili kutetea unga wake?! are you serious ?Unga kutoka kwa nani? ha ha ha..uko shallow kinyama, ila endelea tu ivoivo labda itakusaidieni kupunguza maumivu ya mahakama ya 'kazi' 😀 ..

Halafu unaleta suala la demokrasia kwenye kanisa, unasahau kuwa walioandika huo waraka wamechaguliwa ki-demokrasia, maana taasisi na makundi mbalimbali ya RC yana kanuni zake za kidemokrasia kwenye kuchaguana na hakuna kuchapana bakora kule ,kila kitu kinakwenda sawa bin sawia, hivyo hapo bana mkubwa umechemsha tena na tena na kuzidi kudhihirisha huna ulijualo.

Kwa kifupi, vyeo vya kidini vinaenda kufuatana na mambo ya imani. Na ndio maana hatuchagui mitume, mitume tunaletewa na Mungu.Hawa ni watumishi wa kiroho na vyeo vyao ni vya kiroho.
 
Back
Top Bottom